Umeshawahi kupotea Kariakoo? Juzi ilibaki nukta nipige mayowe

Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.
Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo...

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba,

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa,...

Nilikua na location 9..., Nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee,

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga...."?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, Yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi....

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki....

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau.

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayoweee....

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa, ..

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini....

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia,
Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani??? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza,

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi...
Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo....


Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta..

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"
Hii nyingine zamani Hiyo nilikwenda hapo ubungo business park nakwenda kwenye ATM za EXim ,huko nilikotoka nimetoka na nauli tu sh 500 sina nauli ya kurudia sababu najua naenda kuchukua hela ,hizi huduma za mobile money hazikuwa zimeshika kasi,nafika hapo business park nakuta ATM ina shida haifanyi Kazi ,ATM nyingine ya karibu ipo Mlimani City nikasema sio kesi natembea KWA mguu,

Akili yangu ikapiga hesabu kuwa nikiingilia shekilango nikitembea tembea kisha huko mbele nikakunja kushoto ntatokea Mlimani hahhha
Salaleee!!
Nilikosea hesabu baada ya kuingia Hiyo mitaa ya hapo ubungo ,nilizunguka Sana sanaaaa mwisho wa SIKU nikatokea EMAUS nyuma ya STend ya ubungo baada ya kupoteza muda huko mitaani
Safari ya Mlimani ikaanza upya hapo ubungo Nikiwa hoi .
 
Nimetoka zangu kariakoo naenda Posta Masumin stationery, nimefika pale mnazi mmoja, nikamfuata jamaa anauza duka la vitenge nikamuuliza Masumin ipo wapi? Akanielekeza.

Cha ajabu nimekata mitaa kama 3 naelekea mtaa mwingine nashangaa napita pale pale kwenye njia ya duka la vitenge, namuona jamaa amekaa kwenye stuli anaangalia nje. Nikaona aibu kumuangalia

Ikibadi nimuulize mtu mwingine Masumin ipo wapi.
Hahahaha
 
Nimetoka zangu kariakoo naenda Posta Masumin stationery, nimefika pale mnazi mmoja, nikamfuata jamaa anauza duka la vitenge nikamuuliza Masumin ipo wapi? Akanielekeza.

Cha ajabu nimekata mitaa kama 3 naelekea mtaa mwingine nashangaa napita pale pale kwenye njia ya duka la vitenge, namuona jamaa amekaa kwenye stuli anaangalia nje. Nikaona aibu kumuangalia

Ikibadi nimuulize mtu mwingine Masumin ipo wapi.
Hahaha yaan hiyo mitaa ya mnazi mmoja to posta za hapo ndani ndani ni kisangaa
 
Kila mtu anakazania kuchukua contacts za muuzaji, ila kumbuka kama mtu sio muungwana ukimpigia akijua umepotea na ndio mara yako ya kwanza kwenda kwake ndio kwisha habari yako hio,

Chukua kwa dharura na wewe jitahidi kwenye mzigo wako andika namba(natarajia kama umeenda kwenye manunuzi hukosi angalau viwili kati ya notebook, kalamu na Marker pen) waambie wakitaka kuondoka wakupigie, wakikupigia basi hao ni watu na kama umepotea anzia hapo sasa...

Kukalili mtaa/kumbukumbu kichwani ni muhimu tuuh, Sio kila ukipotea basi kila mtu ajue umepotea, hasa sehemu za fursa kama zile.
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.
Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo...

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba,

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa,...

Nilikua na location 9..., Nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee,

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga...."?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, Yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi....

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki....

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau.

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayoweee....

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa, ..

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini....

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia,
Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani??? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza,

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi...
Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo....


Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta..

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"
asee jamaa yafaa kuwa comedian, nimechekaaa,ila hapo kuuliza watu kama wamekuona ukipita umetisha mkuu,
 
Jumapili nikaingiq njia ya kuelekeq shimoni saiv si wafanya biashara wanafanya biashara nje nikasem ngoja nizunguke nitokee nilipoingilia weeeh najikuta niko mtaa mwingine kabisa faster nikarudi na njia niliyoingilia kariakoo cjwah pazoea
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.
Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo...

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba,

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa,...

Nilikua na location 9..., Nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee,

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga...."?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, Yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi....

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki....

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau.

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayoweee....

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa, ..

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini....

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia,
Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani??? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza,

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi...
Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo....


Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta..

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"
Hahahahahahahahahahahaa dah nimecheka sana wallah
 
Huyu jamaa Pantomath anaonekana ni wale watu wa mikoani waliozoea kuendesha taratibu kwa zao kwa njia za kijima. Ununuzi wa bidhaa wa kukariri namna hii ulikuwa unafnyika miaka hiyo wakati hakuna njia nzuri za mawasiliano au kuweka kumbukumbu. Eti unanunua mzigo maduka 9 halafu unang'ang'aniza yote uyakariri kwa kichwa!

Eti akariri
Wengine hawajui map app ni ipi wanataka wasaidiwe hata kuitumia pia
 
Pole
🤣🤣🤣 ndio maana k.koo unaweza useme mwenzako yupo bussy kutafuta pesa kumbe kapoteanaaa yupo kwenye harakati za pimbi..

Maajabu ya Kariakoo kuzunguka na kushangaa umerudi duka ulilotoka ni kitu cha kawaida, dhamilia kutafuta duka ulilotoka sasa kama utalipata.

Kuna jamaa yangu naye alipoteana, inafika jioni anasema au niende polisi?????

Nikamuuliza unaenda polisi umetapeliwa? Haya lets say umedanganya ukadai umetapeliwa, haya wakikuambia tupeleke utaenda wapi?...

Kariakoo achana tuu na duka, ukiingia kule kati, kuitafuta tuu barabara kuu ya msimbazi pale polisi ni mtihani, badala ya kuifuata unaitoroka kuelekea mnazi mmoja, unakutana na mtu posta unamuuliza aggrey ipo wapi hapa?????
Au unamuuliza mtu, "huku naenda wapi?"

Mimi kipindi ndio naanza machimbo ilikua nikifika sehemu nikifanya manunuzi nikaacha mzigo, naigingia google map na search location then na save au ku screenshot, baadae nafuatilia tuu, kwa njia hio sijawahi potea, kwa sasa sihitaji uongozi wowote popote natoka...

Niliwahi kupotea Tanga usiku kwenye zile barabara zao za namba, ikabidi nirudi baharini nianze kuhesabu barabara.
Sana
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.

Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo.

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba.

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa.

Nilikua na location 9, nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee.

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga"?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi.

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki.

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau.

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayoweee.

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa.

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini.

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia.

Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza.

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi.

Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo.

Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta.

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"
Ha ha ha .

Pole sana mkuu
 
Kuna dada alipiga yowe kama wewe na anachagua watu wakuuliza mimi nilivaa suruali ya kitambaa kubwa nimekula mkanda nje ndio akanifuata kuniuliza alizunguka kuanzia saa nne asubuhi Hadi nakutana naye saa kumi.

Alinunua kandambili baada ya viatu vya mchuchumio kumchosha kwa kuzunguka

Alikuwa anataka atoke akapande bus za mbagala
Endeleza kidogo mkuu, ulimsaidiaje sasa!
 
Nilikwenda kufanya manunuzi maduka matano. Kila nilipoingia na kufunga mzigo walinifata wahuni wakikusanya mzigo kwa kisingizio kwamba niliwatuma wauchukue, wale wahuni walinigawana, kila ukiingia unakuta umeingia naye..ukiondoka anatoa maelezo kama wewe anaoewa mzigo.

Jioni saa mbili Sina mzigo hata mmj wezi wakijibebea, masikini wa Mungu ilikuwa duka la mwisho walau ningeambulia ule mzigo kwa kuwa ndio nilikuwa nao mkonon yule mwiz wa mwisho alifanikiwa baada ya kwenda kuita usafir...

Nikaiyona kariakoo inastahili ipigwe Bomu tufe wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom