Kama kichwa cha mada kinavyojieleza. Nafikiri kuna umuhimu mkubwa kwa serikali kuliangalia suala la umri kwa wananchi wake ili kupunguza au kuondoa kabisa sintofahamu na maswali hapo baadae.
Nasema hivyo nikiwa na maana gani, yaani kwa mfano kama sasa walivyotangaza kwamba mwanafunzi kudahili kujiunga na kidato cha Tano mwisho ni mwenye miaka 25.
Kwahiyo hata kwenye matangazo ya ajila au kujitolea yawe yanashabihiana kwa kuweka ukomo wa kiumri kwa kuangalia vigezo vya kiumri kwenye Elimu. Mfano mwingine mwaka jana vigezo kwa mwanafunzi aliemaliza kidato cha sita kujiunga na JKT ilikuwa mwisho miaka ishirini na mitatu (23).
Sasa hapa tayari kunakuwa na ukinzani yaani wa kiumri nikama kunakuwa vile hakuna ushirikiano kati ya idara moja ya serikali na nyingine *ukinzani "umri kujiunga kidato cha tano mwisho miaka 25 na umri wa mwisho kujiunga na JKT kwa aliyehitimu kidato cha sita ni miaka 23".
Nafikiri hili serikali italiangalia na kulirekebisha kwa njia bora zaidi.
NAWASILISHA
Nasema hivyo nikiwa na maana gani, yaani kwa mfano kama sasa walivyotangaza kwamba mwanafunzi kudahili kujiunga na kidato cha Tano mwisho ni mwenye miaka 25.
Kwahiyo hata kwenye matangazo ya ajila au kujitolea yawe yanashabihiana kwa kuweka ukomo wa kiumri kwa kuangalia vigezo vya kiumri kwenye Elimu. Mfano mwingine mwaka jana vigezo kwa mwanafunzi aliemaliza kidato cha sita kujiunga na JKT ilikuwa mwisho miaka ishirini na mitatu (23).
Sasa hapa tayari kunakuwa na ukinzani yaani wa kiumri nikama kunakuwa vile hakuna ushirikiano kati ya idara moja ya serikali na nyingine *ukinzani "umri kujiunga kidato cha tano mwisho miaka 25 na umri wa mwisho kujiunga na JKT kwa aliyehitimu kidato cha sita ni miaka 23".
Nafikiri hili serikali italiangalia na kulirekebisha kwa njia bora zaidi.
NAWASILISHA