Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Jana Halmashauri kuu ya CCM, imefanya uteuzi wa wagombea ubunge Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania na uwakilishi katika Baraza la wawakilishi Zanzibar. Naungana na wanachama wenzangu wa CCM kumpongeza mwenyekiti, kamati kuu, halmashauri kuu na wagombea wote walioteuliwa.
Baada ya mchakato huu kumalizika, kama vijana tumejifunza nini? Hili ni swali muhimu sana haswa kwa wale wenye mipango ya kushiriki siasa za kugombea na kuteuliwa siku moja. Tathmini yangu ya uteuzi wa wagombea imenifundisha yafuatayo:
1. CCM haivumilii wasaliti wa ndani.
Ndugu January Makamba, Ummy Mwalimu, Luhaga Mpina, Ole Sendeka, Fred Lowassa hawa walisemwa semwa sana kumhujumu Mwenyekiti kwenye uteuzi wake na mgogoro wa ngorongoro. Kutokuteuliwa kwao kunatoa ujumbe muhimu sana, katika CCM, Mwenyekiti hajaribiwi.
2. Mwana mpotevu, akirudi CCM tutamkaribisha.
Esta Bulaya na wenzake walitoka CDM, hawakufanya vizuri kura za maoni. Ingawa uteuzi wao umelalamikiwa na baadhi ya makada kama Shayrose Banji, lakini umetoa ujumbe muhimu kwa wapinzani, CCM inawakaribisha tujenge pamoja.
3. Wasanii wana nafasi CCM
Kama ilivyokuwa kwa mwana FA 2020, Baba Levo ameteuliwa ingawa hakushinda kura za maoni. Ujumbe uliokusudiwa hapa ni mmoja, wasanii, mkikiunga mkono chama hakitawaangusha.
4. Ukitaka ubunge, ishi vizuri na wajumbe.
Ukiacha hayo niliyoyataja hapo juu, wagombea wote waliongoza kura za maoni, wameteuliwa kuwa wagombea. Hii maana yake ni nini? Ukitaka ubunge, ishi vizuri na wajumbe.
Hii ni tathmini yangu inayotoa mwelekeo wa nini vijana wanaotaka kushiriki siasa za nchi yao kupitia CCM wafanye kuzifikia ndoto zao.
Baada ya mchakato huu kumalizika, kama vijana tumejifunza nini? Hili ni swali muhimu sana haswa kwa wale wenye mipango ya kushiriki siasa za kugombea na kuteuliwa siku moja. Tathmini yangu ya uteuzi wa wagombea imenifundisha yafuatayo:
1. CCM haivumilii wasaliti wa ndani.
Ndugu January Makamba, Ummy Mwalimu, Luhaga Mpina, Ole Sendeka, Fred Lowassa hawa walisemwa semwa sana kumhujumu Mwenyekiti kwenye uteuzi wake na mgogoro wa ngorongoro. Kutokuteuliwa kwao kunatoa ujumbe muhimu sana, katika CCM, Mwenyekiti hajaribiwi.
2. Mwana mpotevu, akirudi CCM tutamkaribisha.
Esta Bulaya na wenzake walitoka CDM, hawakufanya vizuri kura za maoni. Ingawa uteuzi wao umelalamikiwa na baadhi ya makada kama Shayrose Banji, lakini umetoa ujumbe muhimu kwa wapinzani, CCM inawakaribisha tujenge pamoja.
3. Wasanii wana nafasi CCM
Kama ilivyokuwa kwa mwana FA 2020, Baba Levo ameteuliwa ingawa hakushinda kura za maoni. Ujumbe uliokusudiwa hapa ni mmoja, wasanii, mkikiunga mkono chama hakitawaangusha.
4. Ukitaka ubunge, ishi vizuri na wajumbe.
Ukiacha hayo niliyoyataja hapo juu, wagombea wote waliongoza kura za maoni, wameteuliwa kuwa wagombea. Hii maana yake ni nini? Ukitaka ubunge, ishi vizuri na wajumbe.
Hii ni tathmini yangu inayotoa mwelekeo wa nini vijana wanaotaka kushiriki siasa za nchi yao kupitia CCM wafanye kuzifikia ndoto zao.