Nina mwanangu alihama home kibishi akaenda kupanga baada ya miezi Sita hivi geto likawa limeshakaa Poa. Oneday ilikua weekend akaenda club kujirusha alivyorudi night wakora wamevunja wakabeba kila kitu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Jamaa akaona isiwe tabu akarudi home. Haikupita hata wiki moja ankow akaja kuwatembelea na kumkuta jamaa home akamuuliza vip? Umekuja kusalimia akajibu hapana nimeibiwa. Anko Akamcheka sana akamwambia mwanaume akiamua kuanza maisha harudi tena home.
Mshkaji akaondoka akarudi getto kwake akatandoka mabox maisha yakaendelea.
Inaitwa get it how you live.ebuana tangu nimezaliwa mimi nilikuwa naishi na mama angu pa1 na wadogo zangu, katikati ya mwaka 2015 nikiwa form four mama aliamua kwenda dar es laam kujichanga kimaisha, akaniacha mimi na wadogo zangu kama watatu, baada ya mwezi akaagizia mtu amuijie yule mdogo kuliko wote(wakati wote huo alikuwa anagharamia pesa za matumizi na kodi ya pango, na Mimi nikiwa bado nipo maskul).
Sasa baada ya kumaliza shule kimbembe ndipo kilipo anza, kwanza kodi ikaanza kusumbua kwa mother, pia hela ya mahemezi nayo ikawa taaabu kweli kweli. mara mama atume buku10 kwa juma zima ikafkia hatua madogo wote wakatoweka home. Mwingine alienda kwa rafki yake mama na mwingine akawa kaenda kwa ndugu zetu nikawa nimebaki peke angu
Nikatafakari maybe niangalie upande wa pili yaani kwa mshua(yupo dar miaka mingi ila yeye ana maisha yake na mama ana harakati zake) ambaye kiuharisia sijakuwa naye wala sijawahi kukaa nae hata siku nzima ikapita, nikamwambia anisaidie walau pesa ya mtaji hata laki1 iweze nisaidia kupata chanzo (wakati huo mama ana kama miezi miwili hatumi pesa ya kodi wala ya magenta). Mara baada ya baba kumuomba pesa alichonijibu sikuwahi kutarajia kujibiwa, aliniambia kuwa "MTAJI WAKO WA KWANZA NI JAMII INAYOKUZUNGUKA" sikuwa na jinsi ilinibidi nikubaliane na matokeo..
Baada ya mda flan iv mama alituma elfu40 pekee akadai nihamie sehem nyingine maana mwenye nyumba alikuwa keshakuwa mbogo.. pia niangalie nyumba yenye bei poa kwa kuwa nimebaki peke angu afadhari nichukue walau single isiyo na umeme ili inisadie kupunguza gharama ya kodi nikalipia hela ya miezi miwili(ila kipindi nahama baba mwenye nyumba ninapo hama alikaba baadhi ya vitu ila nilikuja kuvikomboa baadae, baada ya kupata pesa yake).
Namshukuru mungu baada ya muda kweli ushauri ule wa baba ambao niliuona wa kipuuzi niliutumia kuifanya jamii yangu kuwa mtaji, niliajiliwa kuuza DVD mtaani(yaani kama nikiuza elf2 ya boss ni buku na yangu buku, hata nkiuza zaidi ya elfu mbili ya boss ni buku tu kwa kila DVD) kama mwez kama wa 10, 2016 wadogo zangu walimfuata mama. nikawa nimebaki peke angu..
Kiukweli biashara ilinilipa sana maana kwa siku niliweza kutunza faida ya hadi elf 3o nikawa nanunua mifugo mbuzi&ng'ombe napeleka kwa babu kijijini, nikaanza kujipanga maana vitu vyote vya ndani nilimtumia mama, na mm nikaanza maisha yangu hadi sasa najitegemea na mama anaomba msaada wowote kutoka kwangu..
2017 nilibadili biashara na kuwa mqchinga nilipambana sana na mwanzoninmwa mwaka jana nikaamua kuwa wakala wa mitandao ya kipesa hadi hivi leo nimejiajiri mwenyewe kama wakala.. kiukweli mimi kama mimi hakuna hata sumuni ya mtu nilioipata kutoka kwa mtu yeyote zaidi ya juhudi zangu na nia yangu ya kuishi kwa imani kuwa naweza.
Wito:mwanzoni nilijua kauli ya baba ilikuwa ni ya kunivunja moyo, lkn hadi hivi leo naishi nikiamini siku moja nimuaminishe baba kuwa niliishi kwa kutegemea jamii inayonizunguka ndio maana nimefka hapa nilipo, kila kijana ana kila sababu ya kutokukaa nyumbani kwa kigezo cha kutokuwa na pa kuanzia..
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu una experiance ya geto kitambo kumbeMi nlianza Maisha ya ghetto tangu nipo form 1 hadi sasa nakomaa ghetto nikipata hela nijenge mjengo nisepe Maisha ya ghetto, ila hakuna kitu kizuri kama kuishi kwenye chumba chako unachokilipia kodi ,yani unaishi unavyotaka
Sent using Jamii Forums mobile app
Dah mim nlpata kazi wilaya furanii.ikabidi nlilipoti ujio wangu siku tatu mbele
bwana bwana!! Nfukoni nlikua na elf90 niliyopata kwnye ufundi redio wangu
nkatumia elf tano kama nauli
then kama elf kum hiv kununua vijimahtaj kidogo
basi nkalipoti hilo eneo lakaz kwakufkia nyumba ya wageni,uzuri wa hapa bwana vyumba sio tabu
dah kesho yake nkapambana kutaftata had nikakipata
bas nkanunua zangu mkeka......
mwanaume nkahamia magetoni....
Nakumbuka ule usiku ulikua mrefu kwangu .kunawadudu wanaitwa sungu sungu walipigiana simu aise nadhani waliambiana ...oy mazee uko nje mje kunapilau hapa ndaniiii muwai.....
ila MUNGU MKUBWA leo nnamiezi kama mi 4'ukizama geto unaeza usitoke mziki kama woootee
Voxser empire
Hii thread ina mizuka sana...uyo bro muhesabie siku tu..atafrahi..Hii siredi inanipa hamasa kubwa mno, mimi kwasasa sipo kwa wazazi maana wazazi wako pande za Bujumbura na mimi niko pande za papa misifa(Kinshasa DRCongo) na nna mwaka mmoja tangu nidondoke pande hizi nina job japo hailipi sana ki vile ila bado nnaisha na brother.
Nnapanga kumtoka bro na haifiki october maana kama brother hanipi freedom lote tayari maandalizi ya vitu vya ndani nimesha yaanza nina godoro langu, feni na vingine vidogo vyakuanza ghetto life ila kila nikisoma comments nnatamani ata nipasuwe kesho yani
#Proud_to_be_a_domo_ZEGE
Sent using Jamii Forums mobile app
Big up kwa huyo mwamba wako, mwanaume harudishi nyuma majeshi kizembeNina mwanangu alihama home kibishi akaenda kupanga baada ya miezi Sita hivi geto likawa limeshakaa Poa. Oneday ilikua weekend akaenda club kujirusha alivyorudi night wakora wamevunja wakabeba kila kitu🤣🤣🤣
Jamaa akaona isiwe tabu akarudi home. Haikupita hata wiki moja ankow akaja kuwatembelea na kumkuta jamaa home akamuuliza vip? Umekuja kusalimia akajibu hapana nimeibiwa. Anko Akamcheka sana akamwambia mwanaume akiamua kuanza maisha harudi tena home.
Mshkaji akaondoka akarudi getto kwake akatandoka mabox maisha yakaendelea.
Bro nampa kamba ndefu, kuna siku ataamka sipoHii thread ina mizuka sana...uyo bro muhesabie siku tu..atafrahi..
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha hapana mkuuBigup sana bro...sema hyo kupenda watoto wa watu angalia usje kula.mama zao[emoji3]
Sent from my SM-G920P using Tapatalk
Mkuu hapa ni gheton kwangu yaani kukuazima siku moja umeshakuja kuosha Jf. ! Natania mzeeWakuu mambo vipi,,Leo naomba tufanye kushare kila mtu jinsi alivyo chomoka Nyumbani kwao..Hii itatoa hamasa kwa wale waliokua nyumbani na kuogopa kuhama na kuanza kujitegemea.
Janga hili linawakumba wana vyuo wengi,unakuta mtu anamalza chuo akiwa labda ana 25 then anarud nyumbani ,mbaya zaid anasubir kazi..alaf kazi zenyew haijulkani utapata lini.
Hii inapelekea wana wengi kua na fear ya kuchomoka home...Kiukwel hali ya kukaa hom inakata sana..Mzee unakuta anachomoka anakuachia mikazi flani hivi howcome.
Ukija upande wa MMU ndio mambo yanakua sio mambo...mtoto anataka aje kukusalmia unaona soo kwasababu upo nyumbani..inakata sana hii
Tukija kwenye maisha ya kujituma tu..sometime unakosa hamasa ya kupambana kwasababu ugali wa bure,unalala bure,kila kitu bure..hii inakua ngumu kuwaza kwa mapana ili kuanza kukamilisha dream zako..
Pia inakata sana..pale wanao unakuta wapo na mageto yao..lakin wewe kwako ni tofauti.
Sasa naomba kila mmoja aseme alichomokaje home na kuanza kukomaa na maisha..Achilia changamoto zake kikubwa hapa ni kusepa kwa maza..
##Mimi binafsi geto nilianza kukaa soon nilivyoingia chuo,,,nakumbuka nilipata room ya elf 50 nikaanza nayo kibish,nikanunua bed ya 150, 5 kwa 6,nikatafuta feni tu ya elf 35..si unajua joto la dar..nikaingia k.koo nikavuta subwoofer ya elf 75 tu...geto bila mziki sio geto ni choo,kujichek mfukoni boom likawa lishakata...basi nikaendelea kuishi geto hadi namalza chuo geto likawa limesheheni tu...
sasa baada ya kumalza chuo. Ndio nikarudi hom..ujinga niliofanya ni kurud hom na baadhi ya vitu niliviuza...Kasheshe ndio ipo saiz..wakuu hom akili inalala,,vibe yote hakuna ,hapa ndio najichanga nichomoke tena nirud geto nianze kupambana..hop ndan ya huu mwaka nitakua nishasepa hom kwa mara nyingine.
Sasa share kitu basi nawewe..
#Nini lilikusukuma usepe home?
#Kitu gani kilikupa mzuka wa kuanza kukaa geto?
#Vipi ulianza kukaa geto ukiwa na kazi au kibishi tu?
#Maisha yalkuaje since day one?
#Je ulienjoy uamuzi wako wa kusepa home?
#ulianza kununa vitu gani vya msingi na kuanza kuishi geto
#Una lipi la kuwaambia wana walioko home hadi leo wakiogopa kukaa geto kisa hawana ajira bado?
Karibuni wakuu..
View attachment 878774
Usikubali mkuu huko ni kujishushia heshima unapokaaGetho tamu sana,yaan baby anakuja ijumaa jioni anaondoka jpili jioni na gharama nazotumia n chache tu,nikinunua nusu ya nyama na tambi au mchele kilo moja na nusu we eat the whole weekend.... Home sirudi zaid ya kusalimia tu...
Taabu n kwa washkaj wanaoomba nao walete mademu zao getho kwangu ,yaan mashuka nifue mm half mchafue nyie jmn hii siikubali....tafuta getho naww.....
Kama una getho mwanangu onesha funguo
Hahah mkuu we ukiona geto kali tu unasema lako [emoji3]Mkuu hapa ni gheton kwangu yaani kukuazima siku moja umeshakuja kuosha Jf. ! Natania mzee
Mimi nilianza kujinunulia vitu vya ndani nikiwa form 3 nilijibana sana nakumbuka nilikua nina sutuali mbili na flana 3 na shati 1 pesa yote niliyokuwa napewa na brother zangu na mshua niliibana ninunue vitu vya ndani,,,
Nilipoanza chuo ndo nikaenda kupanga huku nikiwa full kwa 90% mpaka leo,,sikuwa na kazi lakini nilijiban na kupiga ishu ndogo ndogo kwahiyo vijana wenzangu msiogope kutoka home ikiwa una uwezo wa kupata hata buku 5 kwa siku.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa mkuuHahah mkuu we ukiona geto kali tu unasema lako [emoji3]
Sema ww ulianza ona mbali,kama tangu form 3 ulishaanza mipango
Ushaur wako mzur kaka,wana tuache uoga as long mtu unaeza pata buku 5 bas maisha ya geto tunayaweza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ila kuna baadhi ya vijana wenzangu wao hufurahia kuwa na gheto kwa ajili ya kufanya tu umalaya badala ya kufikiria kuwa ni hatua ya kwanza ya maisha yake aitumie nafsi aliyoipata kusogea mbele,,mwisho wa siku anaishia kuzalisha wanawake hovyo anakuja kuoa mwanamke asiyekuwa na matarajio nae wanazaa watoto wakiwa chumba kimoja kipato chake hakijakuwa umaskini tayari maana inakuwa too late
Sent using Jamii Forums mobile app