Umri gani unafaa kujitegemea

Umri gani unafaa kujitegemea

hyle master

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2013
Posts
209
Reaction score
23
Kama kijana anaye ishi na wazazi wake au walezi wake na anawategemea katika Huduma mbalimbali za kijamii.

Ni mambo gani ambayo kijana anatakiwa kujiandaa ili aweze kijitegemea.

Na upi umri sahihi wa kuweza kujitegemea?
 
hm...jiangalie mwenyewe na plans zako..kuna mtu namjua, jamaa ameishi nyumbani kwao hadi siku anaoa, kaingia kwny myumba yake na ana estate yake vizuri...usipojua unaweza fikiri lele mama ila mtu anafanikisha plans zake vizuri..as lomg as unajielewa na mwanamke wako anakuelewa, poa tu
 
Kama kijana anaye ishi na wazaz wake au walezi wake na anawategemea katika Huduma mbalimbali za kijamii ni mambo gani ambayo kijana anatakiwa kujiandaa ili aweze kijitegemea na UPI umri sahihi wakuweza kujitegemea

Vuta picha ya wale watoto ombaomba na wale wa mitaani kisha mshukuru Mungu una pesa ya bundle na simu ya 3G yenye chaji na mtandao halafu kikubwa kuliko vyote una Afya na muda

Kwahiyo kipekee kabisa napenda kukupongeza kwakuwa mpaka mada ikae hapa ni vitu vingi vimejumuika kwa pamoja na kila kimoja kina nafasi yake muhimu bila kujali udogo wake

Post yako yaweza kuonekana ni ya kipuuzi na ya kitoto kabisa lakini kwangu mimi naamini imebeba ujumbe uliofichika na pengine majibu yake yanaweza kuwa tiba na mwanga kwa wengine
Wazungu wanasema 'even a fool has a story to tell'
 
Kuna kitu kinaitwa 20 years old na 20 years and old,unaona tofauti ya sentensi hizi?
 
Mtoto wangu ana miaka 17 kashaanza kujitegemea ana shamba lake la miti, ana ngombe 6, ana kiwanja tayari ila bado ana kula Ugali wangu.
 
Asanteni wakuu kwa mrejesho wenu ila nilicho jufunza kutoka kwenu ni vizur kujitegemea kwanza pale onapokuwa tegemezi na hili bado ni tatizo kwa sisi vijana wengi wetu hatupendi kujituma na tunapenda mambo kimteremko na kufanya baadhi yetu kuwa tegemez hata pale tukiwa katika maisha ya kujitegemea
 
Ukishaanza tu kutongoza/kutongozwa jua unaweza kujitegemea.
 
Back
Top Bottom