Ulimwengu wa Bernardo Mukassa katika nyimbo za Kikatoliki (RC) Tanzania

mwita ke mwita

JF-Expert Member
Aug 13, 2010
7,848
3,483
kwa wale wanaopenda kwaya za kikatoliki, Bernad Mukassa si mgeni kwao, yeye ni mwalimu wa kwaya ya Mt. Kizito makuburi, ni mtunzi alijizolea sifa nyingi kwa utunzi wake wa nyimbo. hata ukichukua albam za kwaya nyingi huwezi kukosa wimbo wa Mukasa, licha ya kuwa mtunzi bora ila kwa upande wangu mimi naona MUKASA, na wenzake kama VICTOR MURISHIWA, E.L MKUDE, E.F JISSU, MANOTA na watunzi wengine wanaochipukia wanaanza kuharibu ladha ya muziki wa kikatoliki kwa kuingiza vionjo na free organ za ajabu ajabu, kwa mfano wimbo uitwao KIDOLE JUU ngoma zake zimechukuliwa kutoka kwenye wimbo wa kihindi uitwao GOLOGOLO na nyimbo nyingine nyingi ambazo MKUDE amekuwa akicheza KINANDA amekuwa akiiba free organ za nyimbo za dunia.Nyimbo za watunzi hawa nyingi zimekuwa ni za kasi yaani 6/16, badala ya nyimbo za kutafakarisha ambazo zilikuwa zikitungwa na JOHN MGANDU, DEO KALOLELA, MARCUS MTINGA,A.NGURUMO, J.MAKOYE, SEVERIN SWILLA na wengine ambapo nyimbo nyingi zilikuwa na mwendo wa 4/4, 2/4,3/4 na 3/8. vilevile watunzi hawa wamezidisha nyimbo mpya kila siku kanisani kama inawezekana nyimbo za kuuzia albam zisipigwe kanisani.
tunataka ile ladha ya kikatoliki irejeee
 
Nyimbo bado ni nzuri sana kwa maono yangu kuongezeka kwa vionjo sio tatzo.. Ila suala kuu ningeomba hao watunzi wakongwe kama kina mukasa wangejikita pia kwenye kufundisha vijana elimu ya muziki na utunzi.
 
hakuna kosa lolote wafanyalo bali nyinyi ndio hamlewi mnachokijadili.. Hakika kwa misingi ya kanisa katoliki kupitia baraza la maaskofu wangekuwa wanafanya ndivyo sivyo wangeshapigwa marufuku.

Kuingizwa kwa vionjo vya kiasili ktk nyimbo za kikatoliki na hasa barani africa; suala hilo liliptishwa kwenye mtaguso wa pili wa vatican.. Na baada ya hapo ndipo urasimishaji mkuu wa vionjo vya kiasili ulipopitishwa ili kunogesha zaidi ibada na kuleta mguso kwa kanisa mahalia kwa maelezo zaidi jaribuni ku'google VATICAN II na humo na mtaona maazimio makuu ya kanisa... NA KUMBEKENI KUWA ZILE NYIMBO ZA TARATIBU ZILIZOKUWA ZINATUMIKA HAPO MWANZO NI KUTOKANA TU NA MAPOKEO YA KANISA KWAKUWA WAO NI ULIKUWA NI UTARATIBU WAO WA UIMBAJI.

Na hivyo ndio kusema hao watuzi hawapaswi kulalamikiwa bali kupongezwa.
 
yani mtoa mada umenigusa. huwa namis sana ile rythm ya kiasili ya kikatoliki niendapo kanisani siku hizi. kilichobaki ni aleluya kuu tu ifikapo pasaka. jamani vile vionjo vya asili vina upako wake.
 
by the way catholic composers wanajitahidi, tatizo wengi siku hizi mziki wanausomea kwa kuunga unga mtaani, inabidi kanisa liwe na shuule za muziki
 
.
Njoo usali parokia ya Mavurunza dsm misa ya saa 4 utaburudika na nyimbo za tradition catholic

nashukuru ndugu yangu nitasali huko siku moja. i really miss that...hiyo atmosphere huwa inanipeleka straight mbinguni. niko dar lakini naomba nijulishe mavurunza ni maeneo gani hasa.. nitashukuru kwa taarifa.
 
Huyu Mukasa ni kiwango kingine aisee.
Nina kitabu cha mkusanyiko wa nyimbo za Catholic, yaani ukiipita moja mbili zinazofuata ni Mukasa. Jamaa anatisha, na ndo anaipaisha Parokia ya Makuburi.

Ila kwa kuimba kuna parokia moja huko Arusha nadhani ni Mt. Theresia. Hawa ni balaa, japo siku hizi siwasikii sana.
 
rythm ya nyimbo za kikabila zipoje ndugu yangu, ukielewa hilo ndo utajua hawa jamaa wanafanya nini na nini kinachotakiwa kutokana na ule mtaguso wa pili wa vatican. style za ngoma, speed na free organ na hata melody zao hawa jamaa zimejikita zaidi huko kwa hiyo me sioni kosa kwao, ila nawapongeza kwa kurudisha tamaduni zetu kanisani. labd kama haupo aware na nyimbo za makabila....
 
kuna ile albam ya Ikulu ya mbingu wameimba Kwaya ya mtakatifu Cecilia Merelani Arusha inaboa video zake maana wananengua kama sebene. Mtoa uko right sana
 
wapo watunz weng wazur wa muzik wenye mahadhi ya kiibada km Saasita,David Wasonga,Edger Mwembe et al dah! muzik wa kwaya mtamu sana
 
Back
Top Bottom