silent lion
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,161
- 1,540
Tujuzane Tafadhali.
Hivi kwa nn suala la umeme haliishi TZ ata aje Rais gani?
Hivi kwa nn suala la umeme haliishi TZ ata aje Rais gani?
*SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)*
*TAARIFA YA KATIZO LA UMEME LA DHARURA*
Shirika la Umeme Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wa Zanzibar na Mkoa wa Kinondoni Kaskazini kuwa, tumelazimika kuzima kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Kunduchi kuanzia Saa 4:00 Asubuhi hadi Saa 9:00 Alasiri.
*SABABU*
Kurekebisha mkondo wa "BREAKER" katika njia ya umeme ya msongo wa 132 Kunduchi- Zanzibar na kurekebisha "loose connection" katika njia ya umeme ya Ubungo- Kunduchi.
*MAENEO YANAYOATHIRIKA NI*
Zanzibar, Bagamoyo, Bunju, Madale, Kunduchi Beach, Mivumoni, Salasala, Bahari Beach, Kawe, baadhi ya maeneo ya Makongo juu, Tegeta, baadhi ya maeneo ya Mwenge, Kondo Village, Boko Magengeni, Ras Kilomoni, baadhi ya maeneo ya Boko, Masanja, Mbweni NHC Msaiti, Mbweni na maeneo jirani,
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Kwa mawasiliano
Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100
Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:
Mitandao ya kijamii
Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,
Facebook Tanesco Yetu
IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU
APRILI 18, 2018