When you lead someone on a path knowing very well the end wont be pleasant for them ,you sure like hell deserve credit for it.Watu wengi wanawake kwa wanaume wanapoingia kwenye mahusiano kwa sababu ambazo ni za kibinafsi mf. sex...pesa...sifa na mengineyo hua wanajua vizuri sana kwamba baada ya wao kupata walichotaka na kuridhika lazima watakua wamewakorofisha/wachanganya wale waliotumiwa kutimiza haja na mahitaji yao kwa namna moja ama nyingine.
Mwanaume/mwanamke anaeingia kwenye mahusiano kwa sababu hizi za kibinafsi alafu akamwaminisha mwenzake kwamba anampenda na ana malengo nae mwenzake anajitolea mengi kuhakikisha mahusiano yao yanachanua.Muda...pesa...marafiki au hata ukaribu wa ndugu unaweza kutolewa kafara kwaajili ya hili alafu siku ya siku mtu anakwambia bwana ehhhh mi nimeshakuchoka au sikupendi tena na kama kaamua kukumaliza anakwambia kabisa nia yangu ilikua kupoteza muda tuna wewe huku nikisubiria wa kunifaa...pole/samahani kwa kukutumia.Muda ulishaenda...waliokupenda kweli ulishawatolea nje sasa nao hawakuhitaji tena...marafiki ulishapoteza kadhaa kwasababu ya mpenzi....pesa ulishatumia nyingi kumsomesha/kumfungulia biashara then unajulisha/gundua kwamba wote ulikua mchezo tu....KWANINI USIONE KWAMBA UMEHARIBIWA MAISHA???!
Mwanaume au hata mwanamke aliye ndoani anapomwaminisha mwenzake yeye ndo yeye kumbe mkewe/mume yuko shule au kamuacha nyumbani mpaka mwenzie anakolea na kuamini ndoa itakuwepo ni muda tu na mipango...ghafla mimba imenasa alafu anakuja ambiwa nna mke/mume mimi ujie....na miaka ilishakata hisia zilishachezewa KWANINI HUYU MTU ASIONE KWAMBA KAHARIBIWA MAISHA in terms of malengo na mipango???!
Mume/mke au mchumba yuko mbali anatuma vijisenti kila mwezi angalau nao siku moja wawe na kwao alafu anarudi kukuta pesa zake zilikua zinamlisha mwanamke/mwanaume mingine au imejengwa akifika anaambiwa hana chake anaingizwa mwingine ndani KWANINI HUYU MTU ASIONE KAHARIBIWA ukizingatia kwamba hata viakiba vyake alivitoa akijua faida ipo?!
Yapo mengi sana yanayompa mtu ruhusa/haki ya kuona ameonewa au hata kuharibiwa malengo na mipango yake aliyojiwekea awali.Ndio kwa kiasi flani hata mkosewa anaweza kua amechangia kwa kutokua wangalifu ila ni wangapi kati yetu wenye bahati ya kufikiria kwa kutumia kichwa badala ya moyo linapokuja swala la kuanguka mapenzini?!Sio wengi....na ndio maana mioyo haiishi kuvunjwa kwahiyo usihukumu kila anaesema hivyo kwamba ni uzembe wake....jua kwanza historia ya aliyomkuta.
Kuhusu wanaoitisha kujiua kwakweli nashukuru sijakutana nao....ila hua najiuliza hua wanapoamua kujia kweli hua wanapania kumkomoa nani haswa maana namjua mzee aliyejiua kwaajili ya mapenzi na mpaka leo hua hata siwezi kuimagine yule mama na wanae watakua wanajiskia vipi kujua yeye ndo msababishi a watoto kujua mama ndie msababishi!
Pheeeeeeewwwww!.....well, well, well....kwa hapo kweli nimeona wapi "tofali" aka "Jiwe la msingi" la umeniharibia maisha lilitaka kuwekwa rasmi!
Nimekosa hata cha kuongeza bana, pole sana kamanda.
Jaman jana tu mwenzenu aliyekuwa mpz wangu wa miaka kansalit na mwaka huu ndio nimefanikiwa fanya nae mapenzi kwani alikuwa bikla na tumefanya tendo hili mara 2 tu chakushangaza mwezi ulio pita alisafili kwenda hom kwao kwan tuna kaa wilaya tofauti baada yakufika huko nikapigiwa sim na aliwekuwa mpz wake wa zaman kabla yangu akiniambia kuwa mpnz wangu ana tembea na rafiki yake na siku ana piga cm aliwakuta mara ya 3 wakitoka guest house mi nikaamua kumuuliza akanijibu ni maneno tu ya watu alafu hapo hapo akampigia sim jama aliyenipa taarifa na kumtukana sana kisha aka mpigia huyo jamaa yake mpya kumuuliza kama ameniambia japo mimi hatufahamiani sasa mtu kama huyu haja nialibia kweli tumekuwa wote kwa miaka 3
kaka unaonekana unaandika kwa hasira sana mpaka storuy imekuwa kama hatuelewi vizuri, pole mwaya hapo hujaharibiwa maisha wala nini, ndio kwanza umeanza nae, jipe mapumziko ili upone jeraha na uendelee na maisha, usimpe kichwa na kusema kaharibu maihsha yako mwili wako baado unaoJaman jana tu mwenzenu aliyekuwa mpz wangu wa miaka kansalit na mwaka huu ndio nimefanikiwa fanya nae mapenzi kwani alikuwa bikla na tumefanya tendo hili mara 2 tu chakushangaza mwezi ulio pita alisafili kwenda hom kwao kwan tuna kaa wilaya tofauti baada yakufika huko nikapigiwa sim na aliwekuwa mpz wake wa zaman kabla yangu akiniambia kuwa mpnz wangu ana tembea na rafiki yake na siku ana piga cm aliwakuta mara ya 3 wakitoka guest house mi nikaamua kumuuliza akanijibu ni maneno tu ya watu alafu hapo hapo akampigia sim jama aliyenipa taarifa na kumtukana sana kisha aka mpigia huyo jamaa yake mpya kumuuliza kama ameniambia japo mimi hatufahamiani sasa mtu kama huyu haja nialibia kweli tumekuwa wote kwa miaka 3
Michango mizuri wakuu.
Tukitoa wale wapumbavu ambao wanajua kabisa hawana malengo na mtu lakini wanaamua kuwa na mtu hili kukamilisha mambo yao binafsi,kuna mengine watu huwa wanajitakia wenyewe. Na mengi yameelezwa juu na wadau wengine mie ningependa kuongeza kwamba mawasiliano muhimu kwenye mahusiano yetu. Tuwe na moyo wa kuuliza pale tunapoona kasoro sio kukaa kimyaa mpaka siku inafika kwamba damage iliofanyika kubwa kihasi cha kuhisi kwamba maisha yako yameharibiwa.
Unapozungumza tatizo lolote na mpenzi wako mapema unampa nafasi ya kujirekebisha na unajipa nafasi wewe mwenyewe ya kufanya maamuzi mapema kama hato jirekebisha.
Ngoja nikae pembeni kwanza mpaka hili sredi lianze maofu topiki....kuna watu humu nna hasira nao sana!
Subiri............!
Hapo bold hapo umenikuna ipasavyo. Na hii tabia wanayo sana wababa kumng'ang'ania mtu ili mradi amchezee tu huku akijua dhahiri hana malengo nae.
Mi binafsi sipendi malawama nifanyapo maamuzi yangu, kwa hiyo ningependa kuheshimu maamuzi ya mwingine akiamua, sio kulalama tu umeharibiwa maisha, kwani mzazi wako huyo? mtu umekutana nae tu ukubwani lets say una miaka 25 then ukae nae miaka miwili useme kakuharibia maisha? umesahau miaka yote 25 uliyokuwa mwenyewe mwenye furaha?
Cha muhimu ni kuangalia wapi ulianguka ili usirudie tena kosa, na umshukuru mungu kwa uzima wako
Umeona eeehheee??
Mtu sononeka then anza maisha kwa sababu una moyo kama wengine, ila sio kulalama tu hadi kunywa dawa, for what umesahau hata wapendwa wako ulioishi nao tangu umezaliwa? hii ni kukufuru Mungu sasa... ndivo navochukulia maisha CPUNaomba uwe unawafundisha na wadada wengine wasiojua haya, hasa mabinti wadogo wanaochipukia ktk mahusiano
Na ukimkatalia kama alikua rafiki basi ujiandae huo urafiki unakufilia mbali, utanona tu anaanza kukuchunia nia, mwisho dah
Kwa kweli nawashangaaga sana wanaume katika hili na wala siwaelewagi kabisa.
Maty mambo mpenzi wiki imeanzaje? naona na wewe umeanza kuwaulumu.
Mtu sononeka then anza maisha kwa sababu una moyo kama wengine, ila sio kulalama tu hadi kunywa dawa, for what umesahau hata wapendwa wako ulioishi nao tangu umezaliwa? hii ni kukufuru Mungu sasa... ndivo navochukulia maisha CPU
Nilipata nafasi ya kuongea na mdada mmoja anaenda kwa jina la Maty nilipoenda kule alipo kwa ajiri ya Seminar fulani hivi. Muda mfupi nilioongea nae nikagundua AMEELIMIKA bila kupita darasani. She's stable in her mind. Kuoa mtu kama huyu ni raha mpaka basi.
Nadhani na wewe ndo wale wale kama huyu Maty . . . lolz
good girl, i can see you are getting stronger and strongerMi binafsi sipendi malawama nifanyapo maamuzi yangu, kwa hiyo ningependa kuheshimu maamuzi ya mwingine akiamua, sio kulalama tu umeharibiwa maisha, kwani mzazi wako huyo? mtu umekutana nae tu ukubwani lets say una miaka 25 then ukae nae miaka miwili useme kakuharibia maisha? umesahau miaka yote 25 uliyokuwa mwenyewe mwenye furaha?
Cha muhimu ni kuangalia wapi ulianguka ili usirudie tena kosa, na umshukuru mungu kwa uzima wako
Hahahaha lol, wiki imeanza vyema mpenzi, kuwalaumu ni lazima ili wajue wafanyacho si kizuri hata kidogo.
Imagine mtu anaanza kutaka kumdanganya mtu mzima maty akifikiri nina miaka 20 lol. Na kwa sababu nimeshapita huo umri wa kudanganyika mtu anakuchunia eti, mwe!
Hahahaha na kupata mume muelewa kama wewe ni raha sana asee lol, unajua nini CPU nimegundua ukitendwa mara mbili tatu ukitoka hapo unakuwa mkakamavu kupita maelezo, ila inabidi na hata wewe ujue una makosa fulani ulichangia na sio kulaumu tu