Umeoa Msukuma?

Teddy Kalonga ni msukuma Pure, Baba na Mama wote ni Wasukuma pure, nadhani ni watu wa Ntuzu zone (Bariadi, Maswa na Magu)

Hapana hatokei Ntuzu huyo. Mimi ndio meya wa Ntuzu na hilo jina sijawahi kulisikia. Kama anadai yeye Mnyantuzu basi Mnyantuzu feki huyo.
 

hata mahari yao ya ng'ombe sitini kwa sifa zao ni kidogo sana😀
 
Nacho wapendea zaidi ni warefu na wenye maumbo mazuri huku wakiwa na sauti nyororo zenye kumtoa nyoka pangoni. Kwa kweli ni warembo sana watoto wa Usukumani.

Fidel, kuhusu urefu, wengi ni average. Ila ukikuta warefu, ni warefu kweli. Pia kuna baadhi ya koo unakuta karibia ukoo mzima ni warefu. Sasa kama wewe unaishi Dar halafu hao watu wanakuwa wamewekeza au kuishi Dar, wengi ya utakao kumbana nao watakuwa kutoka kwenye huo ukoo, na hivyo basi kuonekana kuwa hivyo (warefu/average/au wafupi).
 
Hapana hatokei Ntuzu huyo. Mimi ndio meya wa Ntuzu na hilo jina sijawahi kulisikia. Kama anadai yeye Mnyantuzu basi Mnyantuzu feki huyo.
wewe meya wa Ntunzu?unapafahamu kwa Ng'hwani?mahongo,midimu
 
msukuma jina au msukuma halisi?wengine ni wasukuma jina(baba na mama wasukuma) yy kazaliwa dar,kakulia dar hana hata chembe ya usukuma huyu ni msukuma jina. mwingine kazaliwa na kukulia usukumani ana tabia na utamaduni wa kisukuma,nafikiri hawa wote ni wasukuma lakini ukioa hapa unaoa watu wa aina mbili tofauti,je PAKAJIMMY unazungumzia msukuma gani?
 
Hapana hatokei Ntuzu huyo. Mimi ndio meya wa Ntuzu na hilo jina sijawahi kulisikia. Kama anadai yeye Mnyantuzu basi Mnyantuzu feki huyo.

Kalonga ni Kahama kama sikosei!
 

Ni kweli, kuna wadada fulani nawafahamu ni watu wa Sindiga ila wamekulia Usukumani tangu wakiwa wadogo. Ni mpaka wakwambie kwamba wao sio Wasukuma ndipo utajua. Maana wana tabia za Kisukuma kwa 100%
 
wewe meya wa Ntunzu?unapafahamu kwa Ng'hwani?mahongo,midimu

Kote huko kuanzia kwa kina Ng'wanakilalo, Shumasike, kwa akina Ng'wanacheyo....

Wewe siku siku ukienda pale stendi ya mabasi pale Bariadi (pale karibu na sokoni) ulizia Juli ni nani.....

Nimefanya sana kazi na padri Gapa.....unamjua huyo? Ntuzu nzima wanamjua huyu ni nani...
 

Point nzuri, lakini iko blurred by your own misunderstanding or should I say, lack of knowledge kuhusiana na tabia za binadamu.

Mtu anayetokea sehemu za Usukumani, na akawa pure Msukuma; kisha akawa anakaa/kuishi sehemu tofauti na Usukumani, the likelihood ya yeye ku-conform na society mpya ni rahisi hata pale atakapokuwa ametunza mila na desturi zake zote kutoka kule aliko. And this is a positive aspect in human behavioural matter for my reckoning. Sasa huyo wako katoka Usukumani akiwa darasa la tatu bado tu unataka a-behave kama alikuja Dar akiwa mtu mzima... hii si itakuwa ni mischaracterization.
 
sikubaliani na hayo,uongo mtupu. kama ni hivyo kila mtu atavutia kwake.unafiki mtupu huo hakuna ukweli.wanawake wa makabila yote waweza oa inategemeana na mtu individually hakuna kugeneralize kwamba eti wote wanaheshima msidanganyane.
 
sikubaliani na hayo,uongo mtupu. kama ni hivyo kila mtu atavutia kwake.unafiki mtupu huo hakuna ukweli.wanawake wa makabila yote waweza oa inategemeana na mtu individually hakuna kugeneralize kwamba eti wote wanaheshima msidanganyane.

Wewe ndiyo mnafiki hapa...Maana unaargue kitu ambacho hukijui kwa kun'gang'ania generalization...Kukaa kimya si kosa mkuu,ni busara zaidi
 
sikubaliani na hayo,uongo mtupu. kama ni hivyo kila mtu atavutia kwake.unafiki mtupu huo hakuna ukweli.wanawake wa makabila yote waweza oa inategemeana na mtu individually hakuna kugeneralize kwamba eti wote wanaheshima msidanganyane.

Mama Briana twende rataratibu. Tumeseama wengi wao ni wakarimu na wana heshima kwa waume zao ukilinganisha na wanawake wa makabila mengine!

Give credit where it is due! Mbona sisi tunakubali kwamba Wachaga ni kabila lenye kujua kutafuta pesa na kujiletea maendeleo?
 
Mkuu Julius,
Umesahau kuwa ni wanapenda sana Wazungu na kwenda kwa waganga..
ukiacha hizo sifa hapo juu kwa kweli wanawake Wakisukuma ni ni wanafaa kwa kuoa, mimi mwenyewe nina mpango wa kujichukulia jiko toka huko na mchumba mwenyewe ni mdogo wake Balantanda.
 

Mazee, unapoint nzuri na zote ni valid.

Kuhusu ukicheche, sababu zinaweza kuwa nyingi. Kukaa mbali kama ulivyosema wewe ni mojawapo. Pili, labda umri na mazingira waliyomo yanaendekeza mambo hayo. Kama nilivyosema awali, iwapo wasichana watakuwa wamekuja na umri mdogo hapo, basi uwezekano wa kuwa hawajaishi au kuingiwa na mila za Usukumani ni mkubwa. Kingine, tukumbuke kuwa dunia ya sasa ni ya utandawazi. Hakuna jamii ambayo haiko affected na influence ya mambo ya kisasa kutoka Ulaya na kwingineko ambapo, mapenzi (yasiyoyakweli) au ngono zembe vimeathiri jamii pahala pengi. Si kabila au koo ambapo hutokuta mambo haya ya utandawazi yakiwa ni negative force kwa tamaduni zilizopo au kuzoeleka.

Kuhusu swala la ushirikina, hili jambo ni 50/50 IMHO. Kumbuka kabila la Wasukuma ni kubwa sana. Kuna koo na koo... nyingine nyingi hawaamini hata mambo ya Mungu (ukristo au uislam). Wana abudu miungu yao waijuayo. Isitoshe, dini za Uislam na Ukristo nazo zinatabaka kubwa tu huko. Hivyo basi, mambo ya ushirikina in general ni mambo ya society za Kiafrika. Kuna zile zisizokubaliana nayo na kunazile zinazoyaendekeza. Majirani zako watakuwa ni moja ya kundi la pili kwa maoni yangu.

Kuhusu undugu, hii ni kweli tupu. Lakini nadhani ni easily explainable. Ni mila iliyojengeka kutokana na halihalisi ya living in a land of plenty. Kuanzia ardhi, watu, vyakula, n.k. Wasukuma naturally (kama ilivyokuwa awali), wanamaisha ya kusaidiana, kufanyakazi pamoja na kushiriki kwenye hafla na shughuli nyinginezo kijamii bila kutengana. Hii imejengeka kwenye desturi zao, and sometimes kutokana na kuwa ni desturi ya muda mrefu, inatokea pahala inakuwa executed at wrong time and wrong place. Haswa swala la kuishi mbali na Usukumani linapohusishwa.

Hivyo basi, unaweza kuiita ni tabia mbaya au nzuri, nategemea. Ni mbaya kwa mambo na maisha ya mjini, lakini ni tabia ambayo ni nzuri au yenye mema iwapo, jamii zetu zisingeasirika na msukumo mkubwa kutoka mijini unaoingilia jamii zinazoenzi mila na desturi, haswa vijijini. Na ni kwa nadharia hiyo basi, nami nasema kuwa hii ni mila ya kuacha ife, maana maisha yamebadilika. Na wimbi la mambo ya kimjini na matatizo au forces zote zilizopo katika jamii sasa hivi, hata ujaribu vipi kuzuia zisikukumbe, bado zitajipenyeza. There are times when you have to allow to succumb to negative influences!
 

Mhhh hii kali..Ni wasukuma wa wapi hao unawazungumzia waenda kwa waganga???,heheeeeee

Kuhusu wazungu,nadhani wao ndo huwapenda wamama wakisukuma kwa tabia na uasili wao(si unajua wazungu hawapendi mambo ya mkorogo)
 
Mhhh hii kali..Ni wasukuma wa wapi hao unawazungumzia waenda kwa waganga???,heheeeeee

Kuhusu wazungu,nadhani wao ndo huwapenda wamama wakisukuma kwa tabia na uasili wao(si unajua wazungu hawapendi mambo ya mkorogo)

mmalize kuwajadili hao dadazenu (wifi zangu) afu tufungue mjadala wa waume zetu wasukuma....watu watoe credit hapa!!!!
 

Una-point nzuri lakini umeiharibu wewe mwenyewe kwa kutia chumvi nyingi.

Nullified.
 
mmalize kuwajadili hao dadazenu (wifi zangu) afu tufungue mjadala wa waume zetu wasukuma....watu watoe credit hapa!!!!

Heheeeeeeeee...Hiyo itabidi muianzishe nyie wamama,japo hakuna kitakachoharibika maana hata siye ni funika bovu
 
Heheeeeeeeee...Hiyo itabidi muianzishe nyie wamama,japo hakuna kitakachoharibika maana hata siye ni funika bovu

haaaaaa wawamba ngoma nyie woooote hapa na hao kaka zako.................
 
haaaaaa wawamba ngoma nyie woooote hapa na hao kaka zako.................

Hapana mama,ni ukweli mtupu...Si unaona jinsi wifi zako akina Kabula na Nshoma walivyo,wana tabia safi kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…