Ulinisaliti Juliet

Ulinisaliti Juliet

Shunie

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
157,054
Reaction score
463,971
Mtunzi Nyemo Chilongani SEHEMU YA 01

Sijui nianze kusema nini ili nieleweke, sijui kama ninatakiwa kucheka au kulia kwani kwa kile kilichotokea, ningependa Mungu anisemehe tu.

Kwa jina ninaitwa Steven Edward, mimi ni kijana niliyebahatika kupata msichana mzuri aitwaye Juliet ambaye baadae alikuja kuwa mke wangu niliyempenda sana kabla mambo hayajakwenda kombo.

Kwa Juliet, nilikuwa nimefika, alikuwa mwanamke niliyempenda kuliko wanawake wote duniani, nilimthamini na kumsikiliza kwa kuwa sikuwa na mwingine zaidi yake.

Juliet alikuwa mzuri kila mahali, tukianzia nje mpaka ndani (Nadhani hapo unaelewa namaanisha nini).

Nilidumu na Juliet kwa miaka minne ya ndoa, hakuchuja, bado alikuwa mzuri vilevile, nahisi kwa sababu nilikuwa na fedha hivyo mambo madogomadogo ya make up yalikuwa yakinunuliwa sana.

Nilipoona kwamba kila siku nazidi kulewa kwa mapenzi yake, nikaamua kumnunulia gari la kifahari. Juliet akawa Juliet bwana, mtaani alikuwa akitamba yeye tu. Ana usafiri wa maana, hakanyagi tena ardhini kwa kutembea mwendo mrefu, sasa kwa nini asinione mimi wa thamani?

Ukiachana na gari, nilimnunulia vitu vingi ambavyo alitakiwa kuwa navyo huku nikimfungulia biashara nyingi zilizomfanya kufurahia maisha yake.

Daah! Juliet mke wangu! Hivi ulikosa nini wewe shetani? Au ulitaka nikufanyie nini ili ujue nakupenda?

(Nanyamaza na kuanza kulia kwa pozi, kisha naendelea)
Baada ya kukatika miaka minne ya ndoa yetu huku tukiwa tumepata mtoto wa kike, Magreth, mwaka 2012 ukaingia, siku hiyo ndiyo ilikuwa mwanzo wa majanga yote yaliyosababisha haya yote, ngoja nijaribu kukusimulia, nitakapoishia, naomba mnisamehe kwa kuwa jambo hili linaniuma kupita kawaida.

JANUARI 1

Siku hii ilianzia usiku, nakumbuka siku hiyo nilikuwa na Juliet chumbani kwetu huku tukiwa tumekumbatiana na kupeana mabusu mfululizo. Tulitaka mwaka mpya wa 2012 utukute tukiwa tumekumbatiana namna hiyo.

Kweli bwana, saa ilipogonga na kutuambia kwamba ilikuwa ni saa sita kamili usiku huku siku ikiwa imebadilika, nikammwagia mabusu zaidi.

“Ninakupenda mke wangu,” nilimwambia.
“Ninakupenda pia.”



Screenshot_20181024-163307.jpeg
 
SEHEMU YA 02

Hatukuridhika, tulichokifanya ni kutoka chumbani kwetu na kuelekea chumbani kwa mtoto wetu, Magreth. Tulipofika, tukabaki tukimwangalia tu kwani alikuwa amelala, tukamfuata na kumpiga mabusu mfululizo.

Asubuhi ilipofika, tukaelekea kanisani na baadae kurudi nyumbani. Mfanyakazi aliandaa chakula kizuri, tukala na kisha kutoka kwenda ufukweni, nakumbuka ilikuwa Msasani. Huko, tukayafurahia maisha yetu kwa ujumla, hakika ilikuwa siku nzuri kwetu.

JANUARI 2
Siku hii ilikuwa ni Jumatatu tulivu, sikwenda kazini siku hiyo, niliamua kubaki nyumbani ili kuwa na familia yangu. Bado nilihitaji muda zaidi wa kuwa na familia yangu ambayo ilikuwa na mapenzi ya dhati kwangu.

Maisha yalikuwa matamu mno kwani wote tulikuwa tukiyafurahia maisha kama kawaida.

Mchana hatukutaka kutoka, tulikuwa nyumbani huku tukitazama muvi ambazo kwa kiasi fulani zilituweka karibu sana.

Mpaka usiku tunalala, tulikuwa kwenye amani kubwa, kila siku nikawa namwambia mke wangu kwamba hakukuwa na mwanamke mzuri kama yeye....Oooh! Juliet wangu nikupendae!

JANUARI 3
Siku hii nikaamua kuanza kazi rasmi. Niliamka asubuhi sana na kujiandaa kuelekea kazini. Nilipomaliza kunywa chai iliyoandaliwa na mke wangu, nikapanda garini na kuelekea kazini.

Nilipofika, nikatulia na kuendelea kufanya kazi kama kawaida. Siku hii haikuwa ya kawaida, toka nimefika kazini saa mbili asubuhi, mpaka saa tano mke wangu hakuwa amenicheki simuni.

