Umewahi kulala stesheni enzi za miaka ya 70 hadi 90?

satininus

Senior Member
Feb 11, 2021
135
171
Mimi niliwahi mara kacha kulala stesheni ya Shinyanga kutokana na ukweli kwamba treni za kwenda na kutoka Mwanza(Locomotives) zilikuwa zinapita usiku hivyo mimi mara zote nilikuwa nashuka kutoka Dodoma mishale ya saa 6 usiku kwa vile wazazi walikuwa wanaishi Kahama nilipaswa nilale hapo stesheni ili kukicha niendelee na safari.

Sasa yaliyokuwa yanatokea usiku huo ni mengi kuna wenzetu wenye matatizo ya akili huwa wanalala stesheni na wana maeneo maalum katika moja ya mabenchi halafu usiku kucha wanaongea peke yao au kupiga kelele na kuvuta goso wakati mwingine bange, kundi la pili ni vibaka wanajifanya wasafiri ili kufanya timing ya abiria wanaochukuliwa usingizi ili wawaibie pesa ama mizigo, enzi hizo hakukuwa na simu za mkononi.

Hivyo ilifanya usiku uwe mrefu sana pia kulikuwa na baridi kali, kunguni, mbu na mende halafu pale Shinyanga choo cha abiria kilikuwa nyuma ya nyumba ya abiria halafu unakuwa kama unashuka bondeni yaani sijui ilikuwa ni kusababisha tafrani kwa abiria maana mazingira yote yalikuwa hatarishi bila ulinzi, mwanga wala chakula.

Hebu wadau nanyinyi tiririkeni.
 
Umenikumbusha mambo ya train la central line. Kipindi hicho treni inatoka Dar saa kumi na kuingiashinyanga kesho yake usiku.
Kuna lijamaa Fulani msukuma alikuja Dar kwa ndugu zake. Ndugu zake nao sio watu wachovu walimpa hela ya kutumia njiani Hadi ya huko aendako Ibinzamata.

Huyu msukuma alipata siti vile viti vya third class vya kutizamana vya mbao enzi zile. Hela zake alikua ameziweka kwenye boksa na juu kavaa suruali. Kumbuka boksa za wasukuma enzi hizo sio hizi mnazojua.

Hizo ilikua Ni kaptura ya zamani au suruali iliyokatwa miguu halafu inashonewa mfuko kwa ndani. Yaani ili ufikie pesa kwanza uteremshe suruali, Kisha ufungue vifungo vya boksa ndio uingize mkono mpaka kwenye mfuko ulio katikati ya mapaja. Yaani kumuibia msukuma enzi zile ilikua Ni ndoto maana pesa zinakaa jirani kabisa na p**mb.

Msukuma alijiona pesa yake iko sef kabisa. Alifanya kosa moja. Kufika Dodoma Ile saa nne asubuhi alizitoa zile pesa akazihesabu Kisha akazirudisha mfukoni. Zilikua mia tano nyekundu na arobaini na tano tu. Kufika Singida Tena akazitoa na kuzihesabu na kuzirudisha sehemu ya Siri ndaani ndani huko karibu na wajukuu.

Kumbe wakati akazihesabu Kuna wahuni nao walikua wanazihesabu na kutulia. Kufika Tabora mtani Tena akazichomoa zile pesa na kuzihesabu na kuzirudisha kwenye boksa.

Kufika Shinyanga msukuma akateremka kumbe wahuni nao walikua wanateremkia Shinyanga. Sasa kwa kua Ni usiku na asingeweza kwenda Ibinzamata ilibidi alale pale stesheni akiamini pesa zake ziko salama salmini. Alienda kwenye benchi moja na kuketi na kuanza kulala.

Kumbe wahuni walikua akili zinachaji jinsi ya kumuibia msukuma. Walichukua pochi yao mbovu mbovu wakaweka picha ya mmoja wao kwenye pochi Kisha mmoja wao akaenda kuitupa Ile pochi karibu na yule msukuma. Wahuni wakalala Ila kufika saa kumi alfajiri mmoja wao akasema ameibiwa pochi yake yenye picha yake na shilingi Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano na ishirini mbili na coin ya sh tano.

Mhuni mmoja alisema anamhisi yule msukuma kwani pochi ameiona jirani kabisa na yule msukuma, wengine pale walikua Ni wamama.
Penye wengi hapaharibiki neno.

