Ulimwengu wa macho ni mwepesi sana

Ulimwengu wa macho ni mwepesi sana

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,142
Reaction score
859,435
Hesabu za ulimwengu wa macho.. Yaani ulimwengu unaoonekana ni rahisi sana na zinatatulika... Zina miongozo inayoonekana na tafsiri zake sio kinyume... Huu ndio ulimwengu wa ithibati za kisayansi kwamba hiki kiko hivi kwasababu ya hivi.. Kwamba 2+2=4 na sio 22! Elimu ya ulimwengu wa macho na ndio wengi tulojifunza kwa sehemu kubwa na ndio tunayoijua... Lakini elimu hii na ithibati zake zote bila nguvuroho ni mfu.... Nguvuroho ni nishati (energy)
Ndoto zinaingia kwenye kundi la ulimwengu usionekana, ndoto haziko kwenye ulimwengu wa macho labda tu ziwe ndoto za Alinacha zile za kujiotesha mwenyewe kwenye fikra zako
Hakuna ndoto ina tafsiri moja na ndoto moja ikiotwa na watu wawili tofauti bado tafsiri yake itategemea mambo mengi kutokana na historia ya mwotaji... Na ndoto zina makundi yake kuanzia ndoto maono, ndoto kutokana na mawazo maneno na matendo yetu yaliyopita yaliyopo na yajayo... Ndoto kutokana na kazi za wanga na wachawi
Ulimwengu wa roho ndio ulimwengu mgumu, ulio deep na complicated kabisa... Formula na hata matokeo yake huja kinyume na ulimwengu huu hauna ithibati za kisayansi...
Mungu sio kitu kinachoonekana... Mungu hana ithibati za kisayansi, kwakuwa Mungu ni roho na ulimwengu wake ni ulimwengu usioonekana... Matokeo yake ndio hukupa ithibati za uwepo wake... Kuzimu, pepo, jehanum na mbinguni ni dhana za kiroho tunazoweza tu kuziumbia maumbo ya kibinadamu kutokana na utashi na mitazamo ya kibinadamu katika ulimwengu wa macho... Lakini dhana halisi haichoreki ila inahisika!
Mada hii ni maandalizi ya mada ngumu ijayo ya intuitions of the eight senses in the state of spiritual world... Itakuwa ni mada nitakayoandika kwa kiingereza na kiswahili

Stay tuned...!!!
 
Nakuaminia mzee wa ithibati isio na makando.heri ya pasaka sana.mi niko zangu huku kilema sasahivi tunafurahi bila ithibati yoyote
Hahahaaa uniletee mbege isiyochachuka tafadhali
 
sijawah kuzielewa post zako, unakuwa hujui kitu kamili na unabakia kurukiarukia tuu!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]utanielewesha vizur chumban
 
sijawah kuzielewa post zako, unakuwa hujui kitu kamili na unabakia kurukiarukia tuu!
Haya ni maneno ya wakosaji na washindwa... Hivi unajua kwanini kwenye mitihani kuna kufeli? Hivi unajua ni kwanini kwenye mitihani kuna wa kwanza na kuna wa mwisho!? Ni kwa vile tunatofautiana ufahamu.. Na IQ hazifanani kuna IQ za mende panya kiroboto mbu popo simba nknk...
IQ ya nyani haiwezi kufanana na ya dubu... Itakuwa ni makosa makubwa mno kufananisha IQ ya mende na IQ ya binadamu japo kuna binadamu wenye IQ ya mende.....
 
Back
Top Bottom