Ukweli wangu umeniponza, najuta

Ukweli wangu umeniponza, najuta

vitu kama hivi jamani tuwe tunamuweka Mwenyezi MUNGU mbele kwanza..

kijana nenda katubu, mwambie na mkeo, ongozaneni kanisani mkaombewe..
 
Aisee! Mdomo unaponza kaka..... Hebu ichunguze kolomeo yako kuna sehem pana nundu hyo anayo mwanaume tu na sio mwanamke.... Hapo ndio siri za mwanaume zpo. Meza mdeki mtoto wa kiume sio unakatikiwa kiuno vizur unaanza kuropoka.
hahhaah!! Mwenzio ana jutia alio ya fanya ndio akaona amweleze mwenzie hajakamatwa wala nini,wengine wanakamwatwa na wanakua wakali wao na kesi inahamia kwako, sasa mwambie ivi umefanya vizuri ila angekwenda kupima afya yake kwanza halaf akamchukua mwenzie na akatafuta zawadi nzuri sana akampa mkewe na akazidisha mapenzi kama ametubu kweli lakini kakurupuka tuu hata tena mimi pia ninge chukia....
 
Nazingatia ushauri wenu wadau. Lakini sasa ina maana na mimi niendelee kukaa kimya nisimsemeshe ili nisimvuruge zaidi au...
 
Chanzo cha maOngezi yenu ilikua ni nini? Isije ikawa alikufumania ndo ukaamua kutubu
 
Kuku kala mchele mchana, usiku umefika ni zamu yake kuliwa na wali.

Sosi: Dr Preta

ImageUploadedByJamiiForums1394963635.071981.jpg

Kama hiyo???
 
Last edited by a moderator:
Safiri angalau wiki mbili, ukirudi asira zitakuwa zimekwisha, kumbuka kurudi na vijizawadi. Siku nyingine jaribu kutofautisha siri za kuingia nazo kaburini na siri za kuziacha hapa Duniani.
 
Ni vema kuacha michepuko na kurudi njia kuu,ila ungerudi kimya kimya yasingekukuta Haya!
Ujifunze kuwa na kaba ya ulimi.
Kwa sasa kuwa mpole tu huku usubiri hatma.
 
We nae, sa kilichokufanya uropoke ndio nini. Kumbuka mtu asiyemdanganya mke wake basi hajali kabisa hisia zake. Yaani mwenyewe ukafikiria ukaona kabisa uanze kuropoka??!!!!
 
Ukome,why did u have to say that..hujui mtu asilolijua halimuumizi??but look now she knows...what a pain,kuwaza umpendae akinaniliu na mtu mwingine..
 
Mkuu ingekuwa ni mkeo kakuambia ameshatumia kiuno chake kama msingi hapa mjini bila kupata faida ungejisikiaje? Ulimi umeponza kichwa. Jitahidi siku nyingine ya Msondo umwachie Ngurumo.
 
Takriban wiki moja imepita tangu nilipofanya mazungumzo na mke wangu, nilidiriki kumweleza ukweli kuwa kwa kipindi kirefu nilikuwa natoka nje ya ndoa, na hivyo nikamwomba anisamehe na kuwa najutia nakumwahidi kuwa sintofanya hivyo tena kwani hakuna nilichokipata. Baada ya mazungumzo yetu alionyesha kuniunga mkono kwa kunionyesha upendo wa dhati na mimi pia hali kadhalika. Sasa kilichonichanganya namwona mke wangu kanichenjia hataki kuongea na mimi kila kitu anatuma mtoto, nimwulizapo kulikoni? kimya sijibiwi, kibaya zaidi hataki nimguse ukizingatia kuwa wanandoa ndiyo huwa njia yetu pekee ya kutatua na kuondoa tofauti zilizopo, hakuna amani Nifanye nini sasa wadau?

Njoo nikuazime mgegedo wangu afu kila ikifika usiku unavua shati unakuwa kama hapo kwenye avatar yangu lazima atakuongelesha tu hata kwa vitendo
 
Dhambi zinaungamwa kwa Mungu, sio kwa binadamu...
 
hahhaah!! Mwenzio ana jutia alio ya fanya ndio akaona amweleze mwenzie hajakamatwa wala nini,wengine wanakamwatwa na wanakua wakali wao na kesi inahamia kwako, sasa mwambie ivi umefanya vizuri ila angekwenda kupima afya yake kwanza halaf akamchukua mwenzie na akatafuta zawadi nzuri sana akampa mkewe na akazidisha mapenzi kama ametubu kweli lakini kakurupuka tuu hata tena mimi pia ninge chukia....

sio ndio namshangaa aliropoka mwenyewe tena sasahv anaanza kutulilia sisi ili tufanyeje??. Wakat mm niliwahi wrong msg nilikuwa namtumia nyumba ndogo na ikaenda kwa mamaa ikabidi niwe mkali kama mbogo alipoanza kunihoji na akawa mpole mtoto wa watu mpaka nikamwonea huruma. Wakat kosa ni langu sasa huyu jamaa sijui yukoje?
 
Kuna siri nyingine mtu hupaswa kuzikwa nazo kaburini, for good.

Heaven on Earth hebu ukuje umtafsirie kwa KiQueen Elizabeth
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom