Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,426
- 18,228
- Thread starter
- #41
hehehehe ungenifanyia hivo mimi ningejisikia vibaya sana,mana utakuwa umeshafahamu siri zanguMimi yuko jamaa alinifananisha na mtu tunayefanana sana, hivyo nikaendeleza naye stori mpaka ikafika pahali niseme ukweli kuwa sio mimi.
Sehemu ya mazungumzo yalikuwa hivi:
Yeye: Kwa hivyo ahadi yetu ya J3 ipo.
Mimi: J3?
Yeye: Si jana nilikupigia nikakuambia itabidi tuende J3?
Mimi: Mbona sikumbuki?
Yeye: Kwa hivyo hujawapigia studio kuwaambia kesho tunaenda kurekodi?
Kufika hapa nikaona yamekuwa makubwa, lakini kwa kuwa anayemzungumza ninafahamiana naye na tulikutana si muda mrefu, nikamwambia ukweli kuwa sio mimi, lakini huyo anayemzungumza atafika pale si muda mrefu.