Hewa mkaa
JF-Expert Member
- Sep 3, 2012
- 742
- 377
Mkoa wa Kagera hasa Bukoba kuna umasikini wa kufa mtu. Wahaya walioko Dar ni wanafiki tu lakini huko kwao ni shida tu. Hali hii imeletwa na wanakabila hawa kutokupokea kwa njia iliyo chanya mabadiliko yanayoweza kuleta maendeleo. Kwa mfano kung'ang'ania kilimo cha migomba kwa miongo mingi kumewafanya wahaya kukataa mazao yanayotumia nguvu kazi nyingi. Kwa mfano mahindi, ulezi na mtama. Mazao haya yangesaidia pia kuleta crop rotation ambayo faida zake ni pamoja na kupungua magonjwa na wadudu waharibifu. Mazao haya pia pamoja na maharage ni ya cycle ya miezi mitatu mitatu ambayo huwa inaharakisha mzunguko wa pesa. mazao haya pia yanatunzika kwa muda mrefu na kuongezeka thamani jinsi njaa inavyoongezeka sehemu za jirani. Wahaya wanatakiwa kufunguka akili kuliona hili. Nimewahi kutembea sehemu za Magamba na Lwati huko Mbozi. Watu wametajirika kutokana na kilimo cha mazao haya. Hawachachi. Ukifika kwenye ofisi ya kijiji ambapo ni commercial center utakuta watu wanakula na kunywa. Mbuzi zaidi ya watatu huchinjwa kila siku. Nyumba zote ni tofali za kuchoma. Kila mwanakijiji yuko vizuri. Shime Wahaya tulione hili. 'Mpao'