Wateule
JF-Expert Member
- Sep 17, 2010
- 390
- 368
Makonda" kwa madaraka yake kama mkuu wa mkoa (cheo kilichopitwa na wakati na ambacho tumekikataa kwa mujibu wa Tume ya Warioba) ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama. Kama hivyo ndivyo basi, kesi na tuhuma zake ni kesi dhidi ya jeshi la polisi (na video za CCTV zinaonyesha pia alivamia Clouds na polisi). Kwa maana hiyo, polisi kama watuhumiwa (wao na boss wao Makonda) hawawezi kujichunguza na kujifungulia mashtaka wenyewe.
Uchunguzi ulitakiwa ufanywe na tume huru, muelekeo ambao Nape alianza kuuchua kabla ya kufukuzwa na mkuu.
Tume hiyo ndio ingeendelea na mchakato wa kesi mpaka tuhuma zifikishwe mahakamani na kuamuliwa. Lakini, kwakuwa "Makonda" na anayemlinda wanajifanya wapo juu ya sheria, hakuna kilichofanyika mpaka sasa. Na polisi (wakiongozwa na Sirro) wanaogopa kufanywa kamaalivyofanywa Nape.
Uchunguzi ulitakiwa ufanywe na tume huru, muelekeo ambao Nape alianza kuuchua kabla ya kufukuzwa na mkuu.
Tume hiyo ndio ingeendelea na mchakato wa kesi mpaka tuhuma zifikishwe mahakamani na kuamuliwa. Lakini, kwakuwa "Makonda" na anayemlinda wanajifanya wapo juu ya sheria, hakuna kilichofanyika mpaka sasa. Na polisi (wakiongozwa na Sirro) wanaogopa kufanywa kamaalivyofanywa Nape.