Umejijengea GEREZA LAKO MWENYEWE

Umejijengea GEREZA LAKO MWENYEWE

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
19,147
Reaction score
43,079
Huwezi kuvaa nguo fulani sababu hawatakuelewa.

Huwezi kuishi mtaa fulani watakuona maskini sana au tajiri sana.

Huwezi kula pale kwasababu siyo hadhi yako.

Huwezi kuoa au kuolewa na mtu fulani siyo hadhi yako.

Huwezi kufanya kazi fulani sababu utaonekana umefeli kimaisha.

Huwezi kutumia simu aina fulani kwasababu za kitajiri sana au za kimaskini sana.

Huwezi kwenda beach wewe siyo mshamba wa maji.

Huwezi kwenda baa kukaa ukala au ukanywa wewe siyo malaya.

Hawezi kuwa rafiki yangu yule hana cha kunisaidia.

Umejiwekea sheria nyingi na kanuni nyingi za maisha yako ndiyo maana upo gerezani,upo katika kundi la wafungwa wanaotumikia kifungo cha nje. Upo kwenye shimo lako ulilojichimbia.

Umejawa na upweke,ukimya,huna marafiki wala ndugu,huna wa kwenda kumtembelea mkakaa wote siku nzima.

Umechagua kujitesa mwenyewe ndiyo maana unakasirika na kuchukia ukiona mlevi njiani.

Unakasirika ukiona watu wazima wanacheza mziki kwenye sherehe au baa au kwenye halaiki.

Ukisikia mtu katumia hela nyingi kwa ajili ya sherehe ya mwanae unaona hana akili.

Ukiona mtu anajenga nyumba kubwa unauliza sasa nyumba yote hii kubwa kwa ajili ya nani?

Toa hizo sheria na kanuni ulizojiwekea kuwa huru maisha ni mafupi sana furahia kila pumzi ya uhuru wako.
 
Hakika mkuu
20260228_153207.jpg
 
Uhakika asee. Kitu ninacho furahia mimi hata nisipokuwa na hela ni kutokujiwekea mipaka ya kifala kama hiyo uloitaja mkuu.

Kuna muda watu hushangaa wanaponiona nina tenga nauza nyanya sokoni😂

Muda mwingine huwa naulizwa wewe kazi uliacha au ulifukuzwa? Sasa nabaki najiuliza ina maana mimi sitakiwi kufanya hii kazi/biashara?

Ajabu hao wanaokushangaa unawazidi kila kitu hadi dhambi unaanza tena kuwaonea huruma sana watu aina hii.

Kuna mahali nilienda hivi karibuni moja ya mfanyakazi wangu alisema mimi nikipata kazi ya laki4 tu kwa mwezi siwezi kushika jembe haki ya mungu😅

Daaah visa ni vingi lakini ndo hivyo tena umepiga kwenye mshono kabisa.

GEREZA 📌📍
 
Uhakika asee. Kitu ninacho furahia mimi hata nisipokuwa na hela ni kutokujiwekea mipaka ya kifala kama hiyo uloitaja mkuu.

Kuna muda watu hushangaa wanaponiona nina tenga nauza nyanya sokoni😂

Muda mwingine huwa naulizwa wewe kazi uliacha au ulifukuzwa? Sasa nabaki najiuliza ina maana mimi sitakiwi kufanya hii kazi/biashara?

Ajabu hao wanaokushangaa unawazidi kila kitu hadi dhambi unaanza tena kuwaonea huruma sana watu aina hii.

Kuna mahali nilienda hivi karibuni moja ya mfanyakazi wangu alisema mimi nikipata kazi ya laki4 tu kwa mwezi siwezi kushika jembe haki ya mungu😅

Daaah visa ni vingi lakini ndo hivyo tena umepiga kwenye mshono kabisa.

GEREZA 📌📍
Yeah kazi kazi mkuu, hakuna kuremba hakuna kucheka na kima ila kazi na dawa🍻
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom