Ulimpataje umpendae?

Bado sijabahatika kukutana na ubavu wangu. Naamini ipo siku wakati wa Mungu ni wakati mzuri sana. Hawai wala achelewi.
Bwana wa Majeshi,Mufalme wa Amani hakika ni Muweza wa yote!

Sasa na uamini wakati utayari na neno limetimia,
Karibu Kwangu MPENDWA.
 
Wa kwangu ni kicheko lakini nashukuru Mungu mpaka leo niko naye na sijawahi kuona kasoro zake. Nilipanda daradara asubuhi nikiwa tu nasogeza masaa sikuwa na muelekeo. Baada ya kilomita kama 2 nikamuona anapiga mkono kusimamisha gari. Kabla hajaingia mapigo ya moyo yakanienda mbio bila kutarajia. Lakini nikawa najisikia kumsemesha. Ndo ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona. Bahati nzuri tulishuka kituo kimoja. Konda akakosa change anirudishie huku naona yeye huyoooo anatembea. Nikasema simuachi bora niache hela. Nikamfata kwa nyuma na kumpiga picha. Kumuongelesha nikawa naogopa. Nikaamuwa tu nimfate mpaka nione wapi ataishia na nani ataongea nae ndo nipitie kwake. Mungu si Athumani bhana! Nikamuona mama mmoja mfanya usafi mazingira ya kazini kwao wakasalimiana na kujadili mawili matatu. Nikasema hapa umeisha. Jioni nikampigia simu mjomba wangu tuko sawa kiumri. Nikamueleza. Hapo hapo nikarusha picha whatsapp akamuone. Kumbe anamfahamu ! Akanipa na number yake nikamuona whatsapp ndo nikaanza na kumsoundisha. Mpaka leo hii niko nae,najiulizaga kwa mini sikumpata mapema! Na mwezi wa pili mwaka kesho ubwabwa tutakula na washikaji
 
Binafsi niseme na kuanza kumshukuru Mungu kwa mke nilie nae mke bora na mama wa watoto wangu chipunga, helo na chipoku ukweli siku ya kwanza kumuona aliuchanganya sana moyo wangu mpaka kiasi kwamba nikasahau jinsia yangu kama ni mwanamke au mwanaume wakati nashangaa uumbaji wa manani ungeniita hadija ningeitika ungeniita juma ningeitika alikua kajaaliwa kwa kila kitu sura mpaka umbile nikaona isiwe tabu kwa kipindi kile nilikuwa rijali mwenye miaka 24.


Nilikua na ushawishi wa kila namna kwa mwanamke najua kuvaa vizuri na gari nzuri kifupi maisha yalikua mazuri bila kuchelewa ni katoa business card yangu na kumpa ikakataliwa duh kidume jasho likanitoka nikasema poa hakuna shida kwakuwa hakua anatokea mbali sana na kijiwe changu nikatafuta mtu wa karibu na kuhakikisha nakua karibu nae hatimae nikafanikiwa kumshawishi na kuwa nae karibu niseme tu ukweli.

Pamoja na uzuri wake wote sikuwa na mpango wa kumuoa sikuwa na muda wakati huo wa kuoa wala wazo nilimshawishi kwa muda wa mwaka mzima pasipo hata kuonja papuchi japo alikua anakuja kwangu kama kawaida mwisho nikajifikiria hivi kwa umri huu mwanamke wa kuoa si ndio huyu nahangaikia nini na dunia nimetumia ushawishi wangu wote na vizawadi nini lakini wapi mwisho nikaamua kutangaza ndoa na sasa tuna miaka 8 na watoto wawili asante Mungu.
Hongera sana kwakuopoa kitu cha kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom