Kimsingi, haya mambo yanachanganya.
Kuna kipindi huwa nahisi kuna hawa viongozi wa dini wanajua hivi vitu hakuna ila wanawazuga tu wafuasi wao, kwa sababu wanazozijua wao, Niliwahi kumsikia Dr.W.Slaa akisema kuwa kipindi bado yuko padre alishawahi kutumwa na kanisa, atembee katika vijiji vya karatu kufundisha watu kwamba hakuna uchawi, na katika kitabu hicho cha padre Gregory, kinachoitwa HAKUNA BINADAMU MCHAWI ILA SHETANI, mwishoni ni kama anasema kuwa huo ndio msimamo wa kanisa, Kanisa takatifu la mitume la Roma. (The Holy, Apostolic, Catholic Roman Church).
Amefafanua kuwa kwenye Biblia uchawi umetajwa, ila katika mazingira ya imani tu, kuwa watu waliamini hivyo, na kuna mfano wa wachawi wa Farao kufanya uchawi wa kugeuza fimbo kuwa nyoka, yeye anadai ile ilikuwa aidha kiini macho, au vitu vingine lakini sio uchawi.
Mtazamo huu wa wakatoliki, japo unanishangaza, lakini naupenda.
Unachanganya axiom na uthibitisho.
Axiom si uthibitisho. Euclid aliposema two parallel lines could never meet and a triangle is only 180 degrees, alikuwa hathibitishi hayo. Alikuwa anatoa axioms tu. Baadaye tumeona jinsi parallel lines zinavyoweza kukutana na pembetatu inavyoweza kuwa na zaidi ya nyuzi 180 au pungufu.
Unachotuletea wewe hapa.ninaxioms, sio proofs. Know tye difference.
Mke ni nani? Kuna mtu amekaa na mwanamke miaka anasema mkewe, kuulizwa cheti cha ndoa hana.
Mwingine.kaoa.ana cheti, lakini ndoa haitambuliki kimila.
Nani mseja na nani kaoa?
Pia kuna compyuta inayoendeshwa kwa nishani ya mahindi, hivyo inakula chakula.
Na kuna kiziwi anayesikia kwa kutumia hearing aid.
Epic fail.
Aisee! Huwa unajipa moyo sana. Endelea....!
Utakusaidia nini
I can believe this.Kwa watu wanaosoma.theolojia ya juu kama makasisi, makardinali.na mapapa huwa wanajua kwamba hakuna mungu.
Ila wanaona dini ndio.mhimili pekee wa kuwanyoosha wanadamu.
Kwa hiyo wanaendeleza uongo kwa rationalization ya kwamba ni uongo mzuri unaowafaa watu.
It makes a lot of senseNdio maana kuna watu wanampuuza tu ...!!
Hakuna jaribio lolote la kisayansi linaloweza kuthibitish chochote ambacho hakipo hakipo.
Kama unalo, litaje hapa.
Kwa hiyo, hatuthibitishi chochote ambacho hakipo kwamba hakipo.
Tunathibitisha kile ambacho kipo kipo.
Kwa hiyo unapoongelea habari za mungu, tuondoe.suala.la kuthibitisha kwamba hayupo.
Kwa sababu hakuna chochote ambacho hakipo kinachoweza kuthibitishwa kwamba hakipo, siyo mungu tu.
Tuangalie vinavyoweza kuthibitishwa, vile vilivyopo.
Kama mungu yupo kweli, kwa nini hawezi kuthibitishika?
Mkuu Eiyer,
Kwanza nasikitika kwamba umefikia hitimisho la uwendawazimu na ujinga mapema mno,
Umefikia hitimisho hilo, inwezekana bila hata kukisoma kitabu chenyewe. I can forgive you may be you are a little emotional about this topic!!
Mtunzi wa kitabu hicho, Psdre Gregory Yoanes Mwageni wa Shirika la watawa wa Benedictine mtu mtu mzee sana sasa, ni msomi sana na ameona mambo mengi kuliko mimi na wewe.
Kama wewe ni age mate wangu, basi nikushangaze kuwa katika umri wako, alikuwa anaamini uchawi kuliko hata wewe.
Alipofikisha umri wa miaka saba tu, alipelekwa kuishi na mchawi mkuu wa Ubena, aliitwa Mwalinunge Mahali Mkali, akaishi nae, akafundishwa madawa na uchawi. Amejifunza aina nyingi za unaoitwa uchawi kutoka kwa wachawi wa aina na maeneo mbalimbali ya Tanzania na Zambia hadi akajiridhisha kuwa anajua aina nyingi za uchawi kuliko mchawi yeyote aliyewahi kumjua.
Alianza rasmi kufanya utafiti na uchunguzi kuhusu uchawi mwaka 1933 hadi mwaka 2010 alipojiridhisha kuwa hakuna uchawi ndipo akatengeneza kitabu. Huyu amefanya utafiti kwa miaka yote hiyo, wewe kama hujafanya utafiti huna haki ya kumbishia kwa vitu vichache hivyo tu ulivyoona, yeye kaona maajabu mengi kukushinda mkuu.
Kabla hujaendelea kumkosea adabu, hebu kakitafute kwanza kwenye bookshops za makanisa ya katoliki, ukisome, halafu ndio umkosoe.
Hey man unaongea nini sasa?
Particle physics yote inadili na haya mambo, kuna particles nyingi sana Kimahesabu inatabiri hazipo na watu wakifanya majaribio kweli wanathibitisha hilo, hii inafanyika kila siku, unafikiri kazi ya particle accelerator kama LHC ni nini?!
Ni theory ngapi watu wamendekeza ambapo kimahesabu inatabiri uwepo wa kitu lkn hawawezi kuthibitisha kwa Majaribio (experiments), Mfano mdogo tu Dark Matter, theory nyingi zinatabiri uwepo wake lkn hakuna Jaribio lililothibitisha kama kuna Dark mater na wala hakuna mtu aliyewahi kuona Dark matter hata kwa kutumia telescope, na sasa bila uthibitisho wa kwamba Dark matter ipo mambo mengi yanayojulikana kuhusu Universe yanakwama inabaki kuwa Imani tu kama vile watu wanaoamini Mungu yupo na wengine wanaamini hayupo na wote wawili si ajabu wako sahihi kwa maana hakuna anayeweza kuthibitisha, uwepo wa Dark Matter wala kutokuwepo kwake kwa maana mahesabu yanatabiri ipo lkn Kimajaribio haionekani!
Hilo swali la kama Mungu yupo mimi siwezi kulijibu kwa maana nimeshakwambia kwamba hakuna jaribio lolote la Kisayansi linaloweza kuthibitisha uwepo wake na kinyume cheka!
Huwezi kuthibitisha kwamba kisichopo hakipo.
Kwa sababu uthibitisho upo kwenye domain ya vilivyopo, na always kuna the unknown, kwa hivyo, polisi wakija nyumbani kwangu na kusema nimeficha madawa ya kulevya, hawaniambii mimi nithibitishe kwamba sina madawa ya kulevya. Kwa sababu kama.sina.siwezi kuthibitisha hilo.
Wao watafanya search, wanaweza kuyapata na.kuthibitisha yapo.
The concept of.proving that which is.not there is not there is illogical.
You take things too lightly my friend, things are a little complicated."Hadi akajiridhisha kuwa anajua aina nyingi za uchawi kuliko mchawi yeyote aliyewahi kumjua" halafu akaja kusema hakuna uchawi!!!!
Huyu bado ni mwendawazimu tu!!.
Hili nalijua sana na huenda huyo kibabu aliangukia kwenya hawa ambao ni chakaYou take things too lightly my friend, things are a little complicated.
Kuna watu waamini kuwa wao ni wachawi, lakini kiukweli sio wachawi. Can you understand this Eiyer?
Hivi Mjuni nina haja gani kumsikiliza mtu hata kama naona kabisa anadanganya?Padre akiongea kitu mheshimu sana, wengi wao wamebobea kwenye theolojia na falsafa, unaifahamu theolojia?
Established By Who?
Nauliza tu...
Mungu Ameweka Principles + So does Everyone who's in control! Kanuni hizo zipo kwa ajili ya kubalance mambo yaende sawa...
Tambua tu Maovu yaliyopo ni kipimo cha mema... Yaani ili uweze kugundua jambo jema ni lazima ujue kinyume chake, Upo?
Na kumbuka Mungu hawezi kutupa mtihani/challenge ambayo hatuimudu,, No way.. Ukitizama vizuri haya maradhi, matatizo n.k Yapo kwa ajili ya kutu-push kutoka kwenye comfort-zone ili tumtambue na kumuabudu..
Asingeshindwa kutupa Unconditional Love lakini ingekuwa ni uwendawazimu, tungedumaa, na maisha yasingekuwa hivi uyaonavyo!
Na hata anavyotuadhibu, Ni uthibitisho tosha kuwa anatupenda kwa sababu hataki tufanye makosa!!!!
So the whole thing is arbitrary?
Na.mimi.naweza kuanza kusema mungu ni Mchagga mwenye macho matatu anayeishi juu ya mlima Kilimanjaro nikawa sawa?
inategemea... kama unaamini hivyo basi uko sawa (kutokana na imani yako). suala la ipi iko right na ipi iko wrong lazima iwe tatizo coz matter ya right and wrong ktk dunia hii haiko static. some things which were right in the past are currently wrong & vice versa! Personally, i am religious coz 'right and wrong' concepts dont vary there; they dont have exceptions. kwa hiyo kwa upande wangu, I think earthly Morals are actually the ones which bullshits, unless they corresponds to MY religion.
Final Statement
hapa kazi ipo mkuu lakini tutafika tu ngoja twende taratibuhapa lazima vichwa vifumuke, ya Kaisari mpe Kaisari
Habari zenu wakuu!!
Kwa muda sasa nimekuwa nikifutilia kuhusu mwanzo wa ulimwengu kwa maana ya sayari, mwezi/miezi, Nyota, jua pia Big bang na kinachoitwa Black Hole!!
Katika kufatilia huku nimekuja kupata mkanganyiko kwa namna biblia inavyoelezea vizazi toka kuumbwa Dunia na vilivyomo pamoja na Adam ambapo hata miaka 10,000 haifiki!! Upande wa pili ukiwafatilia wanasayansi ni kwamba kilichoanza ni Big bang(miaka 13.7bilion iliyopita), zikafuatia nyota na baadaye sayari yetu dunia(miaka 4.6 bilion iliyopita).
Je kwanini kuna tofauti kubwa sana kati ya kinachoitwa kitabu kitakatifu na sayansi ya ulimwengu, ni waandika biblia walidanganya au wanasayansi wanadanganya? Vipi kuhusu mabaki ya Dinosaurs yaliyogunduliwa na utafiti kuonesha hawa viumbe waliishi zaidi ya miaka 200 million iliyopita?