Umri wa kustaafu Majaji upunguzwe hadi miaka 50

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,162
7,734
MAGAZETI ya Leo tarehe 5/5/2023 yameandika juu ya hafla ya kustaafu kwa majaji 3 wa mahakama kuu ya Tanzania, tunawapongeza kwa kulitumikia Taifa letu na tunawatakia maisha mazuri ya uraiani.

Jambo nililojifunza ni kwamba Majaji hao wanaonekana kuwa na umri mkubwa sana, nimejiuliza hivi Majaji huwa wanastaafu wakiwa na umri wa miaka mingapi?

Kwa kuzingatia kazi ngumu wanazozifanya nashauri umri wa kustaafu majaji upunguzwe uwe miaka 50.

Inaonekana Majaji wengi wamechoka kwa umri kuwa mkubwa lakini wapo kazini tu, idadi ya majaji wanaostaafu ni ndogo sana ukilinganiaha na idadi ya wazee waliopo makazini, jamani tubadilike, tuwapishe vijana.
 
70 yrs mkuu
Duh!!!

Nakumbuka Hayati JPM aliwahi kusema hivi;

" Nilikuwa namsikia mtalemwa mkurugenzi wa DAWASCO tangu nasoma shule Hadi Leo hii Mimi ni Rais bado mtalemwa yupo kazini!!!!" Baada ya kauli hiyo Rais alimuomba Mtalemwa astaafu na apishe watu wengine.

Hii inatuonyesha kuwa kuna watu/ viongozi hawajui hata umri wao wa kuzaliwa, wamezeeka bado wame ngangana tu!!! Hatari sana hii
 
Nafasi hizi zitangazwe watu waombe kutokana na weledi na hukumu zako za nyuma zisizo na shida zitumikazo km references.
Mishahara yao ikatwe kodi sisi tuu wakina kobeĺo.
 
nawakumbuka sana kina Jaji Lewis Makame, Jaji Nixon Chipeta, Francis Nyalali n.k

sasa hivi nadhani watafutiwe jina tofauti na jina la Jaji kutunza heshma za miamba wale wa sheria na hukumu
 
MAGAZETI ya Leo tarehe 5/5/2023 yameandika juu ya hafla ya kustaafu kwa majaji 3 wa mahakama kuu ya Tanzania, tunawapongeza kwa kulitumikia Taifa letu na tunawatakia maisha mazuri ya uraiani.

Jambo nililojifunza ni kwamba Majaji hao wanaonekana kuwa na umri mkubwa sana, nimejiuliza hivi Majaji huwa wanastaafu wakiwa na umri wa miaka mingapi?

Kwa kuzingatia kazi ngumu wanazozifanya nashauri umri wa kustaafu majaji upunguzwe uwe miaka 50.

Inaonekana Majaji wengi wamechoka kwa umri kuwa mkubwa lakini wapo kazini tu, idadi ya majaji wanaostaafu ni ndogo sana ukilinganiaha na idadi ya wazee waliopo makazini, jamani tubadilike, tuwapishe vijana.
Mkuu
Pamoja na kuwa Jaji ni mwanasheria lakini umri unavyosonga mbele ndivyo anavyokuwa gwiji kwenye kufanyakazi zake.

Umri wao wa miaka 60+ ni sahihi kwani hadi muda huo akili inakuwa njema kabisa
 
Mkuu
Pamoja na kuwa Jaji ni mwanasheria lakini umri unavyosonga mbele ndivyo anavyokuwa gwiji kwenye kufanyakazi zake.

Umri wao wa miaka 60+ ni sahihi kwani hadi muda huo akili inakuwa njema kabisa
Hizo ni fikira za kizamani,
Wapishe vijana wachape kazi, miaka 55, 60 ni umri wa kupumzika sio kupambana.

Nawashauri wazee wangu Majaji wanao jijua kuwa Wana umri zaidi ya miaka 50 wastaafu wapishe vijana nao wasukume gurudumu la Taifa.

Tubadilike tuache mazoea, wazee hawataki kustaafu vijana wanakosa ajira.
 
Majaji..nadhan wanakaa kuamzia High Court na court Appeal .. cjui Sheria lakn nadhan.. hzo mahakama.zinahtaj watu wenye busara na uzoefu sana...maana Kuna makesi ya hatari hko...sishangai sana wap kustaaf umri huo@na ingependezaa wangeendelea tuu
 
Hizo ni fikira za kizamani,
Wapishe vijana wachape kazi, miaka 55, 60 ni umri wa kupumzika sio kupambana.

Nawashauri wazee wangu Majaji wanao jijua kuwa Wana umri zaidi ya miaka 50 wastaafu wapishe vijana nao wasukume gurudumu la Taifa.

Tubadilike tuache mazoea, wazee hawataki kustaafu vijana wanakosa ajira.
Vijana wenyewe akili zimejaa kula kimasihara...

Wazee waendelee tafadhali


Nimekaa paleee
 
Vijana wenyewe akili zimejaa kula kimasihara...

Wazee waendelee tafadhali


Nimekaa paleee
Wazee Wana presha na sukari juu unatarajia kuna jipya hapo? au unataka waifie ofisini?!, nawaomba wazee wetu kwa heshima waende wakapumzike inatosha.

Ukitumikia Taifa lako kwa zaidi ya miaka 20 inatosha, pisha wengine pia.

Kwakweli huwa sipendi kuona wazee wamengangania ofisini wakati umri umewatupa mkono.

Umri wa kuishi/ lifespan umepungua sana ni kati ya miaka 45 Hadi 50 sasa unataka Jaji astaafu na miaka 55!!
 
Majaji..nadhan wanakaa kuamzia High Court na court Appeal .. cjui Sheria lakn nadhan.. hzo mahakama.zinahtaj watu wenye busara na uzoefu sana...maana Kuna makesi ya hatari hko...sishangai sana wap kustaaf umri huo@na ingependezaa wangeendelea tuu
Hekima wapi, tuhuma za rushwa tu.
 
Back
Top Bottom