Sio mfumo dume, sisi tuliokulia vijijini tulipewa mafunzo wakati wa jando kwamba si jambo jema kufunua chakula kilichoandaliwa na mwingine hata akiwa mkeo.
Bravo Hmaster.Avatar yako imetulia,mambo ya wapi hiyo?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sio mfumo dume, sisi tuliokulia vijijini tulipewa mafunzo wakati wa jando kwamba si jambo jema kufunua chakula kilichoandaliwa na mwingine hata akiwa mkeo.
kama wamjua mkeo ni mtu wa wivu bora umwambie uongo unaofanana na ukweli, kwa case yako hapo usingemwabia unampeleka mwanamke tegeta bora ungemdanganya kuna mzigo unaenda chukua/peleka tegeta, dar inaeleweka kwa foleni so angekuelewa. we mtu mzima unatunga uongo ambao ataelewa utakaokupeleka tegeta!
Juzi nilikuwa maeneo ya Ubungo ambapo nilikutana na dada furani akiwa na watoto wa2 na mizigo kadhaa na baada ya kusalimiana aliniomba nauli ya daladala ili aende Tegeta kwa dada yake kwani alikuwa ameibiwa pochi yake ambayo ilikuwa na pesa akiwa safarini kutokea Songea. Mimi kwa vile nilikuwa na gari na kwa namna alivyoonyesha huzuni niliona bora nimchukue tu kwenye gari yangu hadi Tegeta kisha nikarudi hadi Magomeni ninapoishi. Kwa sababu ya foleni nyingi na muda ulipita sana kabla ya kurudi home, hata hivyo my wife wangu nilimweleza kila kitu lakini badala ya kuona umuhimu wa mimi kumsaidia mwanamke mwenzake yeye alikwenda mbali zaidi na aliamua kukata simu na hakupatikana hadi nafika home. Baada ya kufika nikamkuta tayari yupo kitandani akiwa na nguo zake zote, eti ndo keshakasirika na kuamua kulala hiyo saa tatu na wakati huwa tunalala hata saa 5 kila siku. Nilipojaribu kumwamsha ili aniandalie chakula alinijibu niende kula kwa malaya niliyemsindikiza Tegeta. Nilijitahidi kumwelewesha lakini ilishindikana. Nikajiandalia chakula mwenyewe, nikaoga na kisha kulala kwa maana kwa hali hiyo hata kumchombeza sikuweza. Sasa swali ni je Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa, au vyote? Wenye experince na mambo haya waweke hapa maana sasa najiandaa kuwa mwongo kwa vile ukweli umenitokea puani. Na kama wanawake humu jf watueleze wenyewe kipi wanataka kutoka kwetu kati ya hivyo vitatu ili wawe na amani. Nawasilisha!
Heshima kwako Hmaster,kiongozi nadhani hapo kwako kuna tatizo labda uniambie hiyo ndoa yako ina week ya pili hivyo umjui vilivyo mkeo,mi nadhani majibu au sababu ambazo ulipaswa kumpa mwenza wako ni zile zinazojenga kutokana na unavyomuelewa mwenza wako huyo,kwa mfano kama unatambua ni mwenye wivu kupindukia juu yako ungejua njia mbadala ya kumwambia kilichojiri kuliko kumweleza ukweli ambao kwake ni uongo.Hivyo basi kusema ukweli au uongo katika maisha ya ndoa au ya mahusiano yote ni sawa iwapo lengo ni kujenga.Mfano mimi naweza kudanganya leo kwa lengo la kujitetea kama mwenza wangu hayupo kwenye mood,then baada ya siku kadhaa tukiwa wote tupo kwenye mood naweza kumwambia,"unajua dear last week ilibidi nikudanganye maanake ulikuwa umekasirika sana lakini ukweli ilikuwa hivi............" i mean umedanyanya then umeungama uwongo wako hivyo inakuweka huru tena....Mjue mwenza wako kiongozi japo kwa kiasi kidogo tu.Juzi nilikuwa maeneo ya Ubungo ambapo nilikutana na dada furani akiwa na watoto wa2 na mizigo kadhaa na baada ya kusalimiana aliniomba nauli ya daladala ili aende Tegeta kwa dada yake kwani alikuwa ameibiwa pochi yake ambayo ilikuwa na pesa akiwa safarini kutokea Songea. Mimi kwa vile nilikuwa na gari na kwa namna alivyoonyesha huzuni niliona bora nimchukue tu kwenye gari yangu hadi Tegeta kisha nikarudi hadi Magomeni ninapoishi. Kwa sababu ya foleni nyingi na muda ulipita sana kabla ya kurudi home, hata hivyo my wife wangu nilimweleza kila kitu lakini badala ya kuona umuhimu wa mimi kumsaidia mwanamke mwenzake yeye alikwenda mbali zaidi na aliamua kukata simu na hakupatikana hadi nafika home. Baada ya kufika nikamkuta tayari yupo kitandani akiwa na nguo zake zote, eti ndo keshakasirika na kuamua kulala hiyo saa tatu na wakati huwa tunalala hata saa 5 kila siku. Nilipojaribu kumwamsha ili aniandalie chakula alinijibu niende kula kwa malaya niliyemsindikiza Tegeta. Nilijitahidi kumwelewesha lakini ilishindikana. Nikajiandalia chakula mwenyewe, nikaoga na kisha kulala kwa maana kwa hali hiyo hata kumchombeza sikuweza. Sasa swali ni je Ukweli na Uwongo upi hudumisha ndoa, au vyote? Wenye experince na mambo haya waweke hapa maana sasa najiandaa kuwa mwongo kwa vile ukweli umenitokea puani. Na kama wanawake humu jf watueleze wenyewe kipi wanataka kutoka kwetu kati ya hivyo vitatu ili wawe na amani. Nawasilisha!
Sister Lizzy,asilimia kubwa ya ndoa zenye amani na zinazodumu zimejaa uwongo kuliko ukweli,ingawa si maanishi uwongo wa "kujiiba "natumai unajua nachomaanisha kwenye bold hapo...kwa mfano ni mwezi wa tano nadaiwa 'Nadia' nina mambo mengine mengi yananizunguka mfuko hautoshelezi kwa yote at a time inabidi ilo la nadia nidanganye na mtu analidhika na furaha tele,Je nikimpa makavu si itakuwa hatari Sis? hivyo uwongo katika maisha ya mahusiano yenye amani haukwepeki kabisa.Hmaster hongera kwa kua na roho nzuri yenye huruma na pia kwa kua mkweli.
Wewe baki na ukweli wako..atakasirika kwa muda ila baadae atapotezea au atakuelewa.Ukianza kudanganya jua kabisa unaweza kudanganya kitu kidogo sana kisicho na maana kikaja kukuletea matatizo makubwa sana kwenye ndoa yako.Imagine ulivyomjulisha unaenda Tegeta kama ungemwambia unapeleka mzigo au unamfuata mtu alafu bahati mbaya ukapata ajali.Aje kugundua kwenye gari ulikua na mwanamke mwenye mtoto kwa jinsi anavyoonekana ana wivu angeshakusingizia huyo ni mwanamke wako na mtoto ni mwanao ndoa imekufa.Uongo hata siku moja haulipi....jitahidi tu kua unamweleza na kumwelewesha taratibu bila kua mkali!
Well kama uongo kwako unasaidia mi ni nani hata nikwambie uache?!Endelea tu ila jua kwamba mtu mzima hadanganyiki kila siku...na kama ukweli tu anakua mgumu kuukubali na kurlewa imagine siku atakapogundua unamdanganya tena akiwa na uhakika....ndo utazushiwa mpaka yasiyo zushika.Alafu kama hutojali mimi kuuliza unalazimika vipi kumdanganya mkeo mambo yahusuyo pesa?!Kwani yeye hajua hali yenu ilivyo?!Hamna mambo ambayo mmeyawekea kipaumbele kwa pamoja?!Nauliza tu maana kitu kama hicho inabidi nacho umdanganye wakati na yeye yupondani ya hiyo ndoa ni KAAZI KWELI KWELI.Samahani kama ntakua nimekukwaza!Sister Lizzy,asilimia kubwa ya ndoa zenye amani na zinazodumu zimejaa uwongo kuliko ukweli,ingawa si maanishi uwongo wa "kujiiba "natumai unajua nachomaanisha kwenye bold hapo...kwa mfano ni mwezi wa tano nadaiwa 'Nadia' nina mambo mengine mengi yananizunguka mfuko hautoshelezi kwa yote at a time inabidi ilo la nadia nidanganye na mtu analidhika na furaha tele,Je nikimpa makavu si itakuwa hatari Sis? hivyo uwongo katika maisha ya mahusiano yenye amani haukwepeki kabisa.
Jifunze uongo mtakatifu ambao hauwezi kukupeleka Jehanam.
Asante,ujanikwaza hayo ni maoni yangu na hayo ni ya kwako,na hapo nimejaribu kutoa mfano ambao unaweza kunikuta na nikajaribu kutumia uwongo kuweka mambo sawa ingawa hauna uhalisia...Pia sidhani kama mnaweza kukubaliana kila kitu katika maisha ya mahusiano labda kama mmoja wapo anaburuzwa,hivyo hata katika mambo ambayo mnaweza kuyapa kipaumbele mnaweza kushindana pia,itakuwaje kama yeye kumiliki kwanza usafiri ndilo liwe la kwanza then mengine yafatie? Maisha ya mahusiano ni sanaa na waigizaji ni wale ambao wako katika hayo mahusiano kwa mtazamo wangu.Well kama uongo kwako unasaidia mi ni nani hata nikwambie uache?!Endelea tu ila jua kwamba mtu mzima hadanganyiki kila siku...na kama ukweli tu anakua mgumu kuukubali na kurlewa imagine siku atakapogundua unamdanganya tena akiwa na uhakika....ndo utazushiwa mpaka yasiyo zushika.Alafu kama hutojali mimi kuuliza unalazimika vipi kumdanganya mkeo mambo yahusuyo pesa?!Kwani yeye hajua hali yenu ilivyo?!Hamna mambo ambayo mmeyawekea kipaumbele kwa pamoja?!Nauliza tu maana kitu kama hicho inabidi nacho umdanganye wakati na yeye yupondani ya hiyo ndoa ni KAAZI KWELI KWELI.Samahani kama ntakua nimekukwaza!
Kuna ya kusema na ya kutokusema bora ukae kimya tu, kama hapo ungenyamaza labda mkeo anakujua kabisa wewe sio mtu wa kutoa misaada ya aina hiyo, ghafla umempeleka mwanamke huyo tegeta, hata mimi pangechimbika tu, kwa nini usingempeleka stand ukampa alf kumi akasepa zake
Kuna ukweli mwingine ni noma hausemekiMsemakweli ni mpenzi wa mungu. Mie na kusifu kwa ukweli wako.
Kudanganya: Fikiria kama ungedanganya alafu unapata ajari, unakutwa wewe na mwanamke na watoto ndani ya gari mumeumia, je unafkiri mkeo angekufikiriaje? Angekuona muongo na sio muaminifu. Bora ulivo muambia ukweli maana baadae atagundua kama angekuwa mpenzi wako husinge muambia, ungeficha. Ni wivu tu unamuangaisha sio lengine.
Jiulize hata ingekuwa wewe mwenyewe kama mkeo angetoa msaada kama uwo kwa mwanaume na kuchelewa kurudi home ungejiskiaje? Sababu msaada hata wanaume wanaitaji pia. Nazani hata wewe ungekasilika pia, ungeona wivu na ungefikiria vingine.
Mwanaume wengine akili zenu fupi bana, munafanya vitu bila kuzingatia. Mtu alie kuwa ktk ndoa hatakiwi kufanya vitu kama hivyo bila kumshirