Umesikia Marehemu aliyekufa miaka 10 Akidaiwa Kodi

Bowie

JF-Expert Member
Sep 17, 2016
4,372
6,078
Hivi majuzi nilienda TRA kulipa kodi nikaambiwa kuna gari sijalilipia kodi ya mapato na motor vehicle kwa muda wa miaka kumi kwa hiyo natakiwa nilipe hilo deni.

Gari hilo lilishakatwakatwa na watengeneza majiko miaka kumi iliyopita na kwa muda huo wote halikuwa barabarani, wadau hii imekaaje utalipia kodi kitu kilichotupwa zamani.

Mimi binafsi naishauri serikali kama gari linadaiwa kodi ama motor vehicle licence walisubiri barabarani wakilipata walikamate sio deni la gari moja lilete tatizo kwa mlipa kodi, nasikia kuna watu walinunua magari ama gari lakini wamekamatiwa magari kwa deni la gari lingine.

Ukikamua ngo'mbe maziwa kwa kulazimisha matokeo yake utakamua damu.
 
Hivi kwa nini gari kama haijalipiwa ndani ya miaka 5 wasilifute???? Ila waweke mechanism ya kutrack just in case mtu anakwenda lipia???


Miaka 10 halijalipiwa hawajiongezi???
 
Mkuu, sasa kama gari imekatwakatwa na hukurudisha kadi hao jamaa wangejuaje kama uliikatakata.

Mimi nilikuwa na mkweche wangu na ukafia nyumbani ukawa banda la kuku nikaenda TRA nikawaambia wakaniambia niende police gari ikaguliwe na baada ya taarifa ya police nirudishe kadi yao. Nikafanya hivyo na wakaifuta kadi ya hilo gari wakanipa nyingine imeandikwa deregistered. Sidaiwi road licence kwenye hiyo gari.

Kwa hili nadhani tatizo ni hao jamaa kutotoa elimu ya kutosha ili wananchi wajue cha kufanya. Japokuwa hivi karibuni nimeona wakitoa hiyo elimu.
 
Issue siyo kulazimishwa kulipa Kodi ila mlipa Kodi unatakiwa kuzifahamu kanuni za Kodi.

Unapokuwa na gari na liko grounded unatakiwa kumfahamisha Kamishina wa TRA ili aliondoe ktk orodha yake. Kinyume na hapo utadaiwa Kodi ya motor vehicle.
 
Hivi kwa nini gari kama haijalipiwa ndani ya miaka 5 wasilifute???? Ila waweke mechanism ya kutrack just in case mtu anakwenda lipia???


Miaka 10 halijalipiwa hawajiongezi???

Mi kuna kimkokoteni nilimuuzia mtu miaka hiyooo... kumbe jamaa hakubadili umiliki. kilishajifia siku nyingiii... naambiwa nadaiwa road licence sijui nini. Kwakuwa sipendi ujinga kamkokoteni kengine nimekasajili kwa jina la binti yangu. Acha waendelee kujilimbikizia madeni ya mkokoteni mfu
 
Mi kuna kimkokoteni nilimuuzia mtu miaka hiyooo... kumbe jamaa hakubadili umiliki. kilishajifia siku nyingiii... naambiwa nadaiwa road licence sijui nini. Kwakuwa sipendi ujinga kamkokoteni kengine nimekasajili kwa jina la binti yangu. Acha waendelee kujilimbikizia madeni ya mkokoteni mfu
Yaani TRA wabadilike

Haiwezekani ipite miaka 10 bado wawe wanadai. Kma vipi wafanye uhakiki ili kuondoa magari yaliyojifia kwenye system

Yaani kama ushasukuma gari zamani saa hizi tumbo juu
 
Yaani TRA wabadilike

Haiwezekani ipite miaka 10 bado wawe wanadai. Kma vipi wafanye uhakiki ili kuondoa magari yaliyojifia kwenye system

Yaani kama ushasukuma gari zamani saa hizi tumbo juu
Jamaa yangu alikamatwa Same akiwa anaelekea Moshi kwa Xmas... gari alilouza miaka 8 iliyopita limemletea matatizo kwenye gari jingine alilonunua mwaka jana. Yono wanachukua na ada yao ya kukamata eti...jamaa hakuachiwa gari mpk alipolipia gari lililokufa.