Unajua hili halikuwa jambo la kawaida kabisa, nilikwishazoea kwamba kila ninapofika kazini huwa mke wangu ananijulia hali kama nimefika salama au la, ananitania kwa maneno ya hapa na pale na kisha kuniacha.

Leo, hali ilikuwa tofauti sana, nilisubiri simu yake ili anichokozechokoze kwa vineno vyake vitamu lakini hali ilikuwa kimya, kila aliyepiga simu, hakuwa Juliet.
 
SEHEMU YA 03

Moyoni nikakosa amani, nikahisi kama kulikuwa na jambo zito lilitokea nyumbani, nilichokifanya ni kurudi nyumbani ili nijue kuna nini. Nikatoka ofisini na kuelekea nyumbani.

Sikutaka kumwambia mke wangu kwamba nilikuwa nikirudi nyumbani, nilitaka kumfanyia ‘suprise’ tu.

Hata gari sikutaka kulichukua, kwa ubosi wangu, nikapanda daladala, usafiri ambao kwa mara ya mwisho niliupanda miaka kumi iliyopita.

Nilipofika nyumbani, nikapiga hodi na mlinzi kuja kunifungulia. Uso wake ulikuwa na wasiwasi, hakuonekana kujiamini jambo lililonifanya kuwa na hofu kwa kujiuliza nini kilikuwa kikiendelea.

“Mbona upo hivyo Mchichi?” nilimuuliza.
“Nipo kawaida tu bosi.”
“Sawa. Hakuna noma. Shemeji yako yupo?”

“Ndiyo kaka, yupo ndani.”
Nikapiga hatua na kuelekea ndani, nilipofungua mlango, nikapigwa na butwaa kumkuta rafiki yangu wa kitambo, Christopher akiwa sebuleni amejiachia.

Sikufichi, nilishtuka mno kwani haikuwa kawaida kwa Christopher kunitembea bila kunitaarifu simuni, hata yeye aliponiona, akapigwa na mshtuko japokuwa alijitahidi sana kuuficha mstuko wake.

“Christopher!!” niliita kwa mshtuko.
“Niambie Steve, mtoto wa vitoto,” aliniambia huku akijichekesha.

“Hahah! Mzee wa vitoto wapi na wakati niliachana navyo toka miaka minne iliyopita. Karibu sana,” nilimwambia huku nikimpa mkono.

Hata kabla hajanishukuru kwa kumkaribisha, mke wangu, Juliet akatokea hapo sebuleni. Kama ilivyokuwa kwa Christopher, naye akashtuka, akajitahidi kutokuonyesha mshtuko wake lakini wapi.

Hakika sichoki kumsifia mke wangu, siku hiyo alipendeza mno, sikuamini kama kuna siku angeweza kupendeza namba hiyo. Nilifurahi sana, nikaanza kumsogelea.

“Mume wangu! Mbona umekuja kwa kushtukiza hivyo?” aliniuliza, sikutaka kujibu kwanza, nikamkumbatia na kumpiga mabusu mfululizo usoni.
“Nimekukumbuka mke wangu.

Unanukia vizuri,” nilimwambia huku mikono yangu ikiwa imemkumbatia vilivyo.
“Nakupenda pia mume wangu. Karibu.”
“Asante.”

Alichokifanya ni kukaa kochini.
“Umependeza mno, unatoka?” nilimuuliza.
“Hapana. Nimerudi kutoka shuleni, nilimpeleka Magreth.”

“Sawa. Karibu mgeni,” nilimwambia Christopher, nikainuka na kwenda chumbani nikiwaacha wawili hao sebuleni.
 
SEHEMU YA 4

Moyo wangu haukuwa sawa kabisa, nilikuwa nikifikiria ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea lakini sikupata jibu. Muonekano wa mke wangu, Juliet ulinishangaza sana, sikuamini kama kweli alikuwa amerudi kutoka shuleni au la, yaani majibu yake yalinipa wasiwasi kwa sababu:

Moja! Ilikuwaje awe ametoka kumpeleka mtoto shuleni na wakati muda huo ilikuwa ni saa sita kasoro mchana? Kwa kawaida mtoto anakwenda saa mbili asubuhi, iweje awe ametumia muda wote huo kutoka shuleni hadi nyumbani na hapakuwa mbali?

Mbili! Jukumu la kumpeleka Magreth shuleni lilikuwa ni la mfanyakazi, tena alikuwa akimfikisha kituoni, anasubiri gari na linakuja kumchukua, ilikuwaje leo hii yeye ndiyo aende kumpeleka Magreth shuleni?

Mbali na maswali hayo yote, aliniambia kwamba ndiyo ametoka kumpeleka Magreth shuleni, lakini mbona muonekano wake ulionyesha kwamba ndiyo kwanza ametoka kujiandaa, yaani alikuwa msafi kabisa, hata viatu vyake vilikuwa visafi.

Nilichokifanya ni kwenda katika bafu la chumba chetu, kitu cha kwanza nikaigusa sabuni, ilikuwa imelowa kabisa yaani ilionyesha kwamba ilitoka kutumiwa muda si mrefu, na hata nilipoligusa taulo lake, lilikuwa vilevile, sasa ilikuwaje aniambie kwamba alitoka shuleni kumpeleka magreth? Nilikuwa na maswali yasiyokuwa na majibu.

Kiukweli nikabadilika, nilichokifanya ni kutoka chumbani na kurudi sebuleni, wote wawili walionekana kuwa na mashaka, sikutaka kujali kihivyo, si unajua Christopher alikuwa mshikaji wangu, nikakaa nao sebuleni huku tukipiga stori mbili tatu kisha jamaa kuaga, nikabaki na mke wangu.

“Nakupenda mpenzi,” nilimwambia kwa hisia zote, ulikuwa muda wa kulala.
“Nakupenda pia,” aliniambia na kunikumbatia.

Siku hiyo ya Jumatatu ikapita na siku nyingine kuingia.
 
SEHEMU YA 05

Januari 4
Niliamka asubuhi huku nikiwa na mawazo tele, matukio kadhaa yaliyotokea siku iliyopita yalinichanganya mno, nilihisi maumivu makubwa moyoni mwangu japokuwa sikuwa nimeujua ukweli wowote ule.

Nilimpenda sana mke wangu na ndiyo maana kila nilipokuwa nikiona kitu hakiendi sawa, nilikuwa radhi kumuuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
Miaka yote hiyo, kitu nilichokijua ni kwamba mke wangu, Juliet alikuwa mwaminifu, kama kulikuwa na usaliti aliokuwa akiufanya, sijui, lakini wala sikuwa nikigundua kitu chochote kile.

Moyo wangu ulikosa amani kabisa, sikuwa na furaha hata mara moja, kila nilipokuwa nikijiandaa kwa ajili ya kwenda kazini, kichwa changu hakikuwa sawa kabisa.
“Mume wangu..!” aliniita Juliet.
“Naam.”

“Mbona upo hivyo?” aliniuliza kwa sauti ya upole.

“Nipo vipi?” niliuliza huku nikijitahidi kutoa tabasamu lakini wapi, halikuwa likija.

“Unaonekana una mawazo sana, tatizo nini jamani?”
“Mbona nipo sawa tu.”
“Kweli?” “Yaap.”

Juliet alinifahamu sana, toka tumeishi kwa miaka minne, alikuwa akinijua kwa undani sana, nilipokuwa na furaha alinielewa na hata nilipokuwa sina furaha, alijua hivyo.

Siku hiyo nilipokuwa nikimdanganya, alifahamu kwamba nilikuwa nikimdanganya lakini hakutaka kuuliza zaidi.

Hata nilipowekewa chai asubuhi ninywe, chai haikuwa na radha kabisa.
Nikaanza kuingia kwenye maisha mapya, kuishi na mtu ambaye umeanza kumtilia wasiwasi ulikuwa kama kuubeba msalaba usioweza kutokana na uzito wake kuwa mkubwa.

Mpaka naondoka kuelekea kazini, bado akili yangu haikuwa sawa kabisa, bado nilikuwa na mawazo lukuki.

Nilipofika ofisini nikatulia, wakati mwingine nilikuwa nikijuta kwa sababu gani niliamua kumpenda Juliet na kumuoa na wakati kulikuwa na wasichana wengi waliokuwa wakinipenda, ila katika yote hayo, sikutakiwa kulalamika, huo ulikuwa ni muda wa mapambano.

Ofisi hakukukalika kwa raha, nilichokifanya ni kuondoka kuelekea katika Mghahawa wa Chagga Bites ambapo hapo nikaagiza chakula na kuanza kula, japokuwa hakikuwa na radha, nikajitahidi hivyohovyo mpaka kikaisha.
 
SEHEMU YA 06

Sikutaka kurudi ofisini, unajua unapompenda mtu unakuwa tofauti kabisa hasa linapokuja suala la kukusaliti. Nilichokifanya ni kuelekea ufukweni na kutulia.

Mke wangu, Juliet alijitahidi sana kunipigia simu lakini sikuwa na nguvu ya kupokea, nilikuwa naiangalia kisha naachana nayo.

Ilipofika usiku, nikaondoka na kuelekea nyumbani huku kichwa hcangu kikiwa tofauti sana. Nilipofika, nikajitupa kitandani kwani mke wangu alikuwa akioga bafuni.

“Please, read a message” ilisikika sauti ya msichana simuni mwa mke wangu, alikuwa ameuweka mlio huo uwe wa kuitia mara meseji inapoingia simuni.

Nilichokifanya, kwa kuwa nilikuwa huru na simu ya mke wangu, nikachukua simu ile na kuufungua, nikaanza kuusoma.

“Unajua, unajitahidi sana, sikuamini kwa mara ya kwanza, kumbe mtu kama wewe upo katika dunia hii!

Aisee, wewe ni noma sana, umetishaaa, kiuno chote kinauma,” ilisema sehemu ya meseji hiyo.

Sijui nikwambie nini, sijui niseme nini ili upate kunielewa ni kwa jinsi gani nilikuwa nimeumizwa moyoni.

Nikahisi mwili ukitetemeka kwa hasira huku kijasho chembamba kikianza kunitoka.

Mwili ulikuwa ukitetemeka kupita kawaida, sikuamini kama ningeweza kukutana na meseji kama hiyo.

Sikutaka kujiuliza kwamba meseji hiyo ilitoka kwa nani, nilijua huyo mtumaji alikuwa mwanaume na walikuwa wamefanya mapenzi.

Pasipo kutarajia nikajikuta nikitokwa na machozi. Nilichokifanya ili kupata ushahidi wa kila kitu, nikaifoward meseji ile simuni mwangu na kisha kuipeleka kwenye email yangu na kisha kuifuta simuni mwake.

Nilichokuwa nikihitaji ni kupata uhakika tu juu ya mtumaji wa meseji ile, nilipoichukua ile namba na kuipiga simuni mwangu, jina la Chris lilikuwa likionekana, kwa maana hiyo namba ile hata mimi nilikuwa nayo, ilikuwa ni namba ya Christopher.

“Ooopppsss....” nilijikuta nikishusha pumzi kwa nguvu.
Sikutaka kuendelea kukaa chumbani, nilichokifanya ni kuondoka na kuelekea baa.

Huko nilibaki nikibubujikwa na machozi mfululizo, mke wangu niliyekuwa nikimuamini, leo hii alikuwa akinisaliti, mbaya zaidi alinisaliti kwa mtu niliyekuwa nikimwamini sana, Christopher.
 
SEHEMU YA 07

“Wanawake ni wapumbavu sana, hivi mwanamke apewe nini ili atulie?” nilijiuliza bila kupata majibu yoyote yale.

Fikra zangu zikaanza kuunganisha matukio kwamba mke wangu alikuwa ametoka kufanya mapenzi na Christopher na ndiyo maana alikuwa bafuni akioga kujisafisha, niliumia zaidi.

Mke wangu alikuwa akinipigia simu mara kwa mara lakini sikutaka kuipokea kabisa, ilipofika saa nne usiku tena huku nikiwa na pombe kichwani nikarudi nyumbani.
“Ulikwenda wapi?” aliniuliza kwa sauti ya chini.
“Niache nilale.”

“Kuna nini mpenzi? Toka lini umeanza kunywa pombe?”
“Naomba uniache nilale,” nilisema kwa ukali kidogo.

“Niambie kwanza. Nikakuandalie maji ya kuoga?”
“Hapana. Niache nilale,” nilimwambia na kupitiwa na usingizi.

JANUARI 5
Nilikuwa mtu wa kuhuzunika tu, mapenzi yaliutesa moyo wangu kupita kawaida, kuwa na mke ndani ya nyumba huku ukijua kwamba alikuwa akikusaliti lilikuwa suala lenye kuumiza mno.

Asubuhi hiyo nikajifanya kuleta unafiki mkubwa japokuwa lilikuwa suala gumu, kwanza nikajidai nipo kawaida mno kana kwamba hakukuwa na kitu kilichokuwa kimetokea.

Niliamua kufanya hivi kwa sababu nilitaka kumkamata kwa urahisi sana.

Endapo ningeendelea kuwa kwenye hali ya mawazo basi ilikuwa ni lazima ajue kwamba nimeanza kufahamu kila kitu, sasa ili kumtia upofu, nikajifanya nipo kawaida tu japokuwa moyo wangu ulilipuliwa sana.

“Hivi jana nilikunywa?”
“Ndiyo.

Umekuja hapa una mahasira yako weee,” aliniambia.
“Lakini sikukupiga?”
“Ndiyo, haukunipiga.”

“Asante Mungu. Nimeamka kwa nguvu mpya, niandalie chai kwanza ninywe.”
Nilimwambia, nadhani hata na yeye alishangaa sana kwani siku hizi mbili, siku hiyo nilionekana tofauti sana. Akaenda kuniandalia chai huku nikioga.

Maumivu hayakupungua moyoni na suala la kuleta unafiki kwamba nilikuwa na furaha yalikuwa ni moja ya maigizo yenye kuumiza sana. Nilipomaliza kuoga nikavaa na kuelekea kunywa chai, kila nilipomwangalia, nilikuwa nikitabasamu tu.

“Malaika wangu! Kila siku unazidi kuwa mrembo tu, unaonekana mbichiiiii,” nilimwambia kwa kumsifia, uso ulijawa na tabasamu ila moyo ulikuwa ukiwaka moto kwa hasira.
 
SEHEMU YA 8

“Hahah! Asante mpenzi, na wewe unakuwa mzuri sana siku hizi,” aliniambia.
“Nashukuru, yote haya ni matunzo yako kipenzi,” nilimwambia na kutoa tabasamu pana la kinafiki.

Asubuhi hiyo kila mmoja akaonekana kuwa na furaha, hakujua kwamba kila kitu nilichokuwa nikikifanya kilikuwa ni kukamilisha upelelezi niliokuwa nikitaka kufanya.

Tayari nilikuwa na nusu ya ushahidi lakini nilitaka kufahamu mengi zaidi, hivyo nilitakiwa kuwa kwenye hali ya kawaida bila kujifanya kwamba ninakuwa kwenye huzuni wakati wote.
Nilipomaliza kunywa chai nikaondoka na kuelekea kazini.

Kazi hazikufanyika, akili yangu ilikuwa imekwishachanganyikiwa kabisa, wakati mwingine nilitamani kama ningekuwa Muislamu, yaani lingekuwa jambo rahisi tu kumpa talaka yake na kuniacha nikiwa home peke yangu, ila kilichokuwa kikinizuia ni kwa sababu nilikuwa Mkristo.

Niliyakumbuka maneno ambayo niliyafuatisha kwa mchungaji siku ambayo nilifunga naye ndoa kwa kusema kwamba kwenye dhiki na raha, afya na ugonjwa, utajiri na umasikini ningeendelea kuwa naye, sasa wakati huo ulikuwa ni muda wa matatizo, sikutakiwa kumuacha, nilitakiwa kuendelea naye tu.

Nilipoona mawazo yanaendelea zaidi huku moyo wangu ukiumia, nikachukua simu yangu na kutaka kumpigia, nilitaka kusikia japo sauti yake japokuwa nilijua kwamba niliumia sana.
“Hallow,” niliita mara baada ya kupiga simu.

“Niambie Steven,” nilishtuka sana, sauti iliyosikika haikuwa ya mke wangu, ilikuwa ni sauti ya rafiki yangu, Julius.

Nikaanza kujiuliza, kwa nini nilimpigia simu mke wangu na kupokea mtu mwingine, rafiki yangu Julius, iliniumiza sana moyoni, nikaona kwamba mke wangu hakurudhika kunisaliti kwa Christopher na hivyo aliamua kunisaliti kwa mwanaume mwingine, niliuhisi moyo wangu ukiwaka moto.

“Julius, inakuwaje simu ya mke wangu unapokea wewe?” niliuliza huku nikionekana kupagawa.
“Simu ya mke wako? Kivipi? Mbona hii simu yangu,” aliniambia Julius.

Nilishangaa sana, iweje aseme simu ilikuwa yake na wakati nilikuwa na uhakika kwamba ilikuwa simu ya mke wangu, nilichokifanya ni kuangalia namba, kweli Julias alikuwa sahihi kabisa, nilimpigia simu yeye badala ya mke wangu Juliet.
 
SEHEMU YA 09

“Daah! Samahani sana kaka. Nimechanganya namba,” nilimwambia huku nikianza kujichekelesha.

“Hahaha! Juliet, Julius, tupo karibukaribu sana simuni, usijali kaka,” aliniambia Julius na kukata simu.

Presha yote iliyokuwa imepanda ikashuka, nikashusha pumzi ndefu na kisha kumpigia simu mke wangu, simu ikaanza kuita, iliita kwa sekunde kadhaa na kupokelewa, sauti ya mke wangu ikaanza kusikika simuni.

Nilikuwa na hasira mno, moyo ulijawa na maumivu makubwa lakini mara baada ya kusikia sauti ya Juliet, sikufichi, moyo wangu wote ukabadilika, hasira nilizokuwa nazo zikaanza kuyeyuka mithili ya barafu lililowekwa katika bati lililopigwa sana na na jua.

Nikaanza kusikia burudani moyoni mwangu, sauti yake ikanifariji na kujiona nikipata nguvu mpya ya kumpenda huku upande mwingine wa moyo wangu ukiniambia kwamba kila kitu kilichokuwa kimetokea, hakikuwa kweli bali nilijipa presha ya bure kabisa.

“Mpenzi wangu, my babyto....” aliniita Juliet, majina hayo yakanilegeza zaidi.
“Mpenzi wangu...” na mimi niliita.
“U mzima huko?”

“Nipo poa sana, nimekukumbuka kipenzi.”
“Nimekukumbuka pia.”
“Nataka tutoke usiku, twende sehemu yoyote kupata chakula cha usiku.”

“Waooo!! Asante sana mpenzi, nimefurahi kusikia hivyo, basi naomba uwahi kurudi nyumbani, sawa mpenzi?” aliniambia kwa sauti ndogo iliyojaa mahaba tele.
“Sawa mamiii,” nilimwambia na kukata simu.

Furaha ikaongezeka moyoni mwangu, sikuamini kama kweli mke wangu alikuwa akinipenda namna ile, niliendelea kujipa uhakika kwamba ule usaliti niliokuwa nimeuhisi haukuwa kweli kabisa bali presha yangu ndiyo iliyonifanya nihisi vibaya namna ile.

Siku hiyo, nikarudi nyumbani mapema sana, nikakaa na Juliet huku nikionekana mwenye furaha tele, ilipofika usiku, tukaenda katika Hoteli ya Atriums kwa ajili ya kupata chakula cha usiku, kwetu ilikuwa ni furaha tele.
*
*
*

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 10

Hiyo ilikuwa ni Januari 5. Baada ya hapo, zilipita siku kadhaa huku nikiendelea kuwa katika hali ya furaha na mke wangu, hata kama alikuwa akifanya vitu vya kunisaliti lakini sikuweza kubaini chochote kitu kilichonipelekea kuona kwamba Juliet alikuwa amebadilika kabisa.

Ilipofika Januari 20, mambo yakaanza kubadilika tena.

JANUARI 20.
Nakumbuka siku hii niliamka asubuhi na mapema kwa ajili ya kuelekea kazini. Kiukweli nilichoka kuliendesha gari langu hivyo nilitaka kuendesha gari jingine, nikaamua kulichukua gari la mke wangu bila mwenyewe kujua.

Nilipoondoka, nilikuwa na furaha kubwa isiyo kifani kwani mpaka katika tarehe ya siku hiyo bado nilikuwa napendana na mke wangu na hata mambo ya kunisaliti sikuwa nimeyagundua tena.

Nilipofika kazini, nikaegesha gari na kuanza kujiangalia katika kioo. Kama kawaida yangu, huwa mara nyingi napenda kuonekana ‘smart’ kwa hiyo nilikuwa na jukumu la kuuangalia uso wangu vizuri japokuwa nilifanya hivyo nyumbani.

Wakati nataka kutoka garini, kuna kitu nilihisi, sijui ni nini lakini nilikuwa na msukumo mkubwa sana wa kuangalia kwenye kidroo kidogo mule garini. Macho yangu yakakutana na mfuko mweusi ambao niliufungua na kuangalia ndani.

Sikuamini macho yangu, wakati mwingine nilijiona kama nipo ndotoni, macho yangu yalikuwa yametua katika kiboksi kimoja ambacho baada ya kukifungua, nikakutana na pakti tatu za mipira ya kiume (kondomu).

“Mungu wangu!” nilijikuta nikisema kwa mshtuko mkubwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kana kwamba moyo ulitaka kuchoma.

Mwili ukaninyong’onyea, kijasho chembamba kikaanza kunitoka, miguu yangu nikaihisi ikikosa nguvu kabisa, lipsi zangu zikaanza kuchezacheza, pakti zile zilizokuwa mule , mbili zilikuwa zimetumika zote, pakti nyingine moja ilikuwa na mpira mmoja tu, ilionyesha kwamba mbili zilikuwa zimetumika, kwa ujumla, zaidi ya mipira nane ilikuwa imetumika. Moyo wangu ukapigwa ganzi.
 
SEHEMU YA 11

Kama duniani kulikuwa na watu waliochanganyikiwa, nahisi mimi nilikuwa mmojawapo, kukuta mipira ya kiume katika gari la mke wangu hakika ilinichanganya sana.

Sikuamini hata kidogo, sikuwahi kutumia naye mpira hata siku moja, hii ilimaanisha kwamba mipira ile ilikuwa ni kwa ajili ya mwanaume mwingine.

Kama kuna siku moyo wangu ulikuwa kwenye maumivu makali nadhani siku hiyo ilikuwa ni ya kwanza, niliumia mno na kuna wakati nilijiahidi kwamba ilikuwa ni lazima nimuue mke wangu, aliuumiza moyo wangu mno hivyo sikutakiwa kumuacha.

Nilipoingia ofisini, wafanyakazi wote wakaanza kuniangalia, nilipokuwa na furaha, walikuwa wakijua tu na hata nilipokuwa na huzuni, sikuwa nikijificha. Kwa muonekano wangu tu, nilikuwa mtu mwenye majonzi kupita kawaida.

Usiombe…usiombe ndugu yangu. Kama umempata mtu unampenda sana, muombe Mungu huyo mtu asije kukusaliti, na kama atakusaliti, ajitahidi usijue, ila ukijua, maumivu yake yanakuwa makali kupita kawaida.

Ndivyo ilivyokuwa kwangu mimi. Nilimpenda mno Juliet na hata kile kilichokuwa kikitokea kiliniumiza mno. Nikabaki nikiiangalia pete aliyokuwa amenivalisha siku tuliyooana kanisani, sikuamini kama yule aliyenivalisha pete ile ndiye aliyekuwa akiniumiza kipindi hicho.

“Bosi, upo sawa?” aliniuliza Upendo.
“Nipo sawa,” nilimwambia Upendo.
Upendo alikuwa sekretari wangu wa muda mrefu sana, alikuwa msichana mzuri, mwenye umbo zuri ambaye kwa kumwangalia, ungeweza kuwapongeza wazazi wake kwa kumzaa binti mzuri kama yeye huku ukimuuliza Mungu kwa nini alimpendelea Upendo.

Ofisini hapo, wafanyakazi walikuwa bize wakimfuatilia Upendo lakini hakuwa msichana mwepesi kukubali, wapo waliokuwa wakimletea maua, wakimpigia simu kila siku na pia kulikuwa na wale waliokuwa wakimuomba sana kumtoa mtoko wa chakula lakini Upendo hakuwa akikubaliana nao, alionekana mwanamke mwenye msimamo mkubwa mno.

Siku zikaendelea kwenda mbele, mwisho wa siku Upendo akaanza kunionyeshea ishara zote za kunitaka.

Nilionekana kuwa sijali sana kwa kuwa nilikuwa na mke niliyempenda sana, alijaribu kufanya hili na lile lakini kidume nilikuwa ngangari, sikuweza kuwa naye.
 
SHEMU YA 12

“Ninakupenda sana Steven,” aliniambia kipindi alichokuja ofisini mwangu.
“Samahani Upendo niite bosi,” nilimwambia huku sauti yangu ikitoka kwa kumaanisha sana.

Upendo alinisumbua sana lakini nilikuwa na msiamamo mkali, sikutarajia kumsaliti mke wangu maishani mwangu, na kama ingetokea hivyo isingekuwa kwa mfanyakazi wangu, ambaye anaishi kwa fedha zangu, anabadilisha nguo na kununulia magari kwa fedha zangu.
“Siweza kudate nawe,” nilimwambia Upendo.

Hakukoma, aliendelea kunifuatiia zaidi na zaidi lakini msimamo wangu ulikuwa uleule, sikutaka kudate naye.

Siku hiyo nilipoingia ofisini huku nikiwa na majonzi, kwa kuniangalia tu, aligundua kwamba nyumbani kwangu kilikuwa kimenuka, hivyo aliitaka nafasi hiyo kwa kisingizio cha kunipa furaha.

Nilipokaa kitini, akapiga hodi na kuingia, bado sikuonekana kuwa na furaha kabisa. Akapiga hatua na kusogea kule nilipokuwa, akanishika begani.
“Kuna nini bosi?” aliniuliza.
“Hakuna kitu.”

“Hapana. Haiwezekani. Huwa haupo hivyo. Wifi kakukorofisha nini?” aliniuliza huku akionekana kunionea huruma.
“Kawaida tu Upendo. Naombe ukaendelee na kazi.”

“Bosi, nitaendelea vipi na kazi na wakati upo katika hali hii? Siwezi, nakosa amani moyoni kukuona hauna furaha,” aliniambia kwa sauti yake nyembamba.
“Kaendeleea na kazi Upendo,” nilimwambia, kidogo nikatoa sauti yenye ukali.

Akaonekana kuogopa, akaanza kuondoka ofisini mwangu. Kumkataa Upendo ulihitajika moyo wa chuma, alikuwa msichana anayevutia sana, kwa nyuma alikua amejazia halafu siku hiyo sketi yake aliyokuwa ameivaa iliishia magotini huku kukiwa na mpasuo mdogo wa kizushi, nilipouona upaja wake, matemate yakanitoka na kujilaumu kwa kumuumiza mtoto huyu.

Kuna mambo mengi nilijifunza kwamba inawezekana mtu hataki kuchepuka ila kutokana na maisha yanayomzuka nyumbani, anajikuta akiwa amechepuka.

Toka nimuoe Juliet, sikutarajia kama kuna siku ningekuja kuchepuka nje lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea cha kunisaliti, niliona kwamba huo ndiyo ulikuwa muda pekee wa uchepuka.
“Lakini nina mtoto, nitaweza vipi kuchepuka? Kweli nimuumize Juliet? Haiwekani,” nilijiambia.
 
SEHEMU YA 13

Huo ndiyo ulikuwa mtihani mgumu kwangu, kila siku swali lilikuwa likijirudia kichwani mwangu kwamba ingewezaje kumsaliti mtu kama Juliet? M

wanamke mzuri ambaye nilikuwa naye katika shida na raha, hakika nilijisikia hukumu moyoni.

Siku hiyo kazi hazikufanyika, mara kwa mara Upendo alikuwa akinipigia simu na kunijulia hali, aliendelea kusisitiza kwamba isingewezekana kufanya kazi na wakati nilikuwa katika hali hiyo.

“Kwa nini?”
“Ninakupenda Stev....bosi, ninakuhitaji,” nilimwambia.

“Si unajua kwamba nimeoa?”
“Najua lakini nimejitoa kwa kila kitu.”
“Haiwezekani, siwezi kumsaliti mke wangu,” nilimwambia.

“Huwezi kumsaliti? Unamwamini sana mkeo? Utamuamini vipi mtu asilimia mia moja? Hauoni kama naye anaweza akawa anakusaliti kimyakimya?” aliniuliza, maswali yake yalikuwa na uhalisia juu ya kile kilichokuwa kikitokea.

“Ninamwamini mke wangu, hawezi kunisaliti,” nilimwambia maneno yaliyoufanya moyo wangu kunikosoa.
“Sawa. Ila usitake kumwamini mtu usiyekuwa naye karibu,” aliniambia Upendo na kukata simu.

Nilifika ofisini nikiwa na stress, maneno aliyoniambia Upendo yakaniongezea stress zaidi mpaka kufikia hatua ya kutokuendelea kuwepo ndani ya ofisi hiyo, nikatoka zangu na kuondoka kurudi nyumbani.

Garini, kichwa changu kilikuwa kikifikiria kufanya mauaji tu, haukuwezekana kukubaliana na hali iliyokuwa ikitokea, kulikuwa na mambo mawili ya kufanya. Moja, nimuue mke wangu, pili, au nimuue Christopher.

“Nitawaua wote wawili...lakini haiwezekani, kwa nini nisimuue Christopher?” nilijiuliza, nikapata jibu kwamba ili kuupoza moyo wangu, acha nimuue Christopher kwa sababu alijua fika kwamba Juliet ni mke wangu, kwa nini amfuate na kumtongoza? Kwangu, yeye ndiye alionekana kuwa msaliti.

Nilipofika nyumbani, nikateremka na kuelekea ndani. Chumbani, mke wangu, Juliet hakuwepo. Nilijaribu kumcheki kila sehemu lakini sikuweza kumuona. Kidogo nilishtuka, aliondoka nyumbani na sikuwa nimejua alipoelekea.
 
SEHEMU YA 14

Baada ya kumkosa kila kona, nikaamua kumfuata mlinzi wa getini, Mchichi ambaye toka kitambo nilijua kwamba kuna mengi alikuwa akiyafahamu japokuwa hakutaka kuniambia.

Nililijua hili baada ya siku ile Christopher kuja nyumbani na nilipomuuliza alionekana kubabaikababaika.

“Mchichi, mke wangu yupo wapi?” nilimuuliza huku nikionekana tofauti.
“Alitoka bosi.”
“Amekwenda wapi?”
“Hakuniaga.”

Muda wote Mchichi alikuwa akitetemeka tu, kwa jinsi nilivyoonekana, sikuonekana kuwa na utani hata mara moja, kila nilipokuwa nikiendelea kuongea naye, hasira zilikuwa zikiongezeka zaidi.
“Niambie mke wangu amekwenda wapi.”
“Sijui mkuu,” aliniambia huku akitetemeka.

“Niambie kile unachokijua juu ya mke wangu.”
“Sijui chochote mkuu.”
“Unanitania. Nakwambia unanitania. Sasa subiri.”

Sikutaka kuendelea kubaki mahali hapo, niliondoka kwa hasira na kuelekea ndani huku nikimwacha Mchichi akiwa hajui cha kufanya.

Baada ya dakika kadhaa, nikarudi. Mkononi nilikuwa na bastola yangu, nilikuwa nikitetemeka kwa hasira sana, kijasho chembamba kilikuwa kikinitoka.
 
SEHEMU YA 15 *
*
*
“Si umesema haujui! Sasa utamwambia Mungu kwamba nilikuua kwa kuwa haukutaka kuniambia ukweli,” nilimwambia huku nikiwa na hasira, nikaikoki bastola yangu.

Kiukweli siku hiyo nilibadilika, sikuonekana kuwa na utani hata mara moja, kila nilipokuwa nikimwangalia Mchichi, hasira zilikuwa zikiongezeka. Kwa muoekano wake tu, ilionyesha kwamba kulikuwa na kitu alichokuwa akikifahamu ila hakutaka kuwa muwazi.

“Ninakuua,” nilisema kwa hasira.
“Naomba usiniue, nitakwambia ukweli,” aliniambia Mchichi huku akilia, muda huo alikuwa amepiga magoti chini.
“Niambie nini kinaendelea.”

“Shemeji anatembea na rafiki yako Chistopher.”
“Sawa, ndani hayupo, yupo wapi?”
“Ametoka, amesema kwamba anakwenda kuonana na Christopher.”

“Wapi?”
“Hakuniambia lakini nilisikia akisema Monalisa hoteli.”
“Sawasawa. Nakwenda huko. Nipe simu yako.”

Akanipa simu yake, sikutaka kuridhika, nikaenda ndani na kuchukua simu ya mfanyakazi wa ndani. Nilikuwa na jukumu moja tu kwa wakati huo, kuwaua wote wawili.

Nilikuwa na hasira sana na hakukuwa na mtu wa kunizuia kufanya kile nilichokuwa nikitaka kukifanya.
Nilipoona kwamba simu zao zote nilikuwa nazo, nikachukua gari langu na kuelekea Kinondoni katika Hoteli ya Monalisa.
Bastol yangu ilikuwa pembeni.

Kwa wakati huo, hata gari niliyokuwa nikiiendesha ilionekana kwenda taratibu sana, nilitamani ipae. Sikutumia muda mwingi sana, ndani ya dakika tano nilikuwa nje ya hoteli hiyo.
Nikateremka na kuelekea ndani.
*
*
*
Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom