Ukweli unao paswa kuujua kuhusu inverter

Ukweli unao paswa kuujua kuhusu inverter

Transistor

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
1,061
Reaction score
1,640
INVERTER NI NINI?
Inverter ni kifaa kinacho badili umeme mdogo wa Direct Current (DC) kuwa Alternative Current(AC) na kuukuza ili uweze kkutumika kwa matumizi ya vifaa vikubwa vya nyumbani kama vile TV, Fridge etc .

Ikumbukwe kuwa Inveter zinatumia umeme wa battery,ambao ndio hukuza kwa matumizi husika.Kutokana na ukweli huo wengi hupenda kujiuliza maswali yafuatayo.

BATTERY ITAISHA BAADA YA MUDA GANI?

Swali kama hili haliwezi kujibiwa bila kujua mambo makubwa mawili ambayo ni

*Ukubwa wa bank yako ya kuhifadhi umeme (Battery)
*Ukubwa wa mzigo utakao fungwa kuchukua umeme katika benki hiyo(Load)
Kutokana na ukweli huu mimi nadhani swali hapa linatakiwa kuwa hivi "NI MUDA GANI NATAKA BATTERY YANGU IFANYE KAZI?"
Hii inamaanisha kuwa muda wa battery kufanya kazi ni maamuzi ya mtumiaji na sio inverter au battery yenyewe.
Hivyo kutokana na ukweli huo the following calculation can be done to determine "how long your battery will run"

Kanuni za kutambua muda wa kutumika kwa battery
1.Tambua ukubwa wa battery yako katika kuhifadhi umeme hii huandikwa katika battery yenyewe katika mfumo wa AMPERE HOUR (A.H)
Mfano battery imeandikwa 100 A.H hii inamaanisha kuwa kuwa kama mzigo uliofunga katika battery hii unachukua ampere 1 basi battery hii itakuwa na uwezo wa kutumika kwa moda wa masaa 100! Au kama mzigo uliofunga unachukua Miliampere
500(0.5 ampere) basi battery hii itakuwa na uwezo wa kutumika kwa masaa 200!Au kama mzigo uliofunga unachukua 5Ampere basi battery hiyo itatumika kwa masaa 20 tu!

Je inakuaje kama mzigoulio ufunga una chukua ampere 100?battery hiyoitatumika kwa muda wa saa moja tu!

Bila shaka utakubaliana nami kuwa ukubwa wa mzigo unaoendeshwa na battery husika ndio unao determine nimuda gain battery yako itatumika.

Hii inaweza kujulikana kwa kutumia formula hizi

(i) Tafuta Ampere inayo nyonywa kutoka katika battery
[TABLE="class: MsoTableGrid, width: 459, align: left"]
[TR]
[TD="width: 613, bgcolor: transparent"] Ampere inayonyonywa = Load(In Watts) ÷ 10(for 12v battery )or by 20 (for 24v battery)
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Mfano:-
Pasi ya Watt 1000 imefungwa katika inverter ambayo hiyoinveter inachukua umeme wake kutoka katika battery ya Volt 12 yenye ukubwa wa 150 A.H

[TABLE="class: MsoTableGrid, align: left"]
[TR]
[TD] Ampere inayonyonywa = 1000 ÷ 10 = 100 Ampere
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



(ii)Tambua muda ambao battery yako itatumika kutokana na mzigo unao endesha


Time
[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] Time = Battery Capacity(A.H) ÷ Ampere
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] Time = 150 A.H ÷ 100 Ampere = 1.5Hour
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Hivyo mtumiaji wa pasi hiyo ataweza kuitumia pasi yake kwa muda wa saa moja na nusu tu kabla battery haijaisha!


NOTE:-Inverter zinatumia battery na battery hizi zina kanuni na sheria zinazo zilinda ili kudumisha ubora wake kwa muda mrefu.Matumizi yasio fata utaratibu hufupisha maisha ya battery na kuifanya
itumike kwa muda mfupi kabla haijaisha ubora wake.Na ikumbukwe kuwa battery ikisha haribika haifai kwa matumizi tena!Kwani inakuwa imepoteza ubora wake.
Mfano unachaji battery inakuwa full kabisa arafu ukitumia kidogo tu inakwisha bila proportion ya utaratibu rasmi wa formula hiyo hapo juu.Na kama battery ikifikia hatua hii you have to replace it!


NINI CHA KUZINGATIA?
Fundi anaye kutengenezea inverter ahakikishe anatengeneza inverter yenye efficiency isiyo pungua 70% kwa Sealed Lead Acid,Nickle-Cadmium,Lithium-Lon Batteries etc.
Hii inamaanisha kuwa battery yako itatumika kwa asilimia70% baada ya hapo inverter yako inatakiwa iache kuendelea kunyonya umeme kutoka katika battery hiyo!Kwa kifupi battery haitakiwi kuisha zaidi ya hapo ili iwe na maisha marefu.
Inverter nyingi za dukani tayari huwa zimewekewa circuit ya kulinda battery inverter za namna hii huandikwa kabisa katika label yake utakuta imeandikwa efficiency 80% au 70% au 90% etc.

Faida ya kuzingatia kigezo hiki ni kwamba battery yako itatumika muda mrefu bila
kupoteza ubora wake.

Hasara ya kuzingatia kigezo hiki ni kwamba battery yako itatumika kwa muda mfupi kuwasha vifaa vyako ambapo utakuwa na uwezo wa kutumia asilimia 30% to ya nguvu ya battery yako na ile 70% itabakia kulinda ubora wa battery!


Mfano (i)
Inverter inayo endesha mzigo wa watt 500 imefungwa katika battery ya 12v yenye 150 A.H.Je inverter hiyo itafanya kazi kwa muda gani kama kigezo cha efficiency kisipo zingatiwa?
Solution

Ampere= Power ÷ Dc voltage therefore 500w ÷ 10v =50 Ampere


Time=Battery capacity ÷ Ampere therefore 150A.H ÷ 50 Ampere = 3HRS

Hivyo inveter hiyo itafanya kazi kwa muda wa masaa 3 kabla haijazima

Mfano (ii)(tukizingatia kigezo cha efficiency)

Inverter inayo endesha mzigo wa watt 500 yenye efficient ya 70% imefungwa katika battery ya 12v yenye 150 A.H.Je inverter hiyo itafanya kazi kwa muda gani?
Solution
Igawanye 70 kwa 100 =70 ÷ 100 = 0.7

Chukua Wattage gawanya kwa efficiency = 500watt ÷ 0.7 = 714.2 watt

Tafuta current = 714.2 ÷ 12battery Voltage = 59.51 Ampere

Tafuta muda time kwa kutumia ampere yenye kigezo cha efficiency

Time = 150 A.H ÷ 59.51 = 2.5 HRS

Tumeona kwamba kama tukitumia battery bila kujari efficiency tunaweza kuitumia kwa masaa 3 Lakini kama tutajari kigezo cha efficiency tutatumia kwa masaa 2 tu!

Ndiyo maana kama mtu hafahamu hudhani inverter za dukani zinamaliza sana battery kwa sababu nyingi zina Over drain battery protection(efficiency between 70%-90%) hivyo hujizima mapema kuliko za kusuka ambazo nyingi hazina Over drain battery protection hivyo huwaka kwa muda mrefu hadi pale battery itakapo kwisha kabisa!

Hivyo kama wewe ni mteja utaamua mwenyewe mfumo upi kwako ni bora!

KATI YA INVERTER ZA DUKANI NA ZILE ZA KUSUKA ZIPI NZURI (BORA)?

Bila shaka wengi wamekuwa wakijiuliza sana swali hili wengine wanaamini za kusuka ni bora zaidi dhidi ya zile za dukani nawegine wanaamini kinyume chake!

Ukweli ni upi?

Mimi nadhani kabla hatujasema ipi ni nzuri lazima tufahamu inveter nzuri inatakiwa iwe na vitu gani (tukiacha swala la ukubwa au udogo wa inveter(power) because it is variable factor)

INVERTER BORA INATAKIWA IWE NA VITU VIFUATAVYO
-Iwe na circuit ya kuzuia overload
-Iwe na circuit ya kuzuia battery over drain
-Iwe na uwezo za kuhimili voltage surge(start up overload)
-Iwe na efficiency kuanzia 70%-90%

Jibu langu litakua ipi ni bora endapo tu itakuwa na vitu hivyo hapo juu

SIKWELI KWAMBA ETI INVETER NZURI INATEGEMEANA NA KIGEZO CHA KWAMBA ETI HII IMESUKWA NA MKONO AU HII NI YA KIWANDANI!

Tukitazama kigezo cha maintenance inverter za kusukwa ni bora zaidi kwani nyingi hutengenezwa kwa mfumo mnyambuko,hivyo ni rahisi kuzifanyia marekebisho pale zinapo haribika.Hivyo jitahidi kumtafuta fundi mzuri akusukie inverter yenye vitu muhimu kama nilivyo elekeza hapo juu.
Inverter za dukani ni ngumu sana kuzifanyia maintenance pale zinapo haribika kwasababu zinatumia vifaa vidogo vyenye mchanganyiko wa saketi yaani intergrated circuits(ICs),ambapo nyingine huwa ni ndogo sana kiasi cha kuhitaji vifaa vya ziada kuz
ihudumia.



KWA MASWALI ZAIDI WASILIANA NASI 0657-115587
 
Safi sana mkuu maelezo mazuri mno,mimi nataka Regulator yenye kuwezo kubeba hadi watt 3000 inawezekana kwako? Kama una ushsuri wa zaidi naomba pia.
 
Safi sana mkuu maelezo mazuri mno,mimi nataka Regulator yenye kuwezo kubeba hadi watt 3000 inawezekana kwako? Kama una ushsuri wa zaidi naomba pia.


Why NOT?It is possible!
 
Asante sana kwa maelezo ya kina.

Maswali yangu ni kama ifuatavyo:

  1. Nataka kuwa na solar system ambayo itaweza kunipa independent power supply (AC) ya kati ya saa 8 hadi 12, natakiwa kuwa na:
    1. Solar Panels ngapi?
    2. Battery Bank yenye LOAD kiasi gani?
    3. Ningependa kuwa na system ya 5,000 Watts, je, itaweza kutoa umeme wa kutosheleza kwa nyumba nzima ya kawaida, yenye 2 Fridges, 2 Deep Freezers, TV set, two computers (1 desktop, 1 laptop), taa kwenye vyumba tofauti 8, in two wings

Naombeni analysis yenu muifanye kisha mniletee specs na gharama kwa PM. Asante.
 
Asante sana kwa maelezo ya kina.

Maswali yangu ni kama ifuatavyo:

  1. Nataka kuwa na solar system ambayo itaweza kunipa independent power supply (AC) ya kati ya saa 8 hadi 12, natakiwa kuwa na:
    1. Solar Panels ngapi?
    2. Battery Bank yenye LOAD kiasi gani?
    3. Ningependa kuwa na system ya 5,000 Watts, je, itaweza kutoa umeme wa kutosheleza kwa nyumba nzima ya kawaida, yenye 2 Fridges, 2 Deep Freezers, TV set, two computers (1 desktop, 1 laptop), taa kwenye vyumba tofauti 8, in two wings

Naombeni analysis yenu muifanye kisha mniletee specs na gharama kwa PM. Asante.

Usijari tunalifanyia kazi,utajibiwa vizuri kabisa just be patient tukuandalie report.
 
Zaidi ya Dar, mikoani mnapatikana wapi? Mwanza mpo?
 
Huu ufafanuzi nimeupenda sana , hasa kwenye calculation.
 
Miye natumia Inverter kwenye gari ku-run vifaa vinavyohitaji 120V AC.
 
Hongereni kwa kuhudumia wananchi.

Nilitarajia kuona haya maneno mwisho wa yote, vinginevyo ningeshangaa kidogo.
KWA MASWALI ZAIDI WASILIANA NASI 0657-115587
-Tunatoa huduma ya kusuka inveter za ukubwa tofauti
-Tunatoa ushauri wa manunuzi ya solar system
-Tuna repair inverter zilizo kufa kabisa
-Tunarekebisha inverter zenye ukosefu wa system muhimu
-Tunasuka Un interrupted Power Supply (UPS) ambazo ni automatic kwa matumizi ya
nyumbani
-Tunashauri na kutoa uchambuziwa kiufundi juu ya mahitaji na aina ya inveter inayo
husika.

KARIBUNI SANA!
 
Mkuu weka paragraph mkuu, habari nzuri lakini haisomeki

Mi nadhani kwa somo alilotoa inatosha ! wengi waliojaliwa vipaji kama hivyo wamenyimwa vingine,

Let's. Give credit where credit is due!
 
100 AH battery, kwenye load ya 1A practically haiwezi kukaa masaa 100. This is simply because baada ya hapo hiyo battery itakuwa ni ya kutupa. Lazima ijulikane DOD (Depth Of Discharge) ya battery husika. Most of the deap cycle batteires, zina DOD ya 60%. Ukiidischarge kwa 100%, you can not recharge it to full as most of the cell zitakuwa damaged. Ni kama plastic na elastic limits. Mpira unaweza ukaufuta kwa kiwango fulani tu ndo ukiuacha unarudi kwenye original shape yake. Lakini ukivuka plastic limit, inakuwa na permanent damage na haiwezi rudio original shape
 
Nimetumia inverter na huu ni mwaka wa 12. Ila nimeipenda JEC, ina watts 300 na nilipoona kwamba inakula moto sana kuliko inverter fulani niliyokuwa naitumia kipindi cha nyuma, niliamua kuifungua na nikajaribu kupunguza output volts kutoka 220v-200v kwa kuzungusha coils mbili na kufanikiwa kuokoa moto uliokuwa unawahi kuisha. Sasa sijui kama naharibu kitu kimojawapo kati ya Battery, Inverter au Electrical appliances naomba msaada.
Baada ya hapo kuna swali jingine.
 
100 AH battery, kwenye load ya 1A practically haiwezi kukaa masaa 100. This is simply because baada ya hapo hiyo battery itakuwa ni ya kutupa. Lazima ijulikane DOD (Depth Of Discharge) ya battery husika. Most of the deap cycle batteires, zina DOD ya 60%. Ukiidischarge kwa 100%, you can not recharge it to full as most of the cell zitakuwa damaged. Ni kama plastic na elastic limits. Mpira unaweza ukaufuta kwa kiwango fulani tu ndo ukiuacha unarudi kwenye original shape yake. Lakini ukivuka plastic limit, inakuwa na permanent damage na haiwezi rudio original shape


According to the general formula it can provide 100 Ampere for 100 hours

Time=Battery capacity / Ampere required
Time=100AH/A1=100 Hours
But if you want to protect the battery from being over discharge,there now you can talk about efficiency!
 
Nimetumia inverter na huu ni mwaka wa 12. Ila nimeipenda JEC, ina watts 300 na nilipoona kwamba inakula moto sana kuliko inverter fulani niliyokuwa naitumia kipindi cha nyuma, niliamua kuifungua na nikajaribu kupunguza output volts kutoka 220v-200v kwa kuzungusha coils mbili na kufanikiwa kuokoa moto uliokuwa unawahi kuisha. Sasa sijui kama naharibu kitu kimojawapo kati ya Battery, Inverter au Electrical appliances naomba msaada.
Baada ya hapo kuna swali jingine.

Haujatuambia unatumia continous load kiasi gani!lakini kwa kifupi hakuna chochote kilicho haribika kwakuwa hujagusa mfumo wa kuprotect battery kuwa over discharged

Fahamu kuwa kuna circuit ambayo hutengenezwa maalumu kwa ajiri ya kulinda battery ambayo huwa ndani ya inverter yenyewe.

Labda nikueleze kwa nini muda wa matumizi yako umeongezeka

Let say una load ya watt 200w battery yako ni 12v 150 AH

Current=220v/200w=1.1Ampere

Time=150/1.1=136 hrs

Sasa ukipunguza Output voltage itakuwa hivi

Current=200v/200w=1Ampere

Time=150/1=150 hours

So it is true ukipunguza output voltage unaongeza time running ya inverter yako lakini hakuna ubaya but never go below 200v if you are using equipments which need 220v!
 
Back
Top Bottom