Muhuni kaulizwa Ni sh ngapi umeibiwa naye kasema Ni Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano. Ishirini mbili na gobore tu. Mhuni mwingine katoa wazo kwamba wamsachi yule msukuma.

Msukuma kusachiwa kweli bwana ndani ya boksa alikutwa na hicho kiasi Cha pesa. Kwanza pesa zilichukuliwa kisa kachezea kichapo na kuachwa anavuja damu.
 
Umenikumbusha mambo ya train la central line. Kipindi hicho treni inatoka Dar saa kumi na kuingiashinyanga kesho yake usiku.
Kuna lijamaa Fulani msukuma alikuja Dar kwa ndugu zake. Ndugu zake nao sio watu wachovu walimpa hela ya kutumia njiani Hadi ya huko aendako Ibinzamata.
Huyu msukuma alipata siti vile viti vya third class vya kutizamana vya mbao enzi zile. Hela zake alikua ameziweka kwenye boksa na juu kavaa suruali. Kumbuka boksa za wasukuma enzi hizo sio hizi mnazojua. Hizo ilikua Ni kaptura ya zamani au suruali iliyokatwa miguu halafu inashonewa mfuko kwa ndani. Yaani ili ufikie pesa kwanza uteremshe suruali, Kisha ufungue vifungo vya boksa ndio uingize mkono mpaka kwenye mfuko ulio katikati ya mapaja. Yaani kumuibia msukuma enzi zile ilikua Ni ndoto maana pesa zinakaa jirani kabisa na p**mb.
Msukuma alijiona pesa yake iko sef kabisa. Alifanya kosa moja. Kufika Dodoma Ile saa nne asubuhi alizitoa zile pesa akazihesabu Kisha akazirudisha mfukoni. Zilikua mia tano nyekundu na arobaini na tano tu. Kufika Singida Tena akazitoa na kuzihesabu na kuzirudisha sehemu ya Siri ndaani ndani huko karibu na wajukuu. Kumbe wakati akazihesabu Kuna wahuni nao walikua wanazihesabu na kutulia. Kufika Tabora mtani Tena akazichomoa zile pesa na kuzihesabu na kuzirudisha kwenye boksa. Kufika Shinyanga msukuma akateremka kumbe wahuni nao walikua wanateremkia Shinyanga. Sasa kwa kua Ni usiku na asingeweza kwenda Ibinzamata ilibidi alale pale stesheni akiamini pesa zake ziko salama salmini. Alienda kwenye benchi moja na kuketi na kuanza kulala. Kumbe wahuni walikua akili zinachaji jinsi ya kumuibia msukuma. Walichukua pochi yao mbovu mbovu wakaweka picha ya mmoja wao kwenye pochi Kisha mmoja wao akaenda kuitupa Ile pochi karibu na yule msukuma. Wahuni wakalala Ila kufika saa kumi alfajiri mmoja wao akasema ameibiwa pochi yake yenye picha yake na shilingi Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano na ishirini mbili na coin ya sh tano.
Mhuni mmoja alisema anamhisi yule msukuma kwani pochi ameiona jirani kabisa na yule msukuma, wengine pale walikua Ni wamama.
Penye wengi hapaharibiki neno. Mhuni kaulizwa Ni sh ngapi umeibiwa naye kasema Ni Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano. Ishirini mbili na gobore tu. Mhuni mwingine katoa wazo kwamba wamsachi yule msukuma. Msukuma kusachiwa kweli bwana ndani ya boksa alikutwa na hicho kiasi Cha pesa. Kwanza pesa zilichukuliwa kisa kachezea kichapo na kuachwa anavuja damu.
Umeniacha hoi kuhusu msukuma na pia umenikumbusha Ibinzamata nilishawahi kuishi enzi nasoma Buluba
 
Umenikumbusha mbali Mimi nimelala ya tabora mwaka wa 1984 naelekea kigoma kwenye maisha kutafuta rizki.
Nilikuwa nafuata mashati ya Juliana,upo hapo.
Nilishawahi kuibiwa begi baada ya kushuka kwenda kupata msosi kumbe behewa letu lilikatwa na kupelekwa kwenye line ya Kigoma.
 
Pale Tabora mzee kaka tena ilikuwa mwezi wa sita baridi ilinipiga balaa!! Hela ya guest hamna....ni kukomaa tu ..maisha ya shule bana.
 
Pale Tabora mzee kaka tena ilikuwa mwezi wa sita baridi ilinipiga balaa!! Hela ya guest hamna....ni kukomaa tu ..maisha ya shule bana.
Station ya tabora kulikua na wezi sana. Walikua na mtindo wa kutembea juu ya mabehewa halafu wanaingia dirishani kuchomoa mizigo.
 
Mimi niliwahi mara kacha kulala stesheni ya Shinyanga kutokana na ukweli kwamba treni za kwenda na kutoka Mwanza(Locomotives) zilikuwa zinapita usiku hivyo mimi mara zote nilikuwa nashuka kutoka Dodoma mishale ya saa 6 usiku kwa vile wazazi walikuwa wanaishi Kahama nilipaswa nilale hapo stesheni ili kukicha niendelee na safari.

Sasa yaliyokuwa yanatokea usiku huo ni mengi kuna wenzetu wenye matatizo ya akili huwa wanalala stesheni na wana maeneo maalum katika moja ya mabenchi halafu usiku kucha wanaongea peke yao au kupiga kelele na kuvuta goso wakati mwingine bange, kundi la pili ni vibaka wanajifanya wasafiri ili kufanya timing ya abiria wanaochukuliwa usingizi ili wawaibie pesa ama mizigo, enzi hizo hakukuwa na simu za mkononi.

Hivyo ilifanya usiku uwe mrefu sana pia kulikuwa na baridi kali, kunguni, mbu na mende halafu pale Shinyanga choo cha abiria kilikuwa nyuma ya nyumba ya abiria halafu unakuwa kama unashuka bondeni yaani sijui ilikuwa ni kusababisha tafrani kwa abiria maana mazingira yote yalikuwa hatarishi bila ulinzi, mwanga wala chakula.

Hebu wadau nanyinyi tiririkeni...
Acha kabisa tuliwahi lala stand ya KAMATA Mwanza usafiri shida sana tiketi anauziwa msafiri tulikua familia wote tulikesha stand ili kununua tiketi saa 12 asubuhi, maisha yale? sitakuja sahau.
 
Umenikumbusha mambo ya train la central line. Kipindi hicho treni inatoka Dar saa kumi na kuingiashinyanga kesho yake usiku.
Kuna lijamaa Fulani msukuma alikuja Dar kwa ndugu zake. Ndugu zake nao sio watu wachovu walimpa hela ya kutumia njiani Hadi ya huko aendako Ibinzamata.
Huyu msukuma alipata siti vile viti vya third class vya kutizamana vya mbao enzi zile. Hela zake alikua ameziweka kwenye boksa na juu kavaa suruali. Kumbuka boksa za wasukuma enzi hizo sio hizi mnazojua. Hizo ilikua Ni kaptura ya zamani au suruali iliyokatwa miguu halafu inashonewa mfuko kwa ndani. Yaani ili ufikie pesa kwanza uteremshe suruali, Kisha ufungue vifungo vya boksa ndio uingize mkono mpaka kwenye mfuko ulio katikati ya mapaja. Yaani kumuibia msukuma enzi zile ilikua Ni ndoto maana pesa zinakaa jirani kabisa na p**mb.
Msukuma alijiona pesa yake iko sef kabisa. Alifanya kosa moja. Kufika Dodoma Ile saa nne asubuhi alizitoa zile pesa akazihesabu Kisha akazirudisha mfukoni. Zilikua mia tano nyekundu na arobaini na tano tu. Kufika Singida Tena akazitoa na kuzihesabu na kuzirudisha sehemu ya Siri ndaani ndani huko karibu na wajukuu. Kumbe wakati akazihesabu Kuna wahuni nao walikua wanazihesabu na kutulia. Kufika Tabora mtani Tena akazichomoa zile pesa na kuzihesabu na kuzirudisha kwenye boksa. Kufika Shinyanga msukuma akateremka kumbe wahuni nao walikua wanateremkia Shinyanga. Sasa kwa kua Ni usiku na asingeweza kwenda Ibinzamata ilibidi alale pale stesheni akiamini pesa zake ziko salama salmini. Alienda kwenye benchi moja na kuketi na kuanza kulala. Kumbe wahuni walikua akili zinachaji jinsi ya kumuibia msukuma. Walichukua pochi yao mbovu mbovu wakaweka picha ya mmoja wao kwenye pochi Kisha mmoja wao akaenda kuitupa Ile pochi karibu na yule msukuma. Wahuni wakalala Ila kufika saa kumi alfajiri mmoja wao akasema ameibiwa pochi yake yenye picha yake na shilingi Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano na ishirini mbili na coin ya sh tano.
Mhuni mmoja alisema anamhisi yule msukuma kwani pochi ameiona jirani kabisa na yule msukuma, wengine pale walikua Ni wamama.
Penye wengi hapaharibiki neno. Mhuni kaulizwa Ni sh ngapi umeibiwa naye kasema Ni Mia tano na arobaini na tano. Wekundu wstano. Ishirini mbili na gobore tu. Mhuni mwingine katoa wazo kwamba wamsachi yule msukuma. Msukuma kusachiwa kweli bwana ndani ya boksa alikutwa na hicho kiasi Cha pesa. Kwanza pesa zilichukuliwa kisa kachezea kichapo na kuachwa anavuja damu.
Sijakuelewa uliposema ameshindwa kwenda ibinzamata huo usiku ikabidi alale stesheni,nijuavyo mimi ibinzamata na stesheni ni kama km 2 tu hivi
 
Mimi niliwahi mara kacha kulala stesheni ya Shinyanga kutokana na ukweli kwamba treni za kwenda na kutoka Mwanza(Locomotives) zilikuwa zinapita usiku hivyo mimi mara zote nilikuwa nashuka kutoka Dodoma mishale ya saa 6 usiku kwa vile wazazi walikuwa wanaishi Kahama nilipaswa nilale hapo stesheni ili kukicha niendelee na safari.

Sasa yaliyokuwa yanatokea usiku huo ni mengi kuna wenzetu wenye matatizo ya akili huwa wanalala stesheni na wana maeneo maalum katika moja ya mabenchi halafu usiku kucha wanaongea peke yao au kupiga kelele na kuvuta goso wakati mwingine bange, kundi la pili ni vibaka wanajifanya wasafiri ili kufanya timing ya abiria wanaochukuliwa usingizi ili wawaibie pesa ama mizigo, enzi hizo hakukuwa na simu za mkononi.

Hivyo ilifanya usiku uwe mrefu sana pia kulikuwa na baridi kali, kunguni, mbu na mende halafu pale Shinyanga choo cha abiria kilikuwa nyuma ya nyumba ya abiria halafu unakuwa kama unashuka bondeni yaani sijui ilikuwa ni kusababisha tafrani kwa abiria maana mazingira yote yalikuwa hatarishi bila ulinzi, mwanga wala chakula.

Hebu wadau nanyinyi tiririkeni...
Niliwahi kukaa stendi ya Moshi usiku nasubiri basi la KAMATA. Usiku ilikuwa ombaomba wote wa mji wanahamia pale na wengi walikuwa wameugua ugonjwa wa ukoma. Vyoo vilikuwa vichafu sana lakini walikuwa wanalala karibu na vyoo. Vibaka nao walikuwepo na ukizubaa unakuta begi limeshaenda. Basi lilikuja limechelewa saa 8 nikaondoka na kushukuru.
 
Sijakuelewa uliposema ameshindwa kwenda ibinzamata huo usiku ikabidi alale stesheni,nijuavyo mimi ibinzamata na stesheni ni kama km 2 tu hivi
Asingeweza kwenda usiku ule kwani alikua na pesa mingi. Miaka Ile nauli ya treni ya Shy haifiki sh hamsini. Yeye alikua na Mia tano na ushee. Yaani Leo labda ni Kama 2m.
It was a lot of money. Huwezi ku risk
 
Niliwahi kukaa stendi ya Moshi usiku nasubiri basi la KAMATA. Usiku ilikuwa ombaomba wote wa mji wanahamia pale na wengi walikuwa wameugua ugonjwa wa ukoma. Vyoo vilikuwa vichafu sana lakini walikuwa wanalala karibu na vyoo. Vibaka nao walikuwepo na ukizubaa unakuta begi limeshaenda. Basi lilikuja limechelewa saa 8 nikaondoka na kushukuru.
Pole sana yaani ilikuwa ni balaa baridi la Moshi ni balaa tupu.
 
Back
Top Bottom