Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,410
- 119,112
Labda niwe na kichaa ninunue shati la 50000...
Labda niwe na kichaa ninunue shati la 50000...
Uko kama Mimi mkuuKuna watu wanaishi kwa maigizo. Anataka vazi kulingana na bei yake bila kujali uimara na unadhifu. Mwingine atataka vazi flani kisa kuna mtu fulani maarufu kavaa la aina ile. Ni kweli lakini kuna profession zinahitaji mavazi ya kipekee na yenye ubunifu wa hali ya juu kama vile waigizaji, wanamitindo na wanamuziki. lakini utakuta mtu labda ni mwalimu au mwanasiasa au ni mfanyabiashara basi ana complicate kwenye mavazi hadi anasahau kufuatilia mambo mengine, inafikia anasahau hadi majukumu yake.
Ila mimi sijui nikoje, sichaguagi kabisa mitindo wala siishobokei. ninachojali ni nguo safi, za heshima na zinazonisetiri. Amini usiamini...... hata nikikutana na mtu huwa siangalii kavaa namna gani au kavaa mtindo gani, labda awe uchi au nguo zake chafu ndio nitagundua. vinginevyo hata akiniuliza baada ya kuachana alikuwa kavaa nguo gani sitakumbuka.
Mi sina tatizo hata watu wakiamua kutembea uchi kama kwenye nudist colony.Sina tatizo kabisa na jinsi mtu aamuavyo kutumia pesa zake.
Matumizi ya pesa zake mimi hayanihusu kabisa.
Pesa ni zake na ana haki na uhuru wote wa kuzitumia atakavyo na apendavyo.
Kuna wengine wanapenda magari ya kifahari kama Rolls Royce na watanunua kila toleo.
Kuna wengine wanapenda Toyota Corolla na watanunua kila toleo.
Lakini yote hayo ni magari na yana uwezo wa kukutoa kutoka eneo A kwenda eneo B, C, D, na hata E.
Ni suala la mtazamo na mapenzi ya mtu.
Wewe kama unaona wenye kupenda kuvaa vitu vya anasa vya bei mbaya ni washamba au wenye kupenda kujionyesha na wenzio wanaweza kukuona wewe unayewaponda wanaopenda vitu hivyo vya anasa na bei mbaya unafanya hivyo kwa husda kwa sababu huna uwezo wa kuvinunua hivyo vitu na ili kujipa faraja unaona uwaponde kwa sababu kuwaponda huko kunakufanya ujisikie vizuri. Kuwaponda huko kunafidia ukosefu wako wa uwezo wa kuvinunua.
La msingi hapa ni kutambua tu kuwa watu tumetofautiana. Tuache watu waishi watakavyo na si kuhukumu hukumu kila mtu na kila jambo.
Mtu kuvaa nguo za anasa hakuathiri kwa namna yoyote ile maisha yangu [labda kama ninamwonea wivu na siwezi kuwa nacho alichonacho].
Zaidi ya hapo, live and let live.
Mi sina tatizo hata watu wakiamua kutembea uchi kama kwenye nudist colony.
Ili mradi wote tukubaliane mfadhaiko hakuna.
Nini kuvaa shati la bei mbaya.
Hahaha, kama una roho nyepesi hapo lazima unahama.Nakumbuka nikiwa sophomore niliamua kuishi off-campus.
Nikapata chumba kwenye nyumba ya maza mmoja hivi wa kizungu.
Kabla ya ku sign lease agreement akanifahamisha kuwa ana boyfriend wake ambaye ni nudist na mara moja moja huwa anakuja hapo kumtembelea.
Siku moja Ijumaa jioni natoka class ile naingia ndani tu nikakutana naye akiwa uchi kabisa.
Hahahaaaa....sikushtuka sana maana nilikuwa nshapewa heads up but still.....it was awkward.
I said to myself to each his own and kept it moving.
Mimi naishi ughaibunina sijaona umuhimu wa kuvaa mashati yenye milebo mikubwa, yawe ya bei kubwa au rahisi.Ukiishi ughaibun ndio utajua umuhimu wa kuvaa Designer.hata hao wakina Steve Jobs, Mark Zuckerberg,Bill Gates wanaonekana simple hila kiukweli nguo wanazovaa kama ni shati au Pullover sio za bei za chini,kuna Majina mengi sana ya nguo ghali kuliko hata hayo Gucci,na nembo zao si za kuonekana kwa mbali hila ukibahatika kuiona nembo ndio utajua kwamba hao matajiri wanavaa nguo ghali sana. Bill Gates awezi kuvaa shati la H&M au ZARA hata siku moja.
Aisee Una undugu na yule Nyani wa Marekani,kuna siku humu JF alisema "exactly words" khs nguo zenye label kubwa.Au ID Ime....Mahatma Gandhi aliuangusha Ufalme wa Uingereza kwa kueaongoza Wahindi wakatae kuvaa nguo za kigeni na kupenda kuvaa zao.
Binafsi moja ya kitu kinachoweza kunifanya nisinunue nguo ni kama ina m label mkubwa.
Nitajiona kama tangazo la biashara linalotembea.
Marekani kuna movement nzima kabisa.Aisee Una undugu na yule Nyani wa Marekani,kuna siku humu JF alisema "exactly words" khs nguo zenye label kubwa.Au ID Ime....
Marekani kuna movement nzima kabisa.
Inaendana na social consciousness, environmentalism, reduction of the carbon footprint etc.
Huko bongo - hata Marekani pia- kuvaa Nike kali inawezekana kukawa ujiko.
Lakini.
Mtu anaweza kukuambia hataki kuvaa Nike kwa sababu Nike ina exploit wafanyakazi wa "dunia ya tatu"kwa kuwalipa mishahara mbuzi wakati Marekani tunanunua viatu $ 140
Ona https://www.corporatecrimereporter.com/news/200/james-keady-and-the-coming-boycott-of-nike/
Mambo ya kawaida hayo.Juzi nikaingia kwenye store moja wanauza used shoes...nikaulizia bei ya kiatu Jordan cha mtoto wa miaka kama saba hivi. Bei £25, nikajisemea kimoyo moyo ikiwa ikiwa hichi cha mtumba bei hii...je kikiwa kipya!
HahaaaaaAisee Una undugu na yule Nyani wa Marekani,kuna siku humu JF alisema "exactly words" khs nguo zenye label kubwa.Au ID Ime....
Teh teh tehhhUko kama Mimi mkuu