witnessj
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 28,710
- 47,100
EbwanaeehArusha mjini, nakumbuka ilikuwa jumamosi ya Tarehe 5 Julai mwaka 2014, tulikuwa Bar na washkaji zangu watatu na demu mmoja wa msela...jumla tukawa watano including me...sasa katika pombe pale kati jamaa akaanza kuniamshia noma kuwa demu wake ananishobokea na ninaonesha kuwa nimemtamani....tukagombana sana ile kweli kweli....ikafika mahali wakasema tuondoke hapo wote twende kiwanja kingine, tukatoka mpaka nje kwenye gari ya huyo jamaa yetu ambaye ndo mwenye demu, nataka kuingia kwenye gari kumbe masela wote washakubaliana kuwa waniteme kama adhabu yangu, na kweli nikaachwa pale peke yangu usiku ule mnene...nikasema poa nikadaka Toyo zinazopark nje ya bar nikaenda kiwanja tofauti na wao. Asubuhi iliyofuata naamka na taarifa ya msiba, kumbe walipotoka pale Bar wakiwa njiani na speed kali ya Subaru Forester ya msela na pombe juu wakavaana na Land cruiser huko njiani....walikata moto wote wale....yaani wote!!!!!!!!