GE2025 Ulega: Ni Samia pekee anayeweza kuleta Katiba mpya

GE2025 Ulega: Ni Samia pekee anayeweza kuleta Katiba mpya

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Waziri wa Ujenzi na mgombea ubunge wa Jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega amesema kuwa Watanzania wanapaswa kumchagua Samia Suluhu Hassan kama kiongozi wao wa Taifa ili kufanikisha ndoto ya kupata Katiba mpya.

Akizungumza leo Jumamosi Septemba 6, 2025 kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge katika viwanja vya Kongowe, Ulega amesema Ilani ya CCM ya mwaka 2025 - 2030 inaahidi kufufua mchakato wa Katiba ya Tanzania, na Samia ndiye kiongozi pekee aliye na historia, maono na uwezo wa kuleta mabadiliko hayo.

“Watanzania wenzangu, uchaguzi huu ni fursa ya kihistoria. Huu ni wakati wetu kuchagua mgombea urais ambaye anaweza kutuachia zawadi isiyosahaulika ya Katiba mpya ya Tanzania,” amesema.

Ameeleza kuwa historia ya kisiasa ya Samia inamuonyesha kama mwanasiasa aliyechaguliwa kushirikiana kwenye kamati ya maridhiano iliyofanikisha mwafaka wa kisiasa wa Zanzibar, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, na kuanzisha falsafa ya 4R, ambayo mojawapo ya misingi yake ni ujenzi wa maridhiano ya kitaifa.


 
Waziri wa Ujenzi na mgombea ubunge wa Jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega amesema kuwa Watanzania wanapaswa kumchagua Samia Suluhu Hassan kama kiongozi wao wa Taifa ili kufanikisha ndoto ya kupata Katiba mpya.

Akizungumza leo Jumamosi Septemba 6, 2025 kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge katika viwanja vya Kongowe, Ulega amesema Ilani ya CCM ya mwaka 2025 - 2030 inaahidi kufufua mchakato wa Katiba ya Tanzania, na Samia ndiye kiongozi pekee aliye na historia, maono na uwezo wa kuleta mabadiliko hayo.

“Watanzania wenzangu, uchaguzi huu ni fursa ya kihistoria. Huu ni wakati wetu kuchagua mgombea urais ambaye anaweza kutuachia zawadi isiyosahaulika ya Katiba mpya ya Tanzania,” amesema.

Ameeleza kuwa historia ya kisiasa ya Samia inamuonyesha kama mwanasiasa aliyechaguliwa kushirikiana kwenye kamati ya maridhiano iliyofanikisha mwafaka wa kisiasa wa Zanzibar, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, na kuanzisha falsafa ya 4R, ambayo mojawapo ya misingi yake ni ujenzi wa maridhiano ya kitaifa.

Nonsense!
 
Samia mwenyewe mwenye rangi mbili
IMG_2506.jpeg
 
Maxence Melo and your team,nyuzi kama hizi zifuteni. Yan platform inayopigwa vita ndio hawa wapuuzi wanaitumia kueneza propaganda zao kumbe kwa namna nyingine hili jukwaa ni muhimu ila tu wameziba masikio

Rai yangu kwako usiwe mlainilaini agiza mods wafute nyuzi kama hizi hata kama humu ni "where we dare to talk openly".Nasubiri unipm uniambie kama unatekeleza hili

Dawa ya moto ni moto
 
Back
Top Bottom