Gaijin
JF-Expert Member
- Aug 21, 2007
- 11,812
- 5,286
Kisa ni kukataa kunyanyaswa!
Wewe mtu unapigwa kama mtumwa sababu tu monita kakuandika jina eti ulikuwa unapiga kelele?
Halafu unaamriwa ushike dawati au ukuta halafu ucharazwe mboko sita, na kabla ya hapo unapapaswa kuona kama umeweka makaratasi kwenye kaptura.
Hapana bana. Siyo mtumwa miye. Ukinigusa kwa nguvu inakurudia, ima fa ima.
Nchi za watu mwalimu hagusi mwana wa mwingine.
Duh hapo kweli. Mtu akupige utasema si binaadamu au huna masikio na fahamu ya kuelewa jema na baya?!
Mie shule nilizosoma hakukuwa na bakora, adhabu kufagia au kumwagia maji bustani.
Na siku ningepigwa, mama yangu nna guarantee angewaendea huko huko. Hachukui kabisa mwanawe mtii kuonewa.
Keshawahi kuwaendea once, nipo form 3 nikagombwa mbele za wanaume kibaoo ati uniform yangu too flashy. Walijuta kumfahamu