Umuhimu wa pesa kwa mwanaume

Umuhimu wa pesa kwa mwanaume

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
4,780
Reaction score
8,155
Mwanaume anakuwa mzuri akiwa na pesa.

Mwanaume anapendwa akiwa na thamani.

Mwanaume anaogopwa anapokuwa na mamlaka na ushawishi.

Mamlaka, thamani na ushawishi yanaleta mafanikio ya kipeasa, kwahiyo mtu mwenye mamlaka, mtu mwenye thamani na ushawishi, mtu huyo ana pesa, na huyu ndio mtu ambaye anauwezo wa kumpata angalau kila mwanamke anayemuhitaji.

Achana na dhana ya mwanamke kukwambia hana muda, mwanamke ana muda na anapatikana kwa urahisi sana bila shida yoyote.

Mwanamke anapatikana kwa urahisi bila usumbufu wowote kwa wanaume wawili, mwanaume anayempenda na mwanaume mwenye pesa. Kwahiyo ikitokea kila mara mwanamke anakwambia hana muda maana wa kuonana na wewe maana yake hakupendi, lakini pia huna hela. Kama mwanamke anajua una hela na mahitaji yake ya kipesa yatatimizwa bila changamoto yoyote, mwanamke huyo utampata muda wowote utakaomtaka hata kama hakupendi.

Sahau kuhusu hivyo visheria vyao wanavyoviwekaga kwa mwanaume, mara sijui mimi huwa sitoki usiku, hivyo visheria anawekewa mwanaume asiye na hela, ukiwa na hela mwanamke anakupa uhuru wa kuwa kwenye maisha yake muda wowote.

Tafuta pesa nyingi, kila kitu kuhusu wanawake na visheria vyao havitakuhusu, vitahusu wanaume wengine ila sio wewe.

Wanawake wanaweka sheria nyingi kwa wanaume wasio na hela na wanazivunja sheria hizo hizo kwa wanaume matajiri.

Wanaume wengi wanateseka kwenye mahusiano sio kwa sababu ni watu wabaya ila ni kwasababu hawana hela.

Hakuna mwanaume duniani ambaye mwanamke anamchukia na kumvunjia heshima kama mwanaume asiye na hela.

Mwanaume pekee masikini ambaye mwanamke anampenda, kumuheshimu na kumthamini ni Baba yake mzazi, yani mwanamke hanaga shida na umasikini wa baba yake mzazi ila umasikini wako unampa shida sana.

Kama mwanaume hakikisha unatengeneza pesa, halafu tengeneza hayo mahusiano yako, ila pesa iwepo. Kwa mwanamke linapokuja swala la pesa huwa anachanganyikiwa.

Kama kijana usihangaike sana na mapenzi, hangaika kutafuta thamani yako na kuwa na nguvu ya kiuchumi.
 
Ukweli mchungu.

Ila pia na Wanawake waelewe kuwa jinsi hela zinavyozidi ndio pia tunakuwa na uwezo wa kumiliki wanawake zaid ya mmoja.

Kwahiyo wachague wao,.
Walilie kwenye Range Rover na maisha mazuri huku mambo yao yakienda
Au wawe na wanaume wenye kipato cha wastan na kufurahia Maisha.

Umasikini hapana, tuupige vita kwa kupambana kwa namna yoyote ile.
 
Kwahiyo tutafute pesa kwa ajili ya wanawake? yaani tukiwaita waje wameshika chupi mkononi?

Ndugu yangu kama ni wanawake si lazima uwe na pesa ndo umpate, na ukitafuta pesa kwa ajili ya mwanamke utakuja kulia na pesa zako.

Ushauri wa bure, tafuta pesa kuboresha maisha yako, kuitengeneza familia yako, ikiwemo wazazi wako, waingie ndugu zako kutoka kwenye lindi la umasikini, wawezeshe mitaji wajikwamue hiyo ndio iwe maana ya kutafuta pesa.

Kumbuka mambo yote ni ubatili, kuna mtu ana wake wa nne lakini bado ana mchepuko, huwezi ridhika.

USIKOMAE KUTAFUTA PESA ETI KWA AJILI YA MWANAMKE UTAKONDA BUREE!
 
Kwahiyo tutafute pesa kwa ajili ya wanawake? yaani tukiwaita waje wameshika chupi mkononi?

Ndugu yangu kama ni wanawake si lazima uwe na pesa ndo umpate, na ukitafuta pesa kwa ajili ya mwanamke utakuja kulia na pesa zako.

Ushauri wa bure, tafuta pesa kuboresha maisha yako, kuitengeneza familia yako, ikiwemo wazazi wako, waingie ndugu zako kutoka kwenye lindi la umasikini, wawezeshe mitaji wajikwamue hiyo ndio iwe maana ya kutafuta pesa.

Kumbuka mambo yote ni ubatili, kuna mtu ana wake wa nne lakini bado ana mchepuko, huwezi ridhika.

USIKOMAE KUTAFUTA PESA ETI KWA AJILI YA MWANAMKE UTAKONDA BUREE!
Achana na hayo ya ndugu ...we ukipambana yeye anapambana na mbuye uje umsomeshee mtoto ake...Kuna wengine washawekeza kuwa maskini...hawajijali...wazazi unarudisha Kama fungu la kumi tu...
 
Achana na hayo ya ndugu ...we ukipambana yeye anapambana na mbuye uje umsomeshee mtoto ake...Kuna wengine washawekeza kuwa maskini...hawajijali...wazazi unarudisha Kama fungu la kumi tu...
Yote sawa mkuu, ila kumbuka umasikini ni mnyororo, asipotokea wa kuukata hautoki
 
Mwanaume anakuwa mzuri akiwa na pesa.

Mwanaume anapendwa akiwa na thamani.

Mwanaume anaogopwa anapokuwa na mamlaka na ushawishi.

Mamlaka, thamani na ushawishi yanaleta mafanikio ya kipeasa, kwahiyo mtu mwenye mamlaka, mtu mwenye thamani na ushawishi, mtu huyo ana pesa, na huyu ndio mtu ambaye anauwezo wa kumpata angalau kila mwanamke anayemuhitaji.

Achana na dhana ya mwanamke kukwambia hana muda, mwanamke ana muda na anapatikana kwa urahisi sana bila shida yoyote.

Mwanamke anapatikana kwa urahisi bila usumbufu wowote kwa wanaume wawili, mwanaume anayempenda na mwanaume mwenye pesa. Kwahiyo ikitokea kila mara mwanamke anakwambia hana muda maana wa kuonana na wewe maana yake hakupendi, lakini pia huna hela. Kama mwanamke anajua una hela na mahitaji yake ya kipesa yatatimizwa bila changamoto yoyote, mwanamke huyo utampata muda wowote utakaomtaka hata kama hakupendi.

Sahau kuhusu hivyo visheria vyao wanavyoviwekaga kwa mwanaume, mara sijui mimi huwa sitoki usiku, hivyo visheria anawekewa mwanaume asiye na hela, ukiwa na hela mwanamke anakupa uhuru wa kuwa kwenye maisha yake muda wowote.

Tafuta pesa nyingi, kila kitu kuhusu wanawake na visheria vyao havitakuhusu, vitahusu wanaume wengine ila sio wewe.

Wanawake wanaweka sheria nyingi kwa wanaume wasio na hela na wanazivunja sheria hizo hizo kwa wanaume matajiri.

Wanaume wengi wanateseka kwenye mahusiano sio kwa sababu ni watu wabaya ila ni kwasababu hawana hela.

Hakuna mwanaume duniani ambaye mwanamke anamchukia na kumvunjia heshima kama mwanaume asiye na hela.

Mwanaume pekee masikini ambaye mwanamke anampenda, kumuheshimu na kumthamini ni Baba yake mzazi, yani mwanamke hanaga shida na umasikini wa baba yake mzazi ila umasikini wako unampa shida sana.

Kama mwanaume hakikisha unatengeneza pesa, halafu tengeneza hayo mahusiano yako, ila pesa iwepo. Kwa mwanamke linapokuja swala la pesa huwa anachanganyikiwa.

Kama kijana usihangaike sana na mapenzi, hangaika kutafuta thamani yako na kuwa na nguvu ya kiuchumi.
Kwa mtu kama mimi ambae nilianza ujasiriamali ulofungua njia zingine katika maisha nikiwa na umri wa miaka 15, nakupa 5 za nguvu.
 
Back
Top Bottom