SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,240
- 4,270
Je wanaJF, umewahi kukutana na watu wenye wivu mkubwa wa kitu ulichonacho?Watu hawa hutumia saikolojia ya kuponda hicho kitu chako ili ujisikie vibaya na kuchukia kumbe wanaonyesha mauwivu yao tu.
Kama umenunua gari watasema:
'Unaringia sana hilo gari eh? Unaringia kaburi? Nyumba hata hujapaka rangi eti wanunua gari.'
Ukijenga nyumba utawasikia:
'Hio nayo ni nyumba? Nyumba ziko Masaki, sio hicho kibanda chako cha kuku!'
Uwe na binti mwadilifu na anayemudu vizuri masomo yake, maneno yataenda hivi:
'Hana lolote huyo. gesti ndo nyumbani kwake.Si ajabu ana ngoma hapo alipo.
Ukiwa na mke mwenye bidii na mchapakazi utasikia yafuatayo:
'Mwanamke anaringa kama nini sijui, tena mnafiki sana. Tena kamkalia mumewe ile mbaya!
Nk nk
Umeshawasikia au kukutana na watu wa aina hii?
Kama umenunua gari watasema:
'Unaringia sana hilo gari eh? Unaringia kaburi? Nyumba hata hujapaka rangi eti wanunua gari.'
Ukijenga nyumba utawasikia:
'Hio nayo ni nyumba? Nyumba ziko Masaki, sio hicho kibanda chako cha kuku!'
Uwe na binti mwadilifu na anayemudu vizuri masomo yake, maneno yataenda hivi:
'Hana lolote huyo. gesti ndo nyumbani kwake.Si ajabu ana ngoma hapo alipo.
Ukiwa na mke mwenye bidii na mchapakazi utasikia yafuatayo:
'Mwanamke anaringa kama nini sijui, tena mnafiki sana. Tena kamkalia mumewe ile mbaya!
Nk nk
Umeshawasikia au kukutana na watu wa aina hii?