Umaskini wa mkoa wa Kagera

Hewa mkaa

JF-Expert Member
Sep 3, 2012
742
377
Mkoa wa Kagera hasa Bukoba kuna umasikini wa kufa mtu. Wahaya walioko Dar ni wanafiki tu lakini huko kwao ni shida tu. Hali hii imeletwa na wanakabila hawa kutokupokea kwa njia iliyo chanya mabadiliko yanayoweza kuleta maendeleo. Kwa mfano kung'ang'ania kilimo cha migomba kwa miongo mingi kumewafanya wahaya kukataa mazao yanayotumia nguvu kazi nyingi. Kwa mfano mahindi, ulezi na mtama. Mazao haya yangesaidia pia kuleta crop rotation ambayo faida zake ni pamoja na kupungua magonjwa na wadudu waharibifu. Mazao haya pia pamoja na maharage ni ya cycle ya miezi mitatu mitatu ambayo huwa inaharakisha mzunguko wa pesa. mazao haya pia yanatunzika kwa muda mrefu na kuongezeka thamani jinsi njaa inavyoongezeka sehemu za jirani. Wahaya wanatakiwa kufunguka akili kuliona hili. Nimewahi kutembea sehemu za Magamba na Lwati huko Mbozi. Watu wametajirika kutokana na kilimo cha mazao haya. Hawachachi. Ukifika kwenye ofisi ya kijiji ambapo ni commercial center utakuta watu wanakula na kunywa. Mbuzi zaidi ya watatu huchinjwa kila siku. Nyumba zote ni tofali za kuchoma. Kila mwanakijiji yuko vizuri. Shime Wahaya tulione hili. 'Mpao'
 
Nakushukuru mtoa mada kwa kutujuza uloyaona. ukweli ni kuwa maeneo mengi ya bk yameharibika sana kiikolojia. ardhi ambacho ndo chanzo cha utajiri imeharibika viabaya. haiwezi kuotesha mahindi, ndizi hata mihogo ni ya kubahatisha sana. ishu hapa ni ukosefu wa maarifa, kwanza namna ya kurejesha hali ya asili na pia mtaji wa jinsi wa kurejesha rutuba ya asili. shime wasomi wote wa kagera, mambo ya kujifanya hamhusiki na mambo ya kwenu ni unafiki na ujinga, rudini kwenu mkatoe elimu, wahaya wanakufa kwa njaa na utapiamlo. ebo!
 
Nakushukuru mtoa mada kwa kutujuza uloyaona. ukweli ni kuwa maeneo mengi ya bk yameharibika sana kiikolojia. ardhi ambacho ndo chanzo cha utajiri imeharibika viabaya. haiwezi kuotesha mahindi, ndizi hata mihogo ni ya kubahatisha sana. ishu hapa ni ukosefu wa maarifa, kwanza namna ya kurejesha hali ya asili na pia mtaji wa jinsi wa kurejesha rutuba ya asili. shime wasomi wote wa kagera, mambo ya kujifanya hamhusiki na mambo ya kwenu ni unafiki na ujinga, rudini kwenu mkatoe elimu, wahaya wanakufa kwa njaa na utapiamlo. ebo!
ngoja kwanza niwasiliane na brother RWEGOSHORA anambie kama yale makontena yngu yameshafika bandarin.
 
Mkoa wa Kagera hasa Bukoba kuna umasikini wa kufa mtu. Wahaya walioko Dar ni wanafiki tu lakini huko kwao ni shida tu. Hali hii imeletwa na wanakabila hawa kutokupokea kwa njia iliyo chanya mabadiliko yanayoweza kuleta maendeleo. Kwa mfano kung'ang'ania kilimo cha migomba kwa miongo mingi kumewafanya wahaya kukataa mazao yanayotumia nguvu kazi nyingi. Kwa mfano mahindi, ulezi na mtama. Mazao haya yangesaidia pia kuleta crop rotation ambayo faida zake ni pamoja na kupungua magonjwa na wadudu waharibifu. Mazao haya pia pamoja na maharage ni ya cycle ya miezi mitatu mitatu ambayo huwa inaharakisha mzunguko wa pesa. mazao haya pia yanatunzika kwa muda mrefu na kuongezeka thamani jinsi njaa inavyoongezeka sehemu za jirani. Wahaya wanatakiwa kufunguka akili kuliona hili. Nimewahi kutembea sehemu za Magamba na Lwati huko Mbozi. Watu wametajirika kutokana na kilimo cha mazao haya. Hawachachi. Ukifika kwenye ofisi ya kijiji ambapo ni commercial center utakuta watu wanakula na kunywa. Mbuzi zaidi ya watatu huchinjwa kila siku. Nyumba zote ni tofali za kuchoma. Kila mwanakijiji yuko vizuri. Shime Wahaya tulione hili. 'Mpao'

Binafsi nakubaliana na wewe kwa utafiti wako. Nafikiri ma afisa kilimo wako kila Wilaya kwa Mkoa mzima wa Kagera kwa ajili ya kutoa ushauri kama huu kwa wakulima. Sidhani hawa akina 'nshomile' walioko Dsm watasaidia sana ktk hili! Sielewi hawa ma DALDO wanafanya nini cha maana zaidi ya kukaa kwenye stuli ndefu kwenye baa na kusibiri mishahara wasiyoifanyia kazi!
 
Back
Top Bottom