Umaskini wetu watanzania umesababishwa na Wazungu?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,305
33,924
Kila wakati na kila kiongozi mpya akiingia madarakani, inakuwa kama vile Tanzania ndiyo imezaliwa jana na yeye ndiye kiongozi wetu wa kwanza anayetokana na watanzania.

Mwalimu Juliusi Nyerere alipoingia tu madarakani, pamoja na mambo mengi sana aliyoyafanya na kuyajengea dhana, nadharia, na mipango mkakati, lakini aliwataja aliowaona kwamba ni maadui wa Tanganyika baadae Tanzania. Mwalimu alisema kuwa maadui wetu ni watatu, UJINGA, MARADHI NA UMASKINI.

Mwalimu baada ya hapo alikaa madarakani miaka 23 kabla ya kumkabidhi Mzee Ally Hassan Mwinyi. Mwinyi alipoingia tu alikabidhiwa "Ufagio wa Chuma" na wazee wa Dar es salaam ili afagie uozo uliokuwapo serikalini. Hapo tena utaona ni kama vile Mwinyi alipokea serikali iliyojaa uozo hadi kuhitaji kuwa na "ufagio wa chuma" ili kuufagia.

Mzee Mwinyi naye alipoondoka na kuingia Benjamini Mkapa, alikuja na kauli mbiu ya "Uwazi na Ukweli" kama vile kuonesha watangulizi wake hawakujali sana kuendesha mambo yao kwa uwazi na ukweli. Ni kama vile watangulizi wake kuna mambo walikuwa wanawaficha watanzania.

Alipoingia Kikwete na kupokea uongozi toka kwa Mkapa, yeye akaja na kauli mbiu ya "Kasi mpya, Nguvu mpya, Ari Mpya" kama vile aliingia na kuona kwamba wale waliotangulia kasi yao ilikuwa ndogo, nguvu dhaifu na wasiokuwa na hari. Waziri Mkuu wake Edward Lowassa akawa na msemo wake kwamba wanataka kuondoa tabia ya "Business as usual" serikalini.

Sasa tunaye Rais Magufuli ambaye ana kauli mbiu "hapa Kazi tu" ambayo kwa kweli mwanzoni mwa utawala wake ilishabikiwa sana na wafuasi wa CCM.

Lakini leo miaka 59 Tangu Tanganyika kupata Uhuru wake toka kwa Waingereza na miaka 53 Tangu mapinduzi ya Zanzibar lakini bado nchi yetu (Zetu?) ni Maskini. Kila mara ukiwasikiliza baadhi ya viongozi wetu ni kama vile tuko hivi tulivyo kwa kuwa "wakoloni" walitunyonya sana na "Mabeberu" wanatugandamiza tusisonge mbele kimaendeleo.

Hivi ni kweli kushindwa kwetu kupambana vizuri na wale maadui aliwaosema Mwalimu wa UJINGA, MARADHI na UMASKINI kunatokana na wazungu.Wazungu wanatuziaje kufanya mambo yetu ya kimaendeleo?
 
Matatizo yetu yote yanasababishwa na mzungu. Yani 😏😏😏 huo ndio mwisho wetu wa kufikiri.
Mimi sielewi ni kwa nini wao wasababishe. Kama ile mikataba feki ya kina Karl Peters tatizo sio wao bali ni letu. Ilikuwaje tukawa na viongozi wa aina ya kina Mangungo wa msowero? Yaani kwa nini Mzungu alikuwa ni Karl Peters na mwafrika akawa ni Mangungo?
 
Umasikini wetu umesababishwa na udhaifu wa TISS, mfumo mbovu wa kuchagua viongozi wa juu (hasa baada ya nyerere kustaafu) pamoja na elimu mbovu.

Kwa mtazamo wangu haya ndiyo mambo yanayofanya mpaka leo Tanzania iwe na iendelee kuwa maskini.
 
Umasikini wetu umesababishwa na udhaifu wa TISS, mfumo mbovu wa kuchagua viongozi hasa wa juu pamoja na elimu mbovu.

Kwa mtazamo wangu haya ndiyo mambo yanayofanya mpaka leo Tanzania iwe na iendelee kuwa maskini.
Sasa ni kwa nini huwa tunawataja sana wazungu kwamba wao ndio wanasababisha sisi kushindwa kufanya mambo yetu kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe??
 
Sasa ni kwa nini huwa tunawataja sana wazungu kwamba wao ndio wanasababisha sisi kushindwa kufanya mambo yetu kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe??
Marekani ni tajiri kwa sababu ana idara za usalama za kisasa na imara vivyo hivyo kwa china, russia na nchi za ulaya!!

Acha nikupe swali rahis, kama tungekua na elimu imara leo viwanda havikua vya kuwapa wahindi, tungekua na elimu nzuri leo hii tuna korona dawa hatuna watu wanakufa na hapa tunangoja mabeberu wagundue alafu watukopeshe (na tunajua baada ya mkopo kinafwata nini).

Hapa kwetu tutaendelea kulalamika tu ila ukiangalia vizuri yooote yana fall kwenye TISS, elimu mbovu na viongozi wanaopewa dhamana ya kuongoza nchi au idara za juu.
 
Kila wakati na kila kiongozi mpya akiingia madarakani, inakuwa kama vile Tanzania ndiyo imezaliwa jana na yeye ndiye kiongozi wetu wa kwanza anayetokana na watanzania.
Labda tuangalie hapa kwanza....

"...ila kiongozi mpya akiingia madarakani, inakuwa kama vile Tanzania ndiyo imezaliwa jana..."

Mpaka hapa utakubaliana na mimi kwamba kama taifa hatuna long term plan kama nchi, yani tunaongozwa na ilani za vyama which is stupid!!

Tulikua na kilimo kwanza, kikafia mbali! Tukaja kwenye gesi ya mtwara nayo ikafia mbali! Sasa tuna ndege guess what... nazo zitafia mbali!!

Kwa mataifa makubwa kwanza nchi inakua na sera yake, vyama zinajenga ajenda zao kwa kuangalia long term plan ya taifa!! kitu ambacho sisi hatufanyi!!

Yani tunafanya mark time, kila baada ya miaka 10 akija rais mpya tunaanza upya!! Mpaka hapa unatarajia maendeleo gani???

Sasa tunarudi kwenye point yangu ya awali...

Umaskini wa hii nchi unasabishwa na TISS (hawa ndio walitakiwa wawe mstari wa mbele kupigania long term plan za nchi na kama hamna waanze mpango wa kuandaa), mfumo mbaya wa kubata viongozi pamoja na elimu mbovu!!
 
Akili ya mwafrika haibadiliki maana kila kukicha ni kulaumu tu
Hata ashike uongozi mtu gani
Kwa nje atasema nikiwa kiongozi nahakikisha kila mtu atafaidi keki ya taifa na nchi itafika mbali
Kila kiongozi atajaribu kuweka mambo sawa ila baadae akiona kila kona wanaiba na yeye atasema to hell with that acha na Mimi nijilimbikizie tu
Hatutaweza kuacha kulalamika kuwa mzungu ndio sababu wakati huyo mzungu hana hata habari na sisi
Kama hatutaacha wizi na rushwa itatuchukua miaka hata 400 na bado tutakuwa masikini tu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Yaani ukoloni mambo leo unatulazimisha sisi kuwa na mipango ya hovyo ama matumizi yasiyoeleweka kwenye fedha za kodi za watanzania??
Tunarudi pale pale, mfumo mbovu wa uongozi + TISS mbovu!!

Huwezi ukawa na TISS imara alafu yakatokea madudu ya EPA, ESCROW na matumizi mengine mambovu ya fedha yaliyotokea na yanayotokea!!

Pia huwezi kuwa na viongozi bora kama huna TISS bora.

Na huwezi kuwa na TISS imara wala huwezi kuwa na mfumo imara wa uongozi kama huna mfumo bora wa elimu!!!

It's just not gonna happen! Never!
 
Kila wakati na kila kiongozi mpya akiingia madarakani, inakuwa kama vile Tanzania ndiyo imezaliwa jana na yeye ndiye kiongozi wetu wa kwanza anayetokana na watanzania.

Mwalimu Juliusi Nyerere alipoingia tu madarakani, pamoja na mambo mengi sana aliyoyafanya na kuyajengea dhana, nadharia, na mipango mkakati, lakini aliwataja aliowaona kwamba ni maadui wa Tanganyika baadae Tanzania. Mwalimu alisema kuwa maadui wetu ni watatu, UJINGA, MARADHI NA UMASKINI.

Mwalimu baada ya hapo alikaa madarakani miaka 23 kabla ya kumkabidhi Mzee Ally Hassan Mwinyi. Mwinyi alipoingia tu alikabidhiwa "Ufagio wa Chuma" na wazee wa Dar es salaam ili afagie uozo uliokuwapo serikalini. Hapo tena utaona ni kama vile Mwinyi alipokea serikali iliyojaa uozo hadi kuhitaji kuwa na "ufagio wa chuma" ili kuufagia.

Mzee Mwinyi naye alipoondoka na kuingia Benjamini Mkapa, alikuja na kauli mbiu ya "Uwazi na Ukweli" kama vile kuonesha watangulizi wake hawakujali sana kuendesha mambo yao kwa uwazi na ukweli. Ni kama vile watangulizi wake kuna mambo walikuwa wanawaficha watanzania.

Alipoingia Kikwete na kupokea uongozi toka kwa Mkapa, yeye akaja na kauli mbiu ya "Kasi mpya, Nguvu mpya, Ari Mpya" kama vile aliingia na kuona kwamba wale waliotangulia kasi yao ilikuwa ndogo, nguvu dhaifu na wasiokuwa na hari. Waziri Mkuu wake Edward Lowassa akawa na msemo wake kwamba wanataka kuondoa tabia ya "Business as usual" serikalini.

Sasa tunaye Rais Magufuli ambaye ana kauli mbiu "hapa Kazi tu" ambayo kwa kweli mwanzoni mwa utawala wake ilishabikiwa sana na wafuasi wa CCM.

Lakini leo miaka 59 Tangu Tanganyika kupata Uhuru wake toka kwa Waingereza na miaka 53 Tangu mapinduzi ya Zanzibar lakini bado nchi yetu (Zetu?) ni Maskini. Kila mara ukiwasikiliza baadhi ya viongozi wetu ni kama vile tuko hivi tulivyo kwa kuwa "wakoloni" walitunyonya sana na "Mabeberu" wanatugandamiza tusisonge mbele kimaendeleo.

Hivi ni kweli kushindwa kwetu kupambana vizuri na wale maadui aliwaosema Mwalimu wa UJINGA, MARADHI na UMASKINI kunatokana na wazungu.Wazungu wanatuziaje kufanya mambo yetu ya kimaendeleo?
When do we take responsibility for our own destiny? When we do that, we will realise that our fate is in our own hands
 
Kwanza ondoa hiyo ya kusema Nchi yetu eti ni maskini, siyo kweli,

Nchi yetu si maskini Ila watu wake ndio maskini

Na umaskini wa watu wa Tanzania, unaweza kuwa umechangiwa na vitu vingi Sana, kubwa kabisa ni Ujinga, na Ujinga unaweza ukaanzia hata Kwa mleta mada, kushindwa kuelewa Kati ya nchi ambayo ndiyo Aridhi na Mali asili zake ktk Aridhi, watu wanaoishi ktk nchi yaani Aridhi hiyo

Baada ya kuona kwamba, Nchi inayokaliwa na watu hao ina ina vitu gani, unaangalia watu wake,

...Je, maliasili za nchi Yao watu wanazijua?,
..Je,Wanajibidiisha Kwa kuzalisha ili ziwape matokeo?
..Je katika swala la Elimu nalo likoje?
..Je uthubutu wa kufanya mambo ukoje?
..Je siasa za nchi hiyo nazo zikoje?
..Uwezo wa kukabiliana na mazingira upo?

Sasa, ukute vitu Vyote vya mhimu Huna, utakuwaje na watu ambao si maskini?

Sasa ukute, Elimu nzuri ipo, Nchi inautajiri, Siasa Safi ipo, Ila ukawa na watu wavivu, Wala rushwa, majizi, Utakuwa na watu wasio masikini Kwa mbinu gani?

Beberu hajawahi kuwa ndio sababu ya umaskini wetu, Ingawa anaweza pia kuwa sababu Kwa vigezo Fulani!

Sisi umaskini unachangiwa na vitu vingi Sana, Ulaphi wa madaraka nao pia huchangia, kutokuwa na umoja, Siasa zetu, uwoga, na ushenzi mwingi hasa wa kisiasa na Baadhi ya viongozi ktk Vyama

Endapo tukiamua, kuondoa tofauti zetu za kisiasa, tukafanikiwa kudhibiti Kwa dhati wizi wa maofisini, rushwa na uvivu makazini, miaka mitano ni mingi, tayari tunakuwa mbaaali Sana
 
Back
Top Bottom