Na kila siku gari linapolala kwenye yard yao unachajiwa elfu 26, hiyo ni nje ya gharama ya "kukamatwa" na Yono ambayo ni elfu 36 cash!!

Nyambaff
 
Kama kuna Bad debt kwanini kusiwe na bad tax? Wao wanadhani wanaongeza mapato kumbe ukweli wanayapunguza, watu wengi wana-divert TIN zao kukwepa histori za kipuuzi kama hizo. Wanajikosesha tu mapato bila kujielewa.
 
Jamaa yangu alikamatwa Same akiwa anaelekea Moshi kwa Xmas... gari alilouza miaka 8 iliyopita limemletea matatizo kwenye gari jingine alilonunua mwaka jana. Yono wanachukua na ada yao ya kukamata eti...jamaa hakuachiwa gari mpk alipolipia gari lililokufa.

Na kila siku gari linapolala kwenye yard yao unachajiwa elfu 26, hiyo ni nje ya gharama ya "kukamatwa" na Yono ambayo ni elfu 36 cash!!

Nyambaff
Yono.....

Hili ni jipu jingine
 
Yaani TRA wabadilike

Haiwezekani ipite miaka 10 bado wawe wanadai. Kma vipi wafanye uhakiki ili kuondoa magari yaliyojifia kwenye system

Yaani kama ushasukuma gari zamani saa hizi tumbo juu
Ukiuza gari wakati wa kubadilisha umiliki nadhani kuna kodi pale. Sasa kwa kutobadilisha umiliki unakuwa unakwepa kodi. Ukisukuma inabidi umiliki ubadilishwe na kodi ilipwe.
 
Mi kuna kimkokoteni nilimuuzia mtu miaka hiyooo... kumbe jamaa hakubadili umiliki. kilishajifia siku nyingiii... naambiwa nadaiwa road licence sijui nini. Kwakuwa sipendi ujinga kamkokoteni kengine nimekasajili kwa jina la binti yangu. Acha waendelee kujilimbikizia madeni ya mkokoteni mfu
Safi kabisa, mi hata driving license now days natumia ya my wife mke wangu.
 
TRA wanawajibika kutuelinisha
Mkuu naamini hili la elimu ni muhimu. Naona siku hizi wameanza kutoa elimu hii. Pia nadhani system za nchi hii hazijakaa vizuri kwani si rahisi kutambua kwamba gari fulani haipo barabarani na hivyo hata takwimu za magari hapa nchini nadhani si sahihi. Kuna magari ambayo yamekufa na hayapo barabarani lakini hajafutwa kwenye register ya hawa jamaa wa TRA. Ni muhimu wakafanya data clean up.
 
Hivi kwa nini gari kama haijalipiwa ndani ya miaka 5 wasilifute???? Ila waweke mechanism ya kutrack just in case mtu anakwenda lipia???


Miaka 10 halijalipiwa hawajiongezi???
Mkuu nadhani nasi wamiliki wa magari tunatakiwa tuwasaidie. Hivi wanawezaje kufuta gari toka kwenye register yao bila wewe kutoa taarifa. Wakifanya hivi sisi wenyewe tutakuwa wa kwanza kulalamika kwamba wanafuta magari bila kuwa na taarifa.
 
Mkuu naamini hili la elimu ni muhimu. Naona siku hizi wameanza kutoa elimu hii. Pia nadhani system za nchi hii hazijakaa vizuri kwani si rahisi kutambua kwamba gari fulani haipo barabarani na hivyo hata takwimu za magari hapa nchini nadhani si sahihi. Kuna magari ambayo yamekufa na hayapo barabarani lakini hajafutwa kwenye register ya hawa jamaa wa TRA. Ni muhimu wakafanya data clean up.
Tatizo wengi wa wamiliki hawakuwa wanajua 0

Ila watafute utaratibu mzuri (system)

Na waeleze wananchi life span ya haya magari ni miaka mingapi
 
Back
Top Bottom