Ukweli ni kwamba Lissu na Membe wana ushawishi kuliko watanzania wengine wanaotaka Kugombea lakin ...

Ukweli CCM ilijijengea Heshima zamani, Ila kwa sasa mambo yanaenda ndivyo sivyo,

Kwasasa Ndani ya CCM kuna mvurugano mkubwa wa hali ya Juu,

Pamoja na Kugawanyika vipande ndani ya Chama kuna viongozi wakuu wa zamani wamekuwa kimya bila kutaja pande zao,

Leo hii CCM imegawanyika pande 3

1.Wale Pro Magufuli bila kujali anakosea au anapatia kwa afanyayo,

2.Against Magufuli
Hawa hawana muda hata wa kuchambua na kujua ama Magufuli anafanyayo

3.Kuna wale ambao ni wachambuzi makini

Lakin asilimia kubwa wanamsaport Membe

Upinzani Wanaweza kupima je waende na Membe au Lissu,

Wengi wanaompenda Lissu wanahofu je anaweza akarudi Tanzania bila kubambikiwa kesi?

Wengine wanaona Bora Membe ambaye anayaishi maisha ya Kutishiwa ndani ya Tanzania Kuliko Lissu ambaye anahofia usalama wa Maisha yake ndani ya Tanzania, itamnyima nafasi ya kucheza Karata zake vyema,
Shehe upo?
 
Leo hii ni 8.8.2020 mh Lissu amesha chukua form ya kumwingiza ikulu mara baada ya uchaguzi wa October.
Membe anatajwatajwa sana.hii inaashiria Lissu kwisha habari yake.
Lakini mwisho wa siku Membe atarudi CCM piga ua.
photo%20266%2012-18-0.jpeg
 
Hakuna mti wa kukubali upuuzi kama huo cdm
Suala la Membe lipo tofauti na makada wengine waliokimbilia upinzani. Wakati yeye amefutwa uanachama wake na KK ya Halmashauri Kuu ya chama chake, wengine walihama kwa makusudi ili kutafuta fursa iliyokuwepo upinzani kwa wakati huo.

Mimi nashauri, kwa kuwa CDM ktk uchaguzi uliopita kiliungwa mkono na vyama vingine chini ya mwamvuli wa UKAWA. Chama hiki kione vyema kama inafaa ya kwamba, endapo itathibitika mazingira na upepo wa kisiasa utaonyesha kukipa nafasi chama cha ACT Wazalendo chini ya uwepo wa Membe kama mpeperusha bendera, na pia pasipo kujali kama chama hiki kipya kinakwenda kuchukua nafasi yake ya KUB bungeni.

Naamini CDM kimeshakuwa chama maarufu, chenye nguvu kubwa na kuungwa mkono kwa dhati na wananchi wengi wenye kupenda mabadiliko ya kweli nchini. Chama hiki tayari kimeshakuwa "agent of change" ya mabadiliko. Ukweli wa jambo ili unakifanya chama tawala kutahayari.

Basi, kwa kuwa CCM imeshindwa kupambana kihalali na CDM kwa hoja mujarabu za makada wao mahiri ama ubunifu wa sera nzuri ambazo CCM pasipo hata na aibu uzi "copy & paste" na kuanza kuzitekeleza bila hata ya kutoa "application' kwa wamiliki wake.
Kwa hiyo basi ktk mazingira ya sasa ya kuzidi kuandamwa na kufanyiwa visa na uhalifu mwingi na CCM kupitia mbeleko ya vyombo vya dola, basi wanapaswa kuwa na Plan B, nayo si nyingine bali kiendeleze mapambano kupitia "synergy" ya kuunganisha nguvu na mshirika mpya ili adui ashambuliwe kutoka pande mbalimbali za kimkakati, kitu ambacho CCM haikutarajia kabisa kama kitatokea ktk uwanja wa mapambano.
 
Kamwe haitatokea ndani ya cdm, na kamq watarogwa wakafanya ujinga kama huo binafsi ni bora nikaishi maisha yasiyo na stress ya kutokuwa na chama cha siasa.
Brother kama umekula hela ya Membe tunaomba umrudishie. Ya Lowassa yanatutosha, ni bora tupigie kura picha ya Lissu akiwa gerezani au popote pale, kuliko kumpigia kura Membe.
 
Labda nyumbani kwenu koromitdje
Wana ushawishi mkubwa kwa waliokuwa na chuki binafsi kwa JPM. Mmemsingizia mengi lakini yeye anafanya kazi ambayo ametumwa na Watanzania. JPM atashinda tena kwa kishindo.
 
Kama mmesha vuta mkwanja kwa Membe rudisheni fedha zake, hapa hakuna mtu atawaunga mkono kumpigia debe Membe.

Yaliyo tupata kupitia kwa lowasa bado yapo rohoni mwetu, sisi ni lisau na cdm hao wengine tupa kuleeeee
Mkuu Tindo, hili ni jukwaa huru lenye kuchambua hoja mbalimbali za kisiasa. Sidhani kama ni vyema kumhukumu mtoa hoja kuwa amenunulika kwa vipande vya rupia pale inapotokea kuwa anapendelea mlengo ama mpeperusha bendera fulani wa chama cha kisiasa.

Ndiyo! Sote tunatambua, nyakati kama hizi za uchaguzi watu hufungamana na kambi fulani za kisiasa, ndani ama nje ya vyama vya kisiasa. Nashauri ya kuwa, kwa yule ambaye tunamuunga ama kumpigia debe, isiwe sababu kuwa yeye ni "perfect" kwa kila mtu, kitu ambacho kiwafanye wengine wasiweze kuongelea watu wao ambao wanona kuwa wanafaa.
 
Upotolo mtupu
Pole britanika naona sasa uwezo wa kufikili umepungua, vi vema sasa ukajiunge na akina sharifu majini huenda huko utapata ndoto danganyifu kuliko sasa ukiwa mzima.
Hao Watu wako wana ajenda tatu tu nazo ni
1 uhuru wa kutukana viongozi
2 demokrasia
3 mahusiano ya kimataifa
Ya nyongeza ambayo huenda wakaitumia ni kazi na bata,
Sasa hizo tatu za kwanza zipo kwa muda mrefu lakini tanzania bado masikini ni wengi sana,
kwa hiyo hazina tija.
Ukisema mahusiano ya kimataifa yalikuwa yana wanufaisha akina membe kwa kuwa wao walipata posho za kwenda huko lakini mkulima au mfanyakazi hakuwahi kunufaika na mahusiano hayo maana pesa zote walizokuwa wanapata mikopo wanagawana wenyewe.
Na hiyo demokrasia haikuwahi kumsaidia mtu wa chini akipata matatizo
Ni nguvu yake ambayo ingeweza kumsaidia lakini sio demokrasia.
 
Suala la Membe lipo tofauti na makada wengine waliokimbilia upinzani. Wakati yeye amefutwa uanachama wake na KK ya Halmashauri Kuu ya chama chake, wengine walihama kwa makusudi ili kutafuta fursa iliyokuwepo upinzani kwa wakati huo.

Mimi nashauri, kwa kuwa CDM ktk uchaguzi uliopita kiliungwa mkono na vyama vingine chini ya mwamvuli wa UKAWA. Chama hiki kione vyema kama inafaa ya kwamba, endapo itathibitika mazingira na upepo wa kisiasa utaonyesha kukipa nafasi chama cha ACT Wazalendo chini ya uwepo wa Membe kama mpeperusha bendera, na pia pasipo kujali kama chama hiki kipya kinakwenda kuchukua nafasi yake ya KUB bungeni.

Naamini CDM kimeshakuwa chama maarufu, chenye nguvu kubwa na kuungwa mkono kwa dhati na wananchi wengi wenye kupenda mabadiliko ya kweli nchini. Chama hiki tayari kimeshakuwa "agent of change" ya mabadiliko. Ukweli wa jambo ili unakifanya chama tawala kutahayari.

Basi, kwa kuwa CCM imeshindwa kupambana kihalali na CDM kwa hoja mujarabu za makada wao mahiri ama ubunifu wa sera nzuri ambazo CCM pasipo hata na aibu uzi "copy & paste" na kuanza kuzitekeleza bila hata ya kutoa "application' kwa wamiliki wake.
Kwa hiyo basi ktk mazingira ya sasa ya kuzidi kuandamwa na kufanyiwa visa na uhalifu mwingi na CCM kupitia mbeleko ya vyombo vya dola, basi wanapaswa kuwa na Plan B, nayo si nyingine bali kiendeleze mapambano kupitia "synergy" ya kuunganisha nguvu na mshirika mpya ili adui ashambuliwe kutoka pande mbalimbali za kimkakati, kitu ambacho CCM haikutarajia kabisa kama kitatokea ktk uwanja wa mapambano.
Zitto hakusapoti Ukawa,kila mtu ashinde mechi zake.
 
Pascal Mayalla isingekuwa Jamaa kuwa black mailed airport angetoa mambo mengi Sema pesa zake na Yule Mshika pesa wake Eligiva yakaisha hivo
 
Back
Top Bottom