Umeshawahi kupotea Kariakoo? Juzi ilibaki nukta nipige mayowe

1635262418416.jpg
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.

Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo.

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba.

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa.

Nilikua na location 9, nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee.

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga"?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi.

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki.

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayowee, pembeni kuna jamaa kajikalia kachoka kanyoosha miguu na mizigo yake ananung'unika, sijui nini kimempataa.

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa.

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini.

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia.

Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza.

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi.

Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo.

Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta.

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"

Ilifika hatua nakutana na Henganjifu na maji yangu, ndio nashtuka kumbe nazunguka hapa hapa.
Nini maana ya kumiliki mawasiliano
 
Tutawapeleka mji mkongwe Zanzibar, ili mpotee mazima!!
Nilitaka kuandika hii. Yaani ile sehemu huwezi kariri njia kwamba ninapopita wakati wa kwenda nipite mulemule wakati wa kurudi neva . Na hili si kwa mgeni tu hata wenyeji.
 
Hii mada inawalenga sana wale wenye mishe misheza manunuzi kariakoo.

Aisee kama huna uzoefu na ile mitaa, hasa ile ya nguo, nakushauri ukinunua mzigo wako ukiona huwezi tembea nayo bora utafute hoteli ulipie uwe unakusanyia mizigo yako hapo.

Mimi sio mgeni wa k.koo hata kidogo, ila juzi ni kama ndio nimefika kwa mara ya kwanza,

Ipo hivi
Nimefanya manunuzi yangu ya nguo za jumla, Ikawa kila ninapochukua mzigo sababu ni mkubwa na bado naendelea basi naufunga namwachia mwenye duka mpaka nitakapo maliza nazungukia kote nabeba.

Pasipo kuelewa jinsi ninavyoiacha ndio nazidi kuchanganya mambo, imefika saa 9 hivi nikawa nishamaliza, ni kuanza ku kusanya sasa.

Nilikua na location 9, nikaanza moja baada ya nyingine, Zikabaki 3, hizi sasa ndio kimbembeee.

Siku za nyuma ilikua kila nikiacha mzigo basi na kalili ule mtaa na duka ili iwe rahisi baadae, Sasa juzi kwa haraka niliyokua nayo na huku nikiamini sijawahi potea na nishakua mzoefu nika ignore hilo swala,

Aloo, Nilizunguka ile mitaaa huku machozi yakinilenga kadiri mda unavyopita,

Duka la kwanza kati ya yale matatu nililipata baada ya 2hrs, kumbuka hizo 2hrs zote nilikua natafuta bila kupumzika,
Na sio kama nililiona mwenywe ila nilikua napita lesi ndio jamaa akaniita akaniuliza "bro vipi bado sana maana ndio tunakaribia kufunga"?

Nikajifanya "Ahaaa basi poa ngoja tuu nitembee nao" nikachukua mzigo huku moyo ukiruka ruka kwa kushukuru, yaani pale ndio kabisaa nilikua sipawazi kama nilifanya manunuzi.

Sikutaka hata kuchelewa nikaupeleka guest, inshu ni hayo maduka mawili, Kazi ikaanza tena, hapo mda umeenda, watu washaanza kufunga, kila nikisikia wanashusha yale ma milango yao ya bati, napanick natoka nduki.

Nikatafutaweeeeee, inafika saa 12, nimechoka, nimepanick, nimekata tamaa, Jasho na kiu haviniishii Nishanunua maji kama katoni nzima na henganjifu za kutosha ila vyote kila ninapo simama nikiondoka nimesahau

Ikafika saa moja, Hapo sasa wengi washafunga, nikawa natembea kinyonge, machozi yananilenga nikiona magrili yanashushwa tuu, nikakaa sehemu ilibakia nukta nipige mayowee, pembeni kuna jamaa kajikalia kachoka kanyoosha miguu na mizigo yake ananung'unika, sijui nini kimempataa.

Sikua na la kufanya zaidi ya kusubiri kesho yake ambayo ni jana, Akili ilikua ishachoka, nikampigia Rafiki yangu aje tuu anitoe pale nilipokuwepo, maana niliona kabisa mwendokasi ikinivaa.

Asubuhi, nikaingia tena, Inafika saa 6, bila bila, hapa nikaanza kupiga hesabu namna ya ku compensate hasara ya kama 900k na usheee(almost 1M kasoro).

Nikakaa tena sehemu, hapa ndipo nikagundua kweli akili ya binadamu kuna mzingira inafanya kazi baadae ukikaa ukijiuliza ni wewe huamini.

Nilianza kuvuta kumbukumbu za kuanzia Mwanzo naingia k.koo ile jana asubuhi, nini nilianza nacho, wapi nilianzia, basi kuanzi hapo mtiririko wa mazingira ya nje ya kuanzia duka la kwanza mpaka la 9 ukanijia.

Hayo ni mazingira ya pale dukani, inshu ni mtaa na njia gani? Kwa kumbukumbu hivyo hivyo nikaja nikajua ni duka la ngapi na la ngapi katika ule mtiririko ndio nimeyapoteza.

Njia kila nikivuta kumbukumbu haziji, nikaona best option ni kwenda kuanzia duka la kwanza kutembea huku nikivuta kumbukumbu, ile ndio ilikua pona yangu, Mzigo wa kwanza nikaupata duka namba 4 mtaa wa Congo na agrrey, mzigo wa pili duka namba 7 Mchikichi na Nyamwezi.

Bahati nzuri ni waaminifu, nikakuta mizigo yangu salama, nikabeba, huyoooo.

Mpaka nikakumbukaga kale ka meme, watu wanakatumaga kiutani ila kumbe inaonesha wao yalishakuta.

"Ulishawahi kupotea kariakoo mpaka ukapita sehemu ukawauliza watu, mliniona nikipita hapa?"

Ilifika hatua nakutana na Henganjifu na maji yangu, ndio nashtuka kumbe nazunguka hapa hapa.
Kama ni wa kuja kupotea ni kawaida ila kama siyo hata usiku wa manane wa kiza hupotei.
 
Nimewahi poteana hapo Kariakoo mtaa wenyewe sio complicated
Lengo langu niende NMB nyuma ya kituo cha polisi msimbazi ,nimepanda costa natokea manzese ,badala ya Costa kupita fire ikakatisha mitaa ambayo siijui nadhan ni kwenye ofisi za mwendo kasi pale ila sikunote nilikuwa nimelala,
Tukaenda shushwa mitaa siko familiar nayo
Nikaona isiwe tabu nikachukua bodaboda nikampa maelekezo anishushe BIG BON
Nikapelekwa ila akili yangu ikagoma kbsa kuwa pale ni big bon ,
Petrol station naiona,na kituo cha polisi nakiona ,Ili viko upande tofauti na vinapotakiwa kuwa(KWA mujibu wa akili yangu)
Yaani mfano akili inaniambia kituo cha polisi kinatakiwa kiwe upande wa kushoto kwako mimi naona kiko Kulia kwangu ,nikadaka wenge
Najua kbsa Nmb wako nyuma ya kituo cha polisi ,ila akili yangu inageuza mazingira
Nikaamua kujiripua kwenda mtaa unaonipeleka huko nyuma ya kituo cha polisi Ndo kama nikawa nimeRESET akili
Vitu vyote vikarudi kama vinavyitakiwa kuwa.
Mm pia uwa inanitokea hasa ukipelekwa sehemu Kwa kupitishwa njia usizo zijua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom