ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Je, aliyedanganywa ndoa ana haki ya kudai fidia????
Kama ilivyo kwa Sheria za mikataba ambapo mtu anayetoa ahadi anapaswa kutekeleza, sheria ya ndoa pia inamtaka mtu anayetoa ahadi ya ndoa kutekeleza ahadi yake vinginevyo anaweza kudaiwa fidia kwa kuvunja ahadi ya ndoa.
Mtu aliyedanganywa ndoa (kuoa au kuolewa) anayo haki kisheria ya kudai fidia dhidi ya udanganyifu aliyofanyiwa.
Sheria ya Ndoa ya Tanzania inasema:
A suit may be brought for damages for the breach of a promise of marriage made in Tanganyika ( ) whether the breach occurred in Tanganyika or elsewhere, by the aggrieved party or, where that party is below the age of eighteen years, by his or her parent or guardian.
Ikumbukwe pia kuwa:
Kama ilivyo kwa Sheria za mikataba ambapo mtu anayetoa ahadi anapaswa kutekeleza, sheria ya ndoa pia inamtaka mtu anayetoa ahadi ya ndoa kutekeleza ahadi yake vinginevyo anaweza kudaiwa fidia kwa kuvunja ahadi ya ndoa.
Mtu aliyedanganywa ndoa (kuoa au kuolewa) anayo haki kisheria ya kudai fidia dhidi ya udanganyifu aliyofanyiwa.
Sheria ya Ndoa ya Tanzania inasema:
A suit may be brought for damages for the breach of a promise of marriage made in Tanganyika ( ) whether the breach occurred in Tanganyika or elsewhere, by the aggrieved party or, where that party is below the age of eighteen years, by his or her parent or guardian.
Ikumbukwe pia kuwa:
- Madai ya fidia ya kudanganywa ndoa hayamhusu mtua ambaye wakati alipoahidiwa alikuwa chini ya miaka kumi na nane (below the age of eighteen years). Kisheria mtu aliye chini ya miaka kumi na nane haruhusiwi kuingia kwenye mkataba isipokuwa kwa mikataba ya mahitaji ya lazima (necessaries) .
- Fidia itakayotolewa na Mahakama haitazidi kiwango halisi ambacho mdai atakuwa amegharimika kutokana na kuamini kwenye ahadi iliyovunjika (loss actually suffered as a result of expenditure incurred as a direct result of the promise)
- Madai ya jinsi hii pia hayapaswi kuwa ya kumlazimisha mtu aliyevunja ahadi ya ndoa kutekeleze ahadi hiyo ( specific performance).
- Madai ya jinsi hii yanapaswa kuwasilishwa Mahakamani katika kipindi kisichozidi miaka miwili tokea kuvunjika kwa ahadi na sio vinginevyo.