Ulimwengu katumwa na Kikwete. DK. Slaa alishajifunza sana miaka kingi iliyopita. Kwanza, ninyi mnaotaka kumpa heshima huyu kibaka mnaitoa wapi? Unajua huyu akiwa mkuu wa wilaya ndiye aliyezuia mkutano wa kwanza wa mageuzi, hadi pale wanaharakati kama Mabere Marando, Ndimara Tegambage, Anthony Komu walipojitokeza na kupinmga udhalimu wake?
Wanaharakati hao waliandika waraka kwenda nchi za Magharibu na nakumbuka rais wa wakati huo, Ali Hassani Mwinyi aliruhusu wanamageuzi kukutana alipokuwa uwanja wa ndege wa Dar es Salaam akienda ulaya kuomba misaaada baada ya kubanwa na wafadhiri. Sasa huyu Ulimwengu analipi la kujivunia.
Pili, Ulimwengu alikuwa mwenyekiti wa kampuni kubwa - Habari Copr - ikamshinda na badala yake akaiuza kwa fisadi Rostam. Sasa mtu aliyeshimdwa kuongoza watu 200 atawezaje kumshauri rais ajaye?
Anachotaka kukionyesha Ulimwengu hapa ni kwamba Slaa hajakomaa kwa urais hivyo ajifunze. Hili si kweli. CV ya Slaa ni kubwa kuliko yeye na kimsingi Slaa amekuwa kiongozi mkubwa wa madhehebu ya dini, mbumge na katbu mkuu.
Ulimwengu aondoke na pumba zake arudishe jibu kwa Kikkwete - Hatudanganyiki. Angekuwa mrtu wa maana Mkapa asingemvua uraia.