Nilishawahi tapeliwa penzi na mdada iliniuma hadi na mimi nikawa sina huruma na wanawake,nakumbuka nilimsomesha na kumjali kila kitu najinyima najitunza namsubiri yeye amalize chuo nimuoe daaaaah picha linaanza kamaliza chuo hataki kuja dar anataka abaki huo mkoa anadai amemis kukaa na mamaake.nikamtafutia kazi arusha namshara wa kwanza angelipwa 900000 akagoma pia niliumia sana coz mtu niliyemwomba amuunganishe namheshimu sana na yule dada alipata hiyo kazi bila interview ni vyeti tu.hata vyeti mimi ndio nilivipeleka kwa yule mtu.siku ya kazi demu anapigiwa simu areport arusha hapokei simu. Wakanipigia mimi kwa vile niliandikwa kama mdhamini wake.ikabidi nimtafute kwa mamaake nikampata namwambia y hapokei simu hana sababu muhimu za kuniambia.ikabidi nimpigie yule mheshimiwa nikamwambia amcancel tu huyo dada.kumbee hapo mkoa alipo kulikuwa na kajamaa kana mdanganya na kumtia kiburi hadi akawa hataki kazi.maisha yakaenda, kuna siku nakuta msg tuachane nimepata ninayempenda hii msg iliingia wakati nakula nilishindwa kula nampigia simu hapokei baadaye akaja kupokea na kuniambia vile alivyoaandika ndivyo alivyomaanisha na hana hisia na mimi kabisa.niliumia nilikonda ghafla.nikafanya manuva yangu nikapata no ya yule anayemtia kiburi jamaa kwa ustarabu kabisa akanijibu demu wako ananishobokea mwenyewe me simtaki ila yeye ana force tu daaah nikajiuliza huyu demu nilikosea wapi mbona kila anachotaka nampa kama kumgegeda na mgegeda mpaka anasema D unanifikishaga kwenyewe nikajiuliza au kibamia jibu hapana.nikambembeleza wapi kagoma anadai kashafanya maamuzi nikapiga simu kwa mamaake akamgomea mpaka mamaake aisee basi nikawa sina la kufanya nikaacha maisha yaendeleee tu.nikafanya kila njia mpaka nikamsahau kabisa.nika move on na maisha yangu.baada ya miaka kadhaa naona no ngeni kupokea nakuta ni yeye akawa ananiomba msamaha anadai usichana ndio ulimdanganya kwani yule jamaa kamzalisha na hamjali kabisa pia kajaribu kutafuta kazi mpaka sasa kakosa akadai ni laaana niliyompa ndio inayomtesa hadi mambo yake hayaaendi.nilichomjibu ni kwamba mimi nilishamsamehe kitambo sanaa.basi akaanza tena kunijulia hali vimassage kibao.binafsi sinaga hamu naye kabisa wala kumuwazia hadi ananiambia D umebadilika sio kama yule wa mwanzo.mimi nabakigi nacheka angejua ninavyomchukia kwa kunipotezea mda wangu wala asingekuwa anajibebisha.anyway malipo ni hapa hapa duniani.sorry kwa kuwachosha kusoma
Asanteni ndugu wasomaji.