Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,759
- 7,573
Takribani watu 7,000 wanapoteza maisha yao kila saa, duniani. Takwimu hizi zinashtua, ila zinapaswa kutufanya tufikirie kwa kina kuhusu maisha yetu yajayo.
Takwimu hizo ni kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na Idara ya Idadi ya Watu ya Umoja wa Mataifa (UN DESA). Sababu za vifo ni nyingi.
Lakini swali kuu ni hili: Je, wewe ukifa leo, utaenda wapi?
Kifo hakigongi hodi. Kinaweza kuja bila taarifa, asubuhi au jioni, ukiwa barabarani au umelala.
Biblia inatuambia:
"Watu wamewekewa kufa mara moja, na baada ya hapo hukumu." (Ebr 9:27)
Fanya haraka, "ukate tiketi" ya kuingia mbinguni na kuikwepa hukumu ya moto wa milele. Tubu dhambi zako zote, umpokee Yesu Kristo moyoni mwako kwa imani, awe Bwana na Mwokozi wako. Yesu ndiye njia pekee ya kutufikisha mbinguni(Yn 14:6).
Takwimu hizo ni kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na Idara ya Idadi ya Watu ya Umoja wa Mataifa (UN DESA). Sababu za vifo ni nyingi.
Lakini swali kuu ni hili: Je, wewe ukifa leo, utaenda wapi?
Kifo hakigongi hodi. Kinaweza kuja bila taarifa, asubuhi au jioni, ukiwa barabarani au umelala.
Biblia inatuambia:
"Watu wamewekewa kufa mara moja, na baada ya hapo hukumu." (Ebr 9:27)
Fanya haraka, "ukate tiketi" ya kuingia mbinguni na kuikwepa hukumu ya moto wa milele. Tubu dhambi zako zote, umpokee Yesu Kristo moyoni mwako kwa imani, awe Bwana na Mwokozi wako. Yesu ndiye njia pekee ya kutufikisha mbinguni(Yn 14:6).