Umbwe Secondary high school Vs Loyola high school

Umbwe Secondary high school Vs Loyola high school

snps

Member
Joined
Jan 29, 2013
Posts
63
Reaction score
26
Ndugu wadau naomba ushauri wenu tafadhali.

Kijana wangu amepata nafasi ya kwenda kujiunga kidato cha tano katika shule ya umbwe secondary na masomo ya ECA. Lakini nilikuwa nimemwanzisha kusoma Loyola high school masom hayo hayo ECA. Nipo njia panda kuamua kuwa aende Umbwe au abaki Loyola. Nimecheki historia ya Umbwe wanafanya vizuri halikadhalia Loyola sio mbaya. Tofauti zao ni gharma zilizopo. Loyola ni gharama sana kulinganisha na Umbwe. Naomba wenye uzoefu na shule hizi mbili au yeyote yule.

Natanguliza shukrani zangu
 
Muache hapo Loyola,, coz kumuhamisha ni kudistabu akili yake jumla
 
Mwache aende umbwe ni best school Tanzania kwa hiyo combination hutajutia naifahamu
 
Nilisoma Umbwe, Loyola ni chamtoto. Nilisoma ECA darasa lote tulipata division 1
 
Umbwe ndo yenyew.a.k.a mti safi .shule yangu hiyo.eca imetulia sana
 
Akiwa loyola hata pata tu elimu ya darasani bali hata ya kijamii kuishi na watu yaani community servies
 
Nakushauri mwache asome Loyola High School na wala usijali kabisa kumwamishia huko Umbwe. Kwanini
1/Loyola ni miongoni mwa Private catholic day school zinazofanya vizuri sana hapa Tanzania kielimu. Ninaijua shule hii vizuri sana toka mwaka 1995 wakati inaanzishwa. Suala la kufaulu ni lazima na suala la kufeli halipo kabisa.

2/Loyola High School wana uhakika wa walimu wa kutosha na mazingira mazuri sana ya kielimu huenda kuliko shule nyingi sana.

3/Loyola High School wanaushindani mkubwa sana wa kusoma miongoni mwa wanafunzi, kuna kitu kinaitwa Cut off point kutoka kidato kimoja kwenda kingine.

NOTE
*Kufaulu kwa mwanafunzi kunategemea vitu vingi sana ikiwemo JUHUDI BINAFSI.
*Shule za serikali hazina tofauti sana kimatatizo. Mfano Chakula kibovu, Magonjwa ya mlipuko, Ukosefu wa walimu, ufuatiliaji duni wa kitaaluma.
*Ufaulu katika shule za serikali ni jambo lisiloweza kutabirika, trend zao hazieleweki kabisa.
*Shule za Private nyingi(Kama Loyola) ni gharama sana.
 
Thanks Kalichumbage. Naomba kama una contact yoyote maana hata sijapata joining instruction, thanks
 
Thanks Kalichumbage. Naomba kama una contact yoyote maana hata sijapata joining instruction, thanks
 
Hahahaaa. Loyola ilikuwa zamani bwana wakati wetu. Ila namshauri mtoa post amwache hapo ni shule nzuri hasa kimaadili kitaaluma pia. Ila ajipange kwa ada maana utafikiri unaagiza Premio japan
 
Mwenye contact za Umbwe sec naomba wandugu
 
Mpeleke umbwe..
Hapo loyola ajiandae kukosa mkopo
 
Back
Top Bottom