Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Katika ku-balance story, msije hangaika kumuuliza Kawawa; huyu hajawahi kuwa na mawazo yake mwenyewe tangu nianze kumsikiliza. Atakachowaeleza ni hayohayo ya Nyerere ambayo tayari mnayajua.
Nimesoma ile article mara kibao, sijaona hata chembe ya chumvi. Alichofanya yule mwandishi ni kusimulia kile ambacho hakijawahi kusimuliwa.

Lazima tukiri kwamba pamoja na mazuri ya mzee wetu Nyerere, ndani ya nguo zake alikuwa ni mtu hatari sana hasa katika kuwafanya wanasiasa wenzake waonekana ovyo mbele ya jamii. communist style. Unakumbuka jinsi Amini alivyochafuliwa: mla watu, alionyeshwa akibeba nyama za watu na huku inzi wakimzonga, lakini wote sasa tunajuwa kwamba pamoja na ubaya wa Amini hakufikia kiwango cha kubeba nyama za watu kwenye mzegazega, huo ulikuwa ni umafia aliofanyiwa.

Pamoja na mapenzi yangu kwa Nyerere, nasikitika kwamba huyu mzee alijaribu kwa mafanikio makubwa kuua kila kipaji cha mtu yeyote mwingine aliyeibuka. As a result, yeye peke yake mpaka leo anaonekana ndiye aliyekuwa hero. Lakini sote tunajua ukweli kwamba isingewezekana yeye tu peke yake alete mazuri. Sasa swali la kujiuliza hao wengine walikuwa akina na nani na kwa nini hatuwajui?
Mkumbo hata wewe asaiv mawazo yako yapo kifungoni, najua hata sasa una mapenzi na rais magufuli na ana madhaifu makubwa Mara mia afadhali madhaifu ya nyerere uliyosema hapa, lkn sababu ya keki ya taifa unayopata kwa sasa sidhani kama utaona dhaifu hata moja la magufuli, nimefanya hivi ili kukumbusha kuwa koti la kawawa ndo umelivaa wewe muda huu.
 
Kambona alikuwa mwongo. Tena alikuwa mtu wa wivu sana. Hakuwapenda Kawawa na Jamal, na mpaka sasa sababu zake sijui. Lakini sababu kubwa ya Mwalimu kumwambia Kenyatta amwachie ni kwamba hakutaka kumfanya Kambona "a hero" kwa kumweka ndani. Baada ya kuondoka Mwalimu aliwang'oa polepole watu wake aliokuwa amewapachika katika idara ya usalama wa taifa na jeshini. Kwa hiyo historically it was a good move.
wewe lazima ni jasusi mstaafu umeyajuaje haya!
 
Battle ya Kambona na Mwalimu Nyerere ni ya kiitikadi na maono kuhusu uelekeo wa Taifa kuliko ubinafsi unaozungumzwa bila kujali uhalisia wa mambo.

Yale anayoshutumiwa nayo Kambona, alijisafisha nayo kabla hata ya matope kumtapakaa baada ya kurushiwa na wafuasi wa Mwalimu.

Ni ukweli ulio wazi kuwa Kambona hakuupenda Ujamaa ilhal Mwalimu aliuchukia Ubepari. Vyovyote iwavyo leo tu mashahid kuwa Kambona alikuwa na maono sahihi zaidi katika kuendesha nchi kupitia soko huria kuliko kucentralize kila nyenzo ya kiuchumi kama alivyoamini Mwalimu Nyerere.

Hatutaki kuukubali ukweli lakini sera za ujamaa na arrogance ya Mwalimu n chanzo kikuu cha Umaskini wa Tanzania tulio nayo. Alihubir nadharia na kufanya yalioshindwa.

Naiita vita ile ya Mwalimu vs Kambona kama "Wretched Battle of the Country".

Usahihi wa Kambona upo kweny anguko la Ujamaa. Usahihi wa Kambona upo kweny ufukara tulio nao leo hii. Aliiona leo yetu licha ya kuwa aliishi jana yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
thanks
Ngoja nitoe kumbukumbu yangu, it may have holes.

Inasemekana kuwa Kambona alikuwa rafiki mkubwa sana wa Nyerere aliyekuwa bestman kwenye harusi yake iliyofanyika London. Katika serikali za kwanza kwanza za Nyerere, Kambona alikuwa ni Waziri mwandamizi aliyekuwa an sauti kuliko mawaziri wengin wote, isipokuwa labda Kawawa. Wakati wa maasi ya 1964, inasemekana pia kuwa ni Kambona na Okello ndio walioongea na kuwatuliza askari waasi. Vile vile katika zile siku 100 za kuelekea Muungano, Nyerere alisikiliza sana ushauri wa Kambona kuliko mtu yeyote kuhuhusu umuhimu wa muungano na structure yake.

Hata hivyo baadaye uhusiano kati ya Kambona na Nyerere ulianza kuwa mbaya hasa pale Kambona alipoanza kujenga majumba mengi ya kupangisha Dar kwa haraka haraka huku akiwa waziri, jambo ambalo halikuwa tamu kwa Nyerere. Halafu wakati Nyerere anaandika Azimio la Arusha, Kambona alijitokeza kumpinga Nyerere directly kutokana na ile miiko ya uongozi ambayo ilikuwa inaingiliana na zile nyumba alizokuwa amejenga hapo Dar.

Kwa vile mwishoni lile Azimio la Arusha lilipita na kuanza kutaifisha majumba ya kupangisha yakiwemo na yale ya kambona, basi Kambona akasuka mpango wa kumpindua Nyerere kusudi kusimamisha hiyo operation ya Azimio la Arusha. Waliohusika katika mpango walikuwa wengi sana ikiwa ni pamoja na Titi Mohammed, Lifa Chipaka, Kamaliza, na wengineo. Sielewi mpango wenyewe ulivujaje, lakini wahusika wote walishikwa na kuswekwa kwenye gereza la Keko. Kutokana na umaarufu wake, Kambona alisaidiwa na walinzi wa gereza hilo kutotoroka. Nadhani kwanza alikimbilia Malawi ambako ndiko alikoondokea kwenda kuishi uhamishoni London.

Kitu kimoja binafsi huwa nadhani kuwa Mzee kambona was right kuhusu vipengele kadhaa vya Azimio la Arusha, hasa ule utaifishaji wa njia kuu zote za uchumi. Hata hivyo kwenye miiko ya uongozi nadhani vile vile alikuwa kakosea. Kilichotakiwa ni kuwa kuandika upya miiko hiyo huku ikiheshimu mali alizokuwa nazo mtu kabla ya kuwa kiongozi.
 
uko sawa mkuu
Battle ya Kambona na Mwalimu Nyerere ni ya kiitikadi na maono kuhusu uelekeo wa Taifa kuliko ubinafsi unaozungumzwa bila kujali uhalisia wa mambo.

Yale anayoshutumiwa nayo Kambona, alijisafisha nayo kabla hata ya matope kumtapakaa baada ya kurushiwa na wafuasi wa Mwalimu.

Ni ukweli ulio wazi kuwa Kambona hakuupenda Ujamaa ilhal Mwalimu aliuchukia Ubepari. Vyovyote iwavyo leo tu mashahid kuwa Kambona alikuwa na maono sahihi zaidi katika kuendesha nchi kupitia soko huria kuliko kucentralize kila nyenzo ya kiuchumi kama alivyoamini Mwalimu Nyerere.

Hatutaki kuukubali ukweli lakini sera za ujamaa na arrogance ya Mwalimu n chanzo kikuu cha Umaskini wa Tanzania tulio nayo. Alihubir nadharia na kufanya yalioshindwa.

Naiita vita ile ya Mwalimu vs Kambona kama "Wretched Battle of the Country".

Usahihi wa Kambona upo kweny anguko la Ujamaa. Usahihi wa Kambona upo kweny ufukara tulio nao leo hii. Aliiona leo yetu licha ya kuwa aliishi jana yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkumbo hata wewe asaiv mawazo yako yapo kifungoni, najua hata sasa una mapenzi na rais magufuli na ana madhaifu makubwa Mara mia afadhali madhaifu ya nyerere uliyosema hapa, lkn sababu ya keki ya taifa unayopata kwa sasa sidhani kama utaona dhaifu hata moja la magufuli, nimefanya hivi ili kukumbusha kuwa koti la kawawa ndo umelivaa wewe muda huu.
keki ya taifa ni shidaa😄😄😄
 
Kama walitofautiana mitazamo/itikadi basi ni dhahiri kwamba lazima mmoja angeendelea mmoja angebaki.
 
Battle ya Kambona na Mwalimu Nyerere ni ya kiitikadi na maono kuhusu uelekeo wa Taifa kuliko ubinafsi unaozungumzwa bila kujali uhalisia wa mambo.

Yale anayoshutumiwa nayo Kambona, alijisafisha nayo kabla hata ya matope kumtapakaa baada ya kurushiwa na wafuasi wa Mwalimu.

Ni ukweli ulio wazi kuwa Kambona hakuupenda Ujamaa ilhal Mwalimu aliuchukia Ubepari. Vyovyote iwavyo leo tu mashahid kuwa Kambona alikuwa na maono sahihi zaidi katika kuendesha nchi kupitia soko huria kuliko kucentralize kila nyenzo ya kiuchumi kama alivyoamini Mwalimu Nyerere.

Hatutaki kuukubali ukweli lakini sera za ujamaa na arrogance ya Mwalimu n chanzo kikuu cha Umaskini wa Tanzania tulio nayo. Alihubir nadharia na kufanya yalioshindwa.

Naiita vita ile ya Mwalimu vs Kambona kama "Wretched Battle of the Country".

Usahihi wa Kambona upo kweny anguko la Ujamaa. Usahihi wa Kambona upo kweny ufukara tulio nao leo hii. Aliiona leo yetu licha ya kuwa aliishi jana yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni sawa Kawawa alikuwa sahihi hatuna shida na hilo!

Lakini huyu Kambona alishiriki kutunga Sera na Misingi ya Azimio la Arusha,wazi wazi ndani ya jopo la Mwalimu Nyerere! wakakubaliana kwa Umoja jinsi ya kulitekeleza! kwa nini baadaye aligeuka na kulikana? ili kutekeleza kile alicho shiriki kukianzisha?

ni wazi alikuwa ni tatizo la ki-Juda mbele ya macho ya wenye akili hata km huyo angekuwa Rais wetu na kuleta huo Ubepari, angeongoza vibaya, na tungekuwa pabaya zaidi kuliko Ubepari wa mpito tulio nao leo!

Sisi Tanzania siyo maskini hata kidogo sema wewe Mungu amekupiga Kofi tu, Maghorofa haya yoote? Afya bure, Nyumba Bure NH, Nyumba za Biafra kila Mkoa, Barabara lami mpaka chooni, Elimu yetu Bure kwa miaka 50 tu ya Uhuru tuko hapa pazauri,

Taifa la watu tulioathiriwa na Utumwa, Ukoloni, Vita za mara kwa mara za Majirani zetu, lkn bado tuko ngangari, unakufuru bure mwishowe Mungu atuadhibu kwa domo lako! kukosa shkrani! tembea USA uone lundo la Maskini, Lesotho, Senegal ni utachoka wewe! haya maneno ume-copy ya watu vitabuni! sema ya kwako ya dhati moyoni.
 
Kamba!

Agosti 13, 1925 haikuwa Ijumaa! Tuanzie hapo kwanza kwanza.

Which means probably hata hayo mengine ya mvua kali ilikuwa inanyesha, jioni radi kali akiwa anazaliwa nayo ni kamba tupu!


whatsapp-2bimage-2b2019-01-27-2bat-2b19-28-11-25281-2529-jpeg.1007392


Nyerere hawezi kuwa msimamizi wakati hata kwenye harusi hakuwepo.

A picture is worth a thousand lies!
Dah! eeeh! weee jamaa hatari sana, kwa hiyo umerudi nyumaaa! mpaka siku tarehe mwaka? JF si machejo, hadanganywi mtu humu! umesahau kuwa miaka ya zamani kabla ya uhuru siyo kama ya siku hizi!
 
Mengi yamesemwa kuhusu Mzee wetu huyu na sisi tuliokuwa shuleni wakati ule tulilishwa kile ambacho naamini ni sumu. Wakubwa tuelimisheni ukweli kuhusu Mzee huyu.

View attachment 1371792
Oscar Kambona




Natumaini waandishi wa historia ya tanzania watampa nafasi yake kwa mchango mkubwa aliyoutoa.
RIP Mzee Kambona


Oscar Salathiel Kambona, alitaka kumpindua Nyerere kwa kushirikiana na wapiganaji wa Umkhonto.
[/h]

=======


Kichakaa man, ameandika;

Marehemu Oscar Kambona alizaliwa mwaka 1925 katika kijiji cha Kwambe kilichopo mwambao mwa ziwa Nyasa, karibu na Mbamba-bay, wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma. Alikuwa mtoto wa marehemu Rev. David Kambona na Bibi Miriam Kambona.

Rev. Kambona alikuwa ni miongoni mwa waafrika wa kwanza kupata upadre katika kanisa la Anglikana la Tanganyika. Wakati Oscar Kambona akiwa mdogo, baba yake alikuwa akimweleza kuhusu ndoto zake juu ya uhuru wa nchi yake, hivyo Oscar alikuwa akiwa na hamu sana ya kuitumikia nchi yake.

Oscar alipata elimu ya msingi nyumbani kwao, chini ya mwembe (ambao bado upo), katika kijiji chao kwa kuwatumia wazazi wake wote wawili na mjomba wake, ambao wote walikuwa walimu. Baada ya hapo alipelekwa shule ya kati ya Mt. Barnabas, Liuli, na baadaye shule ya Sekondari ya Alliance, ambako alilipiwa ada na Askofu mzungu wa Anglikana kwa vile baba yake hakuweza kumudu kulipa ada ya paundi 30 kwa mwaka.

Oscar alikuwa akisimulia jinsi alivyoweza kumshawishi Askofu huyo amlipie ada kwa kusema sala ya Baba yetu kwa kizungu. Oscar alichaguliwa kwenda ‘Tabora Boy’s Senior Government School’, ambako alionana na Julius Nyerere kwa mara ya kwanza; wakati huo Nyerere alikuwa anafundisha katika shule ya kikatoliki.

Baada ya kumaliza masomo ya sekondari alienda katika shule yake iliyopita ya Alliance kama mwalimu na baadae alichaguliwa kuwa ‘Schoolmaster’. Ilikuwa katika mkutano wa kitaifa wa walimu, mnamo mwaka 1954, ambapo Kambona na Nyerere walikutana tena.

Kambona alikuwa tayari kukitumikia chama cha TANU ambacho kilikuwa kimeanzishwa muda si mrefu, lakini Nyerere akasema wasingeweza kumwajiri kwa vile chama kilikuwa hakina fedha.

Kambona akasema chama hakikuwa na fedha kwa vile hakikuwa na ‘organising secretary, na ndipo alipoamua kufanya kazi hiyo ili kujenga chama, bila ya malipo’. Aliishi kwa kutegemea akiba aliyojitunzia kwa kufanya kazi miezi 6.

Katika kipindi hiki Kambona alisafiri sehemu mbalimbali za nchi na kuonana na machifu na wazee wa vijiji ili kusajili wanachama. Katika miezi 6 alifanikiwa kusajili wanachama 10,000, na hadi kufikia mwaka mmoja alikuwa amepata wanachama hai 100,000. Kambona alitumia michango aliyopata kufungua akaunti ya kwanza ya TANU.

alienda Butiama kumshawishi Nyerere achukuwe uongozi wa chama moja kwa moja. Baada ya miaka mitatu Kambona aliamua kwenda kusomea sheria katika Chuo cha Middle Temple, nchini Uingereza mwaka 1957 kwa ufadhili wa Gavana.

Akiwa London Kambona alikuwa kiongozi wa chama cha wanafunzi wa Tanganyika na Mwenyekiti wa tawi la TANU la London. Ni wakati huo ambapo Kambona alipata fursa ya kukutana kwa mara ya kwanza na watu mashuhuri kama George Padmore, mwanaharakati wa umoja wa Afrika, ambaye alimshawishi ahudhurie mkutano wa mwaka 1958 wa waafrika wote(All Africa’s Peoples Conference), uliofanyika nchini Ghana muda mfupi baada ya kupata Uhuru.

Akiwa Ghana Kambona alipata nafasi ya kukutana na mwanaharakati mwingine maarufu wa siasa za Afrikla, Kwame Nkurumah. Akiwa uingereza Kambona alikuwa mwaafrika wa kwanza kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili katika idhaa ya kiswahili ya BBC.

Aliporudi nchini Tanganyika, mwaka 1959, TANU ilikuwa imeshaweka bayana madai yake ya kupewa serikali ya madaraka, vinginevyo TANU ilikuwa tayari kuanzisha mapambano kama ilivyokuwa kwa Mau Mau ya Kenya. Wakiwa London wakisubiri kupewa madaraka ya ndani, Nyerere na Kambona walijadili hatua mbalimbali ambazo zingechukuliwa ili kuepuka kutoweka kwa amani.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Londoni 1991, Kambona alikumbuka matukio kama hivi, ‘’Bwana Nyerere alikuwa akiishi nami katika chumba kidogo nilichopewa chuoni.

Tulijadiliana ni namna gani angeweza kurudi nyumani na kuonana na wafuasi wake bila kupewa serikali ya madaraka. Baadae nilifanikiwa kumshauri kuwa wakati atapozungumza na vyombo vya habari katika the East African Arch aseme kuwa walowezi wa kizungu ambao wapo Tanganyika wana hekima zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki.

Alikubali kusema hivyo endapo na yeye Kambona angekubali kukatisha masomo yake ya sheria huko London na kurudi Tanganyika ili ampe nguvu na kumuunga mkono katika kikao cha kamati kuu ya TANU wakati akitetea tamko lake la wenye hekima zaidi.

Katika uchaguzi wa kwanza TANU ilishinda viti vyote isipokuwa kimoja. TANU iliunda serikali ya mambo ya ndani chini ya Nyerere ambaye alikuwa Waziri kiongozi wa kwanza.

Na katika harakati hizo za matayarisho ya serikali ya ndani, Kambona alimwoa Flora Moriyo wakati wakiwa kwenye msafara wa harakati za kukamilisha matayarisho ya uhuru na serikali ya Uingereza. Harusi ilifungwa katika kanisa la Mt. Paul, London, na Nyerere ndiye alikuwa msimamizi. Kambona aliteuliwa kuwa waziri wa Elimu.

Baadaye alishika nyadhifa za waziri wa Mambo ya Ndani, Mambo ya nchi za nje na Ulinzi na Tawala za Mikoa. Pia alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika na mwenyekiti wa utayarishaji wa AOU charter.

Mwaka 1964, Kambona alifanya kazi kubwa katika kuunganisha Zanzibar na Tanganyika, akiwa pamoja na Raisi Nyerere, Raisi Karume na Waziri Kiongizi Hanga. Hii ilikuwa ni baada ya mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati wa wanajeshi wa kikosi cha Calito walipoasi mwaka 1964 Kambona alikuwa msuluhishi mkuu kati ya serikali na wanajeshi hao. Nyerere na Kawawa walienda mafichoni Kigamboni. Baada ya siku tatu za majadiliano Kambona aliafiki kuongeza kasi ya kuwawezesha waafrika kushika hatamu jeshini.

Katika mahojiano na gazeti la Daily Telegraph la London Kambona alisema, ‘baada ya kuwatuliza wanajeshi nilikwenda kuwatafuta viongozi wengine na kuwarudisha mjini kwa kutumia Land Rover yangu’. Hatimaye maasi hayo yalidhibitiwa kabisa na majeshi ya Uingereza na Nyerere alimsifu Kambona bushara na uaminifu wake.

Tofauti kati ya Nyerere na Kambona zilianza kujitokeza baada ya maasi ya wanajeshi. Nyerere alitaka kuanzisha mfumo wa chama kimoja nchini ili kuimarisha usalama. Kambona alipinga hoja hiyo kwa maelezo kwamba mfumo huo ungezorotesha uhuru wa watu na maendeleo ya demokrasia.

Hata hivyo, Kambona alishindwa bungeni; alikataa kusaini muswada (bill). Mwaka 1967, baada ya safari ya China ya mwaka 1965, Nyerere akiwa amependezwa na mfumo wa kikomonist wa Mao, alitaka kuanzisha mfumo kama huo kwa jina la ujamaa.

Dhana ya msingi ya mfumo wa ujamaa ilikuwa ni kuwahamishia watu katika vijiji vya ujamaa na kutaifisha viwanda ana mali. Kambona hakukubaliana na utaratibu huo kwa maelezo kwamba ungeongeza umaskini na udhibiti wa serikali kwa watu.

Alijiuzulu kutoka katika serikali na Chama na hatimaye yeye na familia yake walikimbilia Kenya na kisha Uingereza ambako walipatiwa uhifadhi wa kisiasa. Mara baada ya kuondoka mali za Kambona zilichukuliwa.

Ndugu zake wawili, waliwekwa kizuizini bila ya kufikishwa mahakamani na kufungwa kwa zaidi ya miaka kumi. Wanafamilia wengine walinyanyaswa na kuwekwa kizuizini. Wengine kati yao walibambikiziwa kesi za uhaini, wakafikishwa mahakamani na kisha kufungwa na serikali.

Kati yao walikuwa Bibi Titi ambaye alipigania uhuru pamoja ana Nyerere na alikuwa kiongozi wa jumuia ya kina mama. Alikuwepo pia Michael Kamaliza ambaye alikuwa mwanaharakati wa chama cha wafanyakazi, mwanachama wa TANU na waziri.

Wengine ni pamoja na Gray Mattaka, John ana Eliya Chipaka na Prisca Chiombola. Kambona alituhumiwa kuwa kiongozi wa wahaini wakati akiwa London na alihukumiwa bila kuwapo. Watuhumiwa hatimaye walikata rufaa katika mahakama kuu ya Afrika Mashariki na wakaachiwa huru.

Hata hivyo, baadae walikamatwa na serikali na kufungwa tena. Kambona alituhumiwa kuwa aliiba pesa nyingi sana zikiwa ni mali ya umma, kitu ambacho Kambona alikataa katika taarifa yake na waandishi wa habari Septemba 6 huko London 1967.

Tuhuma hizo zilisema kuwa ‘’ Kambona amekutwa na pesa nyingi sana kama karanga alipopekuliwa katika Uwanja wa ndege Embakasi Nairobi’’ Hata hivyo Kambona katika taarifa yake kwa waandishi wa habari alikanusha kuhusika na tuhuma hizi na badala yake akaipa serikali ya Tanzania kuiomba serikali ya Kenya kutoa ukweli juu ya jambo hilo- jambo halikufanyika.

Akiwa Londoni Kambona aliishi maisha ya shida na dhiki. Katika mwaka 1982 ndugu zake Kambona na Otini Kambona walifunguliwa kutoka kizuizini baada ya juhudi za waziri mkuu wa New Zealand Robert Muldoon. Katika mwaka 1990 Kambona akiwa na matumaini makubwa ya mabadiliko ya kisiasa katika Tanzania hususani mabadiliko ya demokrasia, aliunda chama kiitwacho Tanzania Democratic Alliance.

Wakati vyama vingi vilipoanzishwa Tanzania 1992 Kambona aliomba kurudi Tanzania. Serikali ya Tanzania ilimkatalia katakata na kudai kuwa Kambona hakuwa Mtanzania. Kambona badala yake aliomba Serikali ya Uingereza kumpa pasi ya kusafiria kurudi Tanzania. Hata hivyo Serikali ya Tanzania ilitamka kwamba pamoja na kupata pasi hiyo itamweka ndani pindi atakapoingia Tanzania.

Pamoja na msimamo huo wa Serikali, Kambona alitua kwenye ardhi ya Tanzania tarehe 5 september 1992. Hakuna mamlaka iliyomkamata bwana Kambona bali alipewa miezi mitatu awe amekamilisha utata wa uraia wake. Baada ya kurudi, Tanzania aliona kuwa harakati za kuelekea kwenye demokrasia ya kweli zilikuwa zikienda kwa mwendo wa kinyonga.

Hata hivyo Kambona hakuweza kujihusisha kwa kiasi kikubwa na siasa kutokana na matatizo ya kiafya hususani shinikizo la damu. Hatimaye Oscar Kambona alifariki akiwa katika matibabu mjini London mwezi Juni 1997.

Mdogo wake Otini Kambona naye alifariki katika kipindi hichohicho kutokana na magonjwa ya moyo. Wote wawili walizikwa Tanzania, na serikali ya Tanzania iligharimia gharama zote za usafirishaji miili ya marehemu ndugu hawa.

Oscar Kambona ameacha mke na watoto wawili. Mtoto wao wa kwanza Mosi Kambona aliuawa mjini London katika mazingira ya kutatanisha. Roho ya Oscar Kambona na ndugu na jamaa wote waliotangulia MWENYEZI MUNGU aziweke pema peponi, Amin.

Kumsoma bonyeza hapa
Kambona Anatakiwa kusafishwa jina , kulikuwa na dhana mbili Moja kutofautiana kiitikadi na mwalimu , lakini kubwa ni ile kuonewa Wivu na wenzake kwani wakati wa Maasi ya 1964 yeye ndiye alikuwa nyota wa mchezo na laiti angetaka angeweza kutwaaa madaraka , lakini haikua kwenye akili yake , alipambana sana kusaidia Mwalimu awe salama , pamoja na Kawawa ...baada ya pale wenzake walianza kumuona tishio haswa KAWAWA wakaanza kupeleka maneno ya uchonganishi kwa NYERERE.....
Andrew Nyerere yuko hapa atuambie maana hizi zilikuwa family friends
 
Mkuu Nyani,

Heshima mbele, I like kila ulichosema so far kwenye hii topic, now ngoja tujairbu kuchambua kidogo:-

1. After the mutiny, differences between Kambona and Nyerere began to appear. Nyerere wanted to introduce a one party system into Tanzania to strengthen state security. Kambona argued against the move claiming that it would inhibit peoples freedom and progress towards democracy. However, Kambona was defeated in parliament. He refused to sign the bill.

I mean right here, ndipo mambo yetu yalipoanza kwenda mrama as a nation, na ndio ninayoyasema kila siku, kumbuka kuwa to this point tulikuwa on the right track, kuaniza uchumi, uongozi, mpaka siasa, now look at the turn of events ambazo eventually, ndio zilizotufikisha tulipo!

2. In 1967 after a trip to China in 1965, Nyerere impressed with Maos style of communism, wanted to adopt the same system under the guise of Ujamaa. The main doctrine behind Ujamaa was the relocation of peasants into village communes and the nationalization of all industries and property. Kambona did not agree with the policies, arguing that they would rather increase poverty and state control over the people. He resigned from the Government and the party and later with his family fled to neighbouring Kenya and then UK were he was granted political asylum.

Tizama kiongozi aliyekuwa na uwezo wa kuona mbali, exactly his argument then ndio hasa yalipolalia matatizo yetu, kumbe walikuwepo wenye akili ya kuona mbele, I mean this is very interesting story, pumba na mchele uko clear upande gani?

3. Immediately thereafter, Kambonas properties were confiscated. His two brothers Mattiya and Ottini Kambona were detained without trial and put in prison for over ten years. Other family members were harassed and detained. Some were falsely accused of plotting to overthrow the Tanzanian Government and were tried and imprisoned by the Government.

Wooow! Yaaani kweli haya mambo yalifanyika bongo under Mwalimu?

4. Most famous of these were Bibi Titi who fought alongside Nyerere in the independence movement and was head of the womans wing and also Michael Kamaliza, the former trade unionist and TANU member and government Minister. Other family members included Gray Mattaka, John and Elia Chipaka and Prisca Chiombola. Kambona was also accused of being the ring leader of the plotters while in London and was tried in absentia. The accused finally appealed to the East African High Court and were acquitted. Though they were later rounded up by the Tanzanian government and thrown into jail again.

5. Kambona was also accused of stealing millions of public funds,

6. Kambona challenged the Tanzanian government to request the Kenyan authorities to substantiate the allegations which they never did.

7. In London Kambona led a tough life in exile under considerable financial constraints. However in 1982, his two brothers Mattiya and Otini Kambona were eventually released from detention after the intervention of New Zealand Prime Minister Robert Muldoon.


8. On returning to Tanzania Kambona found that the progress towards democracy was disappointingly slow.


9. His eldest son Mosi Kambona was murdered in London in unexplained circumstances.

Sasa wakuu wangu bado kuna maswali kwamba kwa nini as a nation tupo hapa tulipo? Maana kwanga naona majibu yako clear hapa, kama kuna story ya upande wa pili tungekuwa tumeshaisikia, na pia tuliambiwa Kambona amekimbia Azimio La Arusha, lakini hapa ukweli unajionyesha wazi, au labda tusubiri na upande wa pili ulete yao pia, otherwise I am convinced kuwa huu ndio ukweli wenyewe wa kwa nini taifa letu limekwama!

Ahsante Mtoa Mada, yaanai you made my day!
Imagine walituma watu wakamuuwa Mwanaye just to frustrate him
 
Nyerere kwanza alivyoambiwa kwamba Kambona anamsema vibaya, hakuamini.

Ilimchukua mhariri wa magazeti ya serikali, Benjamin William Mkapa, mtu aliyekuwa na waandishi wa habari wanaofuatilia mambo ya Kambona kwa karibu, juhudi kubwa sana kumfanya Nyerere akubali habari kwamba Kambona anamsema vibaya Nyerere.
Alikuwa anamuamini Saana ...
 
Mengi yamesemwa kuhusu Mzee wetu huyu na sisi tuliokuwa shuleni wakati ule tulilishwa kile ambacho naamini ni sumu. Wakubwa tuelimisheni ukweli kuhusu Mzee huyu.

View attachment 1371792
Oscar Kambona




Natumaini waandishi wa historia ya tanzania watampa nafasi yake kwa mchango mkubwa aliyoutoa.
RIP Mzee Kambona


Oscar Salathiel Kambona, alitaka kumpindua Nyerere kwa kushirikiana na wapiganaji wa Umkhonto.
[/h]

=======


Kichakaa man, ameandika;

Marehemu Oscar Kambona alizaliwa mwaka 1925 katika kijiji cha Kwambe kilichopo mwambao mwa ziwa Nyasa, karibu na Mbamba-bay, wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma. Alikuwa mtoto wa marehemu Rev. David Kambona na Bibi Miriam Kambona.

Rev. Kambona alikuwa ni miongoni mwa waafrika wa kwanza kupata upadre katika kanisa la Anglikana la Tanganyika. Wakati Oscar Kambona akiwa mdogo, baba yake alikuwa akimweleza kuhusu ndoto zake juu ya uhuru wa nchi yake, hivyo Oscar alikuwa akiwa na hamu sana ya kuitumikia nchi yake.

Oscar alipata elimu ya msingi nyumbani kwao, chini ya mwembe (ambao bado upo), katika kijiji chao kwa kuwatumia wazazi wake wote wawili na mjomba wake, ambao wote walikuwa walimu. Baada ya hapo alipelekwa shule ya kati ya Mt. Barnabas, Liuli, na baadaye shule ya Sekondari ya Alliance, ambako alilipiwa ada na Askofu mzungu wa Anglikana kwa vile baba yake hakuweza kumudu kulipa ada ya paundi 30 kwa mwaka.

Oscar alikuwa akisimulia jinsi alivyoweza kumshawishi Askofu huyo amlipie ada kwa kusema sala ya Baba yetu kwa kizungu. Oscar alichaguliwa kwenda ‘Tabora Boy’s Senior Government School’, ambako alionana na Julius Nyerere kwa mara ya kwanza; wakati huo Nyerere alikuwa anafundisha katika shule ya kikatoliki.

Baada ya kumaliza masomo ya sekondari alienda katika shule yake iliyopita ya Alliance kama mwalimu na baadae alichaguliwa kuwa ‘Schoolmaster’. Ilikuwa katika mkutano wa kitaifa wa walimu, mnamo mwaka 1954, ambapo Kambona na Nyerere walikutana tena.

Kambona alikuwa tayari kukitumikia chama cha TANU ambacho kilikuwa kimeanzishwa muda si mrefu, lakini Nyerere akasema wasingeweza kumwajiri kwa vile chama kilikuwa hakina fedha.

Kambona akasema chama hakikuwa na fedha kwa vile hakikuwa na ‘organising secretary, na ndipo alipoamua kufanya kazi hiyo ili kujenga chama, bila ya malipo’. Aliishi kwa kutegemea akiba aliyojitunzia kwa kufanya kazi miezi 6.

Katika kipindi hiki Kambona alisafiri sehemu mbalimbali za nchi na kuonana na machifu na wazee wa vijiji ili kusajili wanachama. Katika miezi 6 alifanikiwa kusajili wanachama 10,000, na hadi kufikia mwaka mmoja alikuwa amepata wanachama hai 100,000. Kambona alitumia michango aliyopata kufungua akaunti ya kwanza ya TANU.

alienda Butiama kumshawishi Nyerere achukuwe uongozi wa chama moja kwa moja. Baada ya miaka mitatu Kambona aliamua kwenda kusomea sheria katika Chuo cha Middle Temple, nchini Uingereza mwaka 1957 kwa ufadhili wa Gavana.

Akiwa London Kambona alikuwa kiongozi wa chama cha wanafunzi wa Tanganyika na Mwenyekiti wa tawi la TANU la London. Ni wakati huo ambapo Kambona alipata fursa ya kukutana kwa mara ya kwanza na watu mashuhuri kama George Padmore, mwanaharakati wa umoja wa Afrika, ambaye alimshawishi ahudhurie mkutano wa mwaka 1958 wa waafrika wote(All Africa’s Peoples Conference), uliofanyika nchini Ghana muda mfupi baada ya kupata Uhuru.

Akiwa Ghana Kambona alipata nafasi ya kukutana na mwanaharakati mwingine maarufu wa siasa za Afrikla, Kwame Nkurumah. Akiwa uingereza Kambona alikuwa mwaafrika wa kwanza kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili katika idhaa ya kiswahili ya BBC.

Aliporudi nchini Tanganyika, mwaka 1959, TANU ilikuwa imeshaweka bayana madai yake ya kupewa serikali ya madaraka, vinginevyo TANU ilikuwa tayari kuanzisha mapambano kama ilivyokuwa kwa Mau Mau ya Kenya. Wakiwa London wakisubiri kupewa madaraka ya ndani, Nyerere na Kambona walijadili hatua mbalimbali ambazo zingechukuliwa ili kuepuka kutoweka kwa amani.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Londoni 1991, Kambona alikumbuka matukio kama hivi, ‘’Bwana Nyerere alikuwa akiishi nami katika chumba kidogo nilichopewa chuoni.

Tulijadiliana ni namna gani angeweza kurudi nyumani na kuonana na wafuasi wake bila kupewa serikali ya madaraka. Baadae nilifanikiwa kumshauri kuwa wakati atapozungumza na vyombo vya habari katika the East African Arch aseme kuwa walowezi wa kizungu ambao wapo Tanganyika wana hekima zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki.

Alikubali kusema hivyo endapo na yeye Kambona angekubali kukatisha masomo yake ya sheria huko London na kurudi Tanganyika ili ampe nguvu na kumuunga mkono katika kikao cha kamati kuu ya TANU wakati akitetea tamko lake la wenye hekima zaidi.

Katika uchaguzi wa kwanza TANU ilishinda viti vyote isipokuwa kimoja. TANU iliunda serikali ya mambo ya ndani chini ya Nyerere ambaye alikuwa Waziri kiongozi wa kwanza.

Na katika harakati hizo za matayarisho ya serikali ya ndani, Kambona alimwoa Flora Moriyo wakati wakiwa kwenye msafara wa harakati za kukamilisha matayarisho ya uhuru na serikali ya Uingereza. Harusi ilifungwa katika kanisa la Mt. Paul, London, na Nyerere ndiye alikuwa msimamizi. Kambona aliteuliwa kuwa waziri wa Elimu.

Baadaye alishika nyadhifa za waziri wa Mambo ya Ndani, Mambo ya nchi za nje na Ulinzi na Tawala za Mikoa. Pia alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika na mwenyekiti wa utayarishaji wa AOU charter.

Mwaka 1964, Kambona alifanya kazi kubwa katika kuunganisha Zanzibar na Tanganyika, akiwa pamoja na Raisi Nyerere, Raisi Karume na Waziri Kiongizi Hanga. Hii ilikuwa ni baada ya mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati wa wanajeshi wa kikosi cha Calito walipoasi mwaka 1964 Kambona alikuwa msuluhishi mkuu kati ya serikali na wanajeshi hao. Nyerere na Kawawa walienda mafichoni Kigamboni. Baada ya siku tatu za majadiliano Kambona aliafiki kuongeza kasi ya kuwawezesha waafrika kushika hatamu jeshini.

Katika mahojiano na gazeti la Daily Telegraph la London Kambona alisema, ‘baada ya kuwatuliza wanajeshi nilikwenda kuwatafuta viongozi wengine na kuwarudisha mjini kwa kutumia Land Rover yangu’. Hatimaye maasi hayo yalidhibitiwa kabisa na majeshi ya Uingereza na Nyerere alimsifu Kambona bushara na uaminifu wake.

Tofauti kati ya Nyerere na Kambona zilianza kujitokeza baada ya maasi ya wanajeshi. Nyerere alitaka kuanzisha mfumo wa chama kimoja nchini ili kuimarisha usalama. Kambona alipinga hoja hiyo kwa maelezo kwamba mfumo huo ungezorotesha uhuru wa watu na maendeleo ya demokrasia.

Hata hivyo, Kambona alishindwa bungeni; alikataa kusaini muswada (bill). Mwaka 1967, baada ya safari ya China ya mwaka 1965, Nyerere akiwa amependezwa na mfumo wa kikomonist wa Mao, alitaka kuanzisha mfumo kama huo kwa jina la ujamaa.

Dhana ya msingi ya mfumo wa ujamaa ilikuwa ni kuwahamishia watu katika vijiji vya ujamaa na kutaifisha viwanda ana mali. Kambona hakukubaliana na utaratibu huo kwa maelezo kwamba ungeongeza umaskini na udhibiti wa serikali kwa watu.

Alijiuzulu kutoka katika serikali na Chama na hatimaye yeye na familia yake walikimbilia Kenya na kisha Uingereza ambako walipatiwa uhifadhi wa kisiasa. Mara baada ya kuondoka mali za Kambona zilichukuliwa.

Ndugu zake wawili, waliwekwa kizuizini bila ya kufikishwa mahakamani na kufungwa kwa zaidi ya miaka kumi. Wanafamilia wengine walinyanyaswa na kuwekwa kizuizini. Wengine kati yao walibambikiziwa kesi za uhaini, wakafikishwa mahakamani na kisha kufungwa na serikali.

Kati yao walikuwa Bibi Titi ambaye alipigania uhuru pamoja ana Nyerere na alikuwa kiongozi wa jumuia ya kina mama. Alikuwepo pia Michael Kamaliza ambaye alikuwa mwanaharakati wa chama cha wafanyakazi, mwanachama wa TANU na waziri.

Wengine ni pamoja na Gray Mattaka, John ana Eliya Chipaka na Prisca Chiombola. Kambona alituhumiwa kuwa kiongozi wa wahaini wakati akiwa London na alihukumiwa bila kuwapo. Watuhumiwa hatimaye walikata rufaa katika mahakama kuu ya Afrika Mashariki na wakaachiwa huru.

Hata hivyo, baadae walikamatwa na serikali na kufungwa tena. Kambona alituhumiwa kuwa aliiba pesa nyingi sana zikiwa ni mali ya umma, kitu ambacho Kambona alikataa katika taarifa yake na waandishi wa habari Septemba 6 huko London 1967.

Tuhuma hizo zilisema kuwa ‘’ Kambona amekutwa na pesa nyingi sana kama karanga alipopekuliwa katika Uwanja wa ndege Embakasi Nairobi’’ Hata hivyo Kambona katika taarifa yake kwa waandishi wa habari alikanusha kuhusika na tuhuma hizi na badala yake akaipa serikali ya Tanzania kuiomba serikali ya Kenya kutoa ukweli juu ya jambo hilo- jambo halikufanyika.

Akiwa Londoni Kambona aliishi maisha ya shida na dhiki. Katika mwaka 1982 ndugu zake Kambona na Otini Kambona walifunguliwa kutoka kizuizini baada ya juhudi za waziri mkuu wa New Zealand Robert Muldoon. Katika mwaka 1990 Kambona akiwa na matumaini makubwa ya mabadiliko ya kisiasa katika Tanzania hususani mabadiliko ya demokrasia, aliunda chama kiitwacho Tanzania Democratic Alliance.

Wakati vyama vingi vilipoanzishwa Tanzania 1992 Kambona aliomba kurudi Tanzania. Serikali ya Tanzania ilimkatalia katakata na kudai kuwa Kambona hakuwa Mtanzania. Kambona badala yake aliomba Serikali ya Uingereza kumpa pasi ya kusafiria kurudi Tanzania. Hata hivyo Serikali ya Tanzania ilitamka kwamba pamoja na kupata pasi hiyo itamweka ndani pindi atakapoingia Tanzania.

Pamoja na msimamo huo wa Serikali, Kambona alitua kwenye ardhi ya Tanzania tarehe 5 september 1992. Hakuna mamlaka iliyomkamata bwana Kambona bali alipewa miezi mitatu awe amekamilisha utata wa uraia wake. Baada ya kurudi, Tanzania aliona kuwa harakati za kuelekea kwenye demokrasia ya kweli zilikuwa zikienda kwa mwendo wa kinyonga.

Hata hivyo Kambona hakuweza kujihusisha kwa kiasi kikubwa na siasa kutokana na matatizo ya kiafya hususani shinikizo la damu. Hatimaye Oscar Kambona alifariki akiwa katika matibabu mjini London mwezi Juni 1997.

Mdogo wake Otini Kambona naye alifariki katika kipindi hichohicho kutokana na magonjwa ya moyo. Wote wawili walizikwa Tanzania, na serikali ya Tanzania iligharimia gharama zote za usafirishaji miili ya marehemu ndugu hawa.

Oscar Kambona ameacha mke na watoto wawili. Mtoto wao wa kwanza Mosi Kambona aliuawa mjini London katika mazingira ya kutatanisha. Roho ya Oscar Kambona na ndugu na jamaa wote waliotangulia MWENYEZI MUNGU aziweke pema peponi, Amin.

Kumsoma bonyeza hapa
Inasisimua

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Mkumbo hata wewe asaiv mawazo yako yapo kifungoni, najua hata sasa una mapenzi na rais magufuli na ana madhaifu makubwa Mara mia afadhali madhaifu ya nyerere uliyosema hapa, lkn sababu ya keki ya taifa unayopata kwa sasa sidhani kama utaona dhaifu hata moja la magufuli, nimefanya hivi ili kukumbusha kuwa koti la kawawa ndo umelivaa wewe muda huu.
We jamaa sio mtu mzuri yaani unawakumbushia wenzako mambo ya nyuma
 
Nyerere alikuwa anakopi vitu tokea USSR ama uchina analeta hapa nyumbani.hata alama ya nyundo ,jembe aama mundo pia mwenge amekopi tokea USSR.aliyekaa Russia ataleta shuhuda nzuri nadhani. Namie Nina uhakika mana nimeishi huko miaka miwili so Nina uhakika nachoongea
Mkuu Nyani,

Heshima mbele, I like kila ulichosema so far kwenye hii topic, now ngoja tujairbu kuchambua kidogo:-

1. After the mutiny, differences between Kambona and Nyerere began to appear. Nyerere wanted to introduce a one party system into Tanzania to strengthen state security. Kambona argued against the move claiming that it would inhibit peoples freedom and progress towards democracy. However, Kambona was defeated in parliament. He refused to sign the bill.

I mean right here, ndipo mambo yetu yalipoanza kwenda mrama as a nation, na ndio ninayoyasema kila siku, kumbuka kuwa to this point tulikuwa on the right track, kuaniza uchumi, uongozi, mpaka siasa, now look at the turn of events ambazo eventually, ndio zilizotufikisha tulipo!

2. In 1967 after a trip to China in 1965, Nyerere impressed with Maos style of communism, wanted to adopt the same system under the guise of Ujamaa. The main doctrine behind Ujamaa was the relocation of peasants into village communes and the nationalization of all industries and property. Kambona did not agree with the policies, arguing that they would rather increase poverty and state control over the people. He resigned from the Government and the party and later with his family fled to neighbouring Kenya and then UK were he was granted political asylum.

Tizama kiongozi aliyekuwa na uwezo wa kuona mbali, exactly his argument then ndio hasa yalipolalia matatizo yetu, kumbe walikuwepo wenye akili ya kuona mbele, I mean this is very interesting story, pumba na mchele uko clear upande gani?

3. Immediately thereafter, Kambonas properties were confiscated. His two brothers Mattiya and Ottini Kambona were detained without trial and put in prison for over ten years. Other family members were harassed and detained. Some were falsely accused of plotting to overthrow the Tanzanian Government and were tried and imprisoned by the Government.

Wooow! Yaaani kweli haya mambo yalifanyika bongo under Mwalimu?

4. Most famous of these were Bibi Titi who fought alongside Nyerere in the independence movement and was head of the womans wing and also Michael Kamaliza, the former trade unionist and TANU member and government Minister. Other family members included Gray Mattaka, John and Elia Chipaka and Prisca Chiombola. Kambona was also accused of being the ring leader of the plotters while in London and was tried in absentia. The accused finally appealed to the East African High Court and were acquitted. Though they were later rounded up by the Tanzanian government and thrown into jail again.

5. Kambona was also accused of stealing millions of public funds,

6. Kambona challenged the Tanzanian government to request the Kenyan authorities to substantiate the allegations which they never did.

7. In London Kambona led a tough life in exile under considerable financial constraints. However in 1982, his two brothers Mattiya and Otini Kambona were eventually released from detention after the intervention of New Zealand Prime Minister Robert Muldoon.


8. On returning to Tanzania Kambona found that the progress towards democracy was disappointingly slow.


9. His eldest son Mosi Kambona was murdered in London in unexplained circumstances.

Sasa wakuu wangu bado kuna maswali kwamba kwa nini as a nation tupo hapa tulipo? Maana kwanga naona majibu yako clear hapa, kama kuna story ya upande wa pili tungekuwa tumeshaisikia, na pia tuliambiwa Kambona amekimbia Azimio La Arusha, lakini hapa ukweli unajionyesha wazi, au labda tusubiri na upande wa pili ulete yao pia, otherwise I am convinced kuwa huu ndio ukweli wenyewe wa kwa nini taifa letu limekwama!

Ahsante Mtoa Mada, yaanai you made my day!
 
Ni sawa Kawawa alikuwa sahihi hatuna shida na hilo!

Lakini huyu Kambona alishiriki kutunga Sera na Misingi ya Azimio la Arusha,wazi wazi ndani ya jopo la Mwalimu Nyerere! wakakubaliana kwa Umoja jinsi ya kulitekeleza! kwa nini baadaye aligeuka na kulikana? ili kutekeleza kile alicho shiriki kukianzisha?

ni wazi alikuwa ni tatizo la ki-Juda mbele ya macho ya wenye akili hata km huyo angekuwa Rais wetu na kuleta huo Ubepari, angeongoza vibaya, na tungekuwa pabaya zaidi kuliko Ubepari wa mpito tulio nao leo!

Sisi Tanzania siyo maskini hata kidogo sema wewe Mungu amekupiga Kofi tu, Maghorofa haya yoote? Afya bure, Nyumba Bure NH, Nyumba za Biafra kila Mkoa, Barabara lami mpaka chooni, Elimu yetu Bure kwa miaka 50 tu ya Uhuru tuko hapa pazauri,

Taifa la watu tulioathiriwa na Utumwa, Ukoloni, Vita za mara kwa mara za Majirani zetu, lkn bado tuko ngangari, unakufuru bure mwishowe Mungu atuadhibu kwa domo lako! kukosa shkrani! tembea USA uone lundo la Maskini, Lesotho, Senegal ni utachoka wewe! haya maneno ume-copy ya watu vitabuni! sema ya kwako ya dhati moyoni.
Kuna muda unaweza kushiriki katka maamuzi fulan ila utakapokaa na kutafakari kwa kina unaweza ona kabisa kuwa ulikosea. Kubadili mwelekeo juu ya kutafuta usahihi wa kile ulichokiazimia kimakosa awali ndo ukomavu wa fikra. Kushiriki katka kuandaa azimio la Arusha na kisha kuja kulipinga sioni kama ni shida ikiwa aliliona kwa jicho la tatu kuwa n janga la nchi kwa siku za usoni. Haya maisha yanahitaji mnyumbuliko wa kiwakati, hivyo kuna haja ya kurudufu maamuzi na misimamo yetu kila mara kama inaendana na wakati na mivumo ya pepo za ulimwengu. Hivyo naendelea kusisitiza kuwa Kambona alikuwa Big Brain.

Kuhusu umaskini/na ufukara nmeungumza kwa istilah pana ya kinchi na sio kwa kupoint vitu vichache kama ulivyofanya mwanabodi. Tanzania ina rasilimali nyingi ila bado ni Nchi ya Taifa Fukara. Ni ukweli ulio dhahir kuwa asilimia kubwa ya watu wa nchi hii n mafukara. Serikali ina bajet yenye nakisi kubwa. Nchi ina reserve ndogo ya Dhahabu safi katka mabenk ya kiulimwengu, fedha yetu n yenye thamani ndogo, urari wetu kibiashara n hasi (Export vs Import). Hizi zote n miongon mwa alama za nchi maskini. Hayo maghorofa na miundombinu unayosema ww, yamemuondolea shida na dhiki yule mkulima wabjembe la mkono mwenye kutegemea hisan ya hali ya hewa?

Kawawa na Nyerere wote walikuwa failures katka maamuzi mengi yaliyohusu mustakabali wa nchi. Jaribu kutafuta ngano za Sir George Kahama kuhusu usuhuba wake yeye na Mwalimu Nyerere husuan yey Kahama akiwa anasoma England, anasema kabisa kuwa Nyerere alikuwa ana damu ya kichifu hivyo hakuwa na uvumilivu wa kupingwa juu ya kile alichokiamin licha ya kutajwa kuwa na uwezo mkubwa wa kusikiliza hoja. Wengi wa wafuasi wake walikuwa n wale wa "Zidumu Fikra za Mwenyekit".

Kitendo cha Mkapa kutogusia battle ya Nyerere vs Kambona kweny kitabu chake inaweza kutupa tafsir ya ukweli unaofichwa ambao kama angeamua kuuweka wazi basi huenda baadhi ya watu wangehis kuwa Mwalimu kafanyiwa dharau na Hayati Ben Mkapa.

Tusome na kudadisi yaliyo nyuma ya pazia yasiosemwa wala kuandikwa kuhusu Mwalimu Nyerere.
 
Mengi yamesemwa kuhusu Mzee wetu huyu na sisi tuliokuwa shuleni wakati ule tulilishwa kile ambacho naamini ni sumu. Wakubwa tuelimisheni ukweli kuhusu Mzee huyu.

View attachment 1371792
Oscar Kambona




Natumaini waandishi wa historia ya tanzania watampa nafasi yake kwa mchango mkubwa aliyoutoa.
RIP Mzee Kambona


Oscar Salathiel Kambona, alitaka kumpindua Nyerere kwa kushirikiana na wapiganaji wa Umkhonto.
[/h]

=======


Kichakaa man, ameandika;

Marehemu Oscar Kambona alizaliwa mwaka 1925 katika kijiji cha Kwambe kilichopo mwambao mwa ziwa Nyasa, karibu na Mbamba-bay, wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma. Alikuwa mtoto wa marehemu Rev. David Kambona na Bibi Miriam Kambona.

Rev. Kambona alikuwa ni miongoni mwa waafrika wa kwanza kupata upadre katika kanisa la Anglikana la Tanganyika. Wakati Oscar Kambona akiwa mdogo, baba yake alikuwa akimweleza kuhusu ndoto zake juu ya uhuru wa nchi yake, hivyo Oscar alikuwa akiwa na hamu sana ya kuitumikia nchi yake.

Oscar alipata elimu ya msingi nyumbani kwao, chini ya mwembe (ambao bado upo), katika kijiji chao kwa kuwatumia wazazi wake wote wawili na mjomba wake, ambao wote walikuwa walimu. Baada ya hapo alipelekwa shule ya kati ya Mt. Barnabas, Liuli, na baadaye shule ya Sekondari ya Alliance, ambako alilipiwa ada na Askofu mzungu wa Anglikana kwa vile baba yake hakuweza kumudu kulipa ada ya paundi 30 kwa mwaka.

Oscar alikuwa akisimulia jinsi alivyoweza kumshawishi Askofu huyo amlipie ada kwa kusema sala ya Baba yetu kwa kizungu. Oscar alichaguliwa kwenda ‘Tabora Boy’s Senior Government School’, ambako alionana na Julius Nyerere kwa mara ya kwanza; wakati huo Nyerere alikuwa anafundisha katika shule ya kikatoliki.

Baada ya kumaliza masomo ya sekondari alienda katika shule yake iliyopita ya Alliance kama mwalimu na baadae alichaguliwa kuwa ‘Schoolmaster’. Ilikuwa katika mkutano wa kitaifa wa walimu, mnamo mwaka 1954, ambapo Kambona na Nyerere walikutana tena.

Kambona alikuwa tayari kukitumikia chama cha TANU ambacho kilikuwa kimeanzishwa muda si mrefu, lakini Nyerere akasema wasingeweza kumwajiri kwa vile chama kilikuwa hakina fedha.

Kambona akasema chama hakikuwa na fedha kwa vile hakikuwa na ‘organising secretary, na ndipo alipoamua kufanya kazi hiyo ili kujenga chama, bila ya malipo’. Aliishi kwa kutegemea akiba aliyojitunzia kwa kufanya kazi miezi 6.

Katika kipindi hiki Kambona alisafiri sehemu mbalimbali za nchi na kuonana na machifu na wazee wa vijiji ili kusajili wanachama. Katika miezi 6 alifanikiwa kusajili wanachama 10,000, na hadi kufikia mwaka mmoja alikuwa amepata wanachama hai 100,000. Kambona alitumia michango aliyopata kufungua akaunti ya kwanza ya TANU.

alienda Butiama kumshawishi Nyerere achukuwe uongozi wa chama moja kwa moja. Baada ya miaka mitatu Kambona aliamua kwenda kusomea sheria katika Chuo cha Middle Temple, nchini Uingereza mwaka 1957 kwa ufadhili wa Gavana.

Akiwa London Kambona alikuwa kiongozi wa chama cha wanafunzi wa Tanganyika na Mwenyekiti wa tawi la TANU la London. Ni wakati huo ambapo Kambona alipata fursa ya kukutana kwa mara ya kwanza na watu mashuhuri kama George Padmore, mwanaharakati wa umoja wa Afrika, ambaye alimshawishi ahudhurie mkutano wa mwaka 1958 wa waafrika wote(All Africa’s Peoples Conference), uliofanyika nchini Ghana muda mfupi baada ya kupata Uhuru.

Akiwa Ghana Kambona alipata nafasi ya kukutana na mwanaharakati mwingine maarufu wa siasa za Afrikla, Kwame Nkurumah. Akiwa uingereza Kambona alikuwa mwaafrika wa kwanza kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili katika idhaa ya kiswahili ya BBC.

Aliporudi nchini Tanganyika, mwaka 1959, TANU ilikuwa imeshaweka bayana madai yake ya kupewa serikali ya madaraka, vinginevyo TANU ilikuwa tayari kuanzisha mapambano kama ilivyokuwa kwa Mau Mau ya Kenya. Wakiwa London wakisubiri kupewa madaraka ya ndani, Nyerere na Kambona walijadili hatua mbalimbali ambazo zingechukuliwa ili kuepuka kutoweka kwa amani.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Londoni 1991, Kambona alikumbuka matukio kama hivi, ‘’Bwana Nyerere alikuwa akiishi nami katika chumba kidogo nilichopewa chuoni.

Tulijadiliana ni namna gani angeweza kurudi nyumani na kuonana na wafuasi wake bila kupewa serikali ya madaraka. Baadae nilifanikiwa kumshauri kuwa wakati atapozungumza na vyombo vya habari katika the East African Arch aseme kuwa walowezi wa kizungu ambao wapo Tanganyika wana hekima zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki.

Alikubali kusema hivyo endapo na yeye Kambona angekubali kukatisha masomo yake ya sheria huko London na kurudi Tanganyika ili ampe nguvu na kumuunga mkono katika kikao cha kamati kuu ya TANU wakati akitetea tamko lake la wenye hekima zaidi.

Katika uchaguzi wa kwanza TANU ilishinda viti vyote isipokuwa kimoja. TANU iliunda serikali ya mambo ya ndani chini ya Nyerere ambaye alikuwa Waziri kiongozi wa kwanza.

Na katika harakati hizo za matayarisho ya serikali ya ndani, Kambona alimwoa Flora Moriyo wakati wakiwa kwenye msafara wa harakati za kukamilisha matayarisho ya uhuru na serikali ya Uingereza. Harusi ilifungwa katika kanisa la Mt. Paul, London, na Nyerere ndiye alikuwa msimamizi. Kambona aliteuliwa kuwa waziri wa Elimu.

Baadaye alishika nyadhifa za waziri wa Mambo ya Ndani, Mambo ya nchi za nje na Ulinzi na Tawala za Mikoa. Pia alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika na mwenyekiti wa utayarishaji wa AOU charter.

Mwaka 1964, Kambona alifanya kazi kubwa katika kuunganisha Zanzibar na Tanganyika, akiwa pamoja na Raisi Nyerere, Raisi Karume na Waziri Kiongizi Hanga. Hii ilikuwa ni baada ya mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati wa wanajeshi wa kikosi cha Calito walipoasi mwaka 1964 Kambona alikuwa msuluhishi mkuu kati ya serikali na wanajeshi hao. Nyerere na Kawawa walienda mafichoni Kigamboni. Baada ya siku tatu za majadiliano Kambona aliafiki kuongeza kasi ya kuwawezesha waafrika kushika hatamu jeshini.

Katika mahojiano na gazeti la Daily Telegraph la London Kambona alisema, ‘baada ya kuwatuliza wanajeshi nilikwenda kuwatafuta viongozi wengine na kuwarudisha mjini kwa kutumia Land Rover yangu’. Hatimaye maasi hayo yalidhibitiwa kabisa na majeshi ya Uingereza na Nyerere alimsifu Kambona bushara na uaminifu wake.

Tofauti kati ya Nyerere na Kambona zilianza kujitokeza baada ya maasi ya wanajeshi. Nyerere alitaka kuanzisha mfumo wa chama kimoja nchini ili kuimarisha usalama. Kambona alipinga hoja hiyo kwa maelezo kwamba mfumo huo ungezorotesha uhuru wa watu na maendeleo ya demokrasia.

Hata hivyo, Kambona alishindwa bungeni; alikataa kusaini muswada (bill). Mwaka 1967, baada ya safari ya China ya mwaka 1965, Nyerere akiwa amependezwa na mfumo wa kikomonist wa Mao, alitaka kuanzisha mfumo kama huo kwa jina la ujamaa.

Dhana ya msingi ya mfumo wa ujamaa ilikuwa ni kuwahamishia watu katika vijiji vya ujamaa na kutaifisha viwanda ana mali. Kambona hakukubaliana na utaratibu huo kwa maelezo kwamba ungeongeza umaskini na udhibiti wa serikali kwa watu.

Alijiuzulu kutoka katika serikali na Chama na hatimaye yeye na familia yake walikimbilia Kenya na kisha Uingereza ambako walipatiwa uhifadhi wa kisiasa. Mara baada ya kuondoka mali za Kambona zilichukuliwa.

Ndugu zake wawili, waliwekwa kizuizini bila ya kufikishwa mahakamani na kufungwa kwa zaidi ya miaka kumi. Wanafamilia wengine walinyanyaswa na kuwekwa kizuizini. Wengine kati yao walibambikiziwa kesi za uhaini, wakafikishwa mahakamani na kisha kufungwa na serikali.

Kati yao walikuwa Bibi Titi ambaye alipigania uhuru pamoja ana Nyerere na alikuwa kiongozi wa jumuia ya kina mama. Alikuwepo pia Michael Kamaliza ambaye alikuwa mwanaharakati wa chama cha wafanyakazi, mwanachama wa TANU na waziri.

Wengine ni pamoja na Gray Mattaka, John ana Eliya Chipaka na Prisca Chiombola. Kambona alituhumiwa kuwa kiongozi wa wahaini wakati akiwa London na alihukumiwa bila kuwapo. Watuhumiwa hatimaye walikata rufaa katika mahakama kuu ya Afrika Mashariki na wakaachiwa huru.

Hata hivyo, baadae walikamatwa na serikali na kufungwa tena. Kambona alituhumiwa kuwa aliiba pesa nyingi sana zikiwa ni mali ya umma, kitu ambacho Kambona alikataa katika taarifa yake na waandishi wa habari Septemba 6 huko London 1967.

Tuhuma hizo zilisema kuwa ‘’ Kambona amekutwa na pesa nyingi sana kama karanga alipopekuliwa katika Uwanja wa ndege Embakasi Nairobi’’ Hata hivyo Kambona katika taarifa yake kwa waandishi wa habari alikanusha kuhusika na tuhuma hizi na badala yake akaipa serikali ya Tanzania kuiomba serikali ya Kenya kutoa ukweli juu ya jambo hilo- jambo halikufanyika.

Akiwa Londoni Kambona aliishi maisha ya shida na dhiki. Katika mwaka 1982 ndugu zake Kambona na Otini Kambona walifunguliwa kutoka kizuizini baada ya juhudi za waziri mkuu wa New Zealand Robert Muldoon. Katika mwaka 1990 Kambona akiwa na matumaini makubwa ya mabadiliko ya kisiasa katika Tanzania hususani mabadiliko ya demokrasia, aliunda chama kiitwacho Tanzania Democratic Alliance.

Wakati vyama vingi vilipoanzishwa Tanzania 1992 Kambona aliomba kurudi Tanzania. Serikali ya Tanzania ilimkatalia katakata na kudai kuwa Kambona hakuwa Mtanzania. Kambona badala yake aliomba Serikali ya Uingereza kumpa pasi ya kusafiria kurudi Tanzania. Hata hivyo Serikali ya Tanzania ilitamka kwamba pamoja na kupata pasi hiyo itamweka ndani pindi atakapoingia Tanzania.

Pamoja na msimamo huo wa Serikali, Kambona alitua kwenye ardhi ya Tanzania tarehe 5 september 1992. Hakuna mamlaka iliyomkamata bwana Kambona bali alipewa miezi mitatu awe amekamilisha utata wa uraia wake. Baada ya kurudi, Tanzania aliona kuwa harakati za kuelekea kwenye demokrasia ya kweli zilikuwa zikienda kwa mwendo wa kinyonga.

Hata hivyo Kambona hakuweza kujihusisha kwa kiasi kikubwa na siasa kutokana na matatizo ya kiafya hususani shinikizo la damu. Hatimaye Oscar Kambona alifariki akiwa katika matibabu mjini London mwezi Juni 1997.

Mdogo wake Otini Kambona naye alifariki katika kipindi hichohicho kutokana na magonjwa ya moyo. Wote wawili walizikwa Tanzania, na serikali ya Tanzania iligharimia gharama zote za usafirishaji miili ya marehemu ndugu hawa.

Oscar Kambona ameacha mke na watoto wawili. Mtoto wao wa kwanza Mosi Kambona aliuawa mjini London katika mazingira ya kutatanisha. Roho ya Oscar Kambona na ndugu na jamaa wote waliotangulia MWENYEZI MUNGU aziweke pema peponi, Amin.

Kumsoma bonyeza hapa
Hauwezi kuwa na boga ambalo ua lake si la boga! Kambona na Kawawa walikuwa ni ndugu, wajomba. Kutokana na udugu huu serikali ililazimika kumkubali kimyakimya kuwa mtanzania badala ya mmalawi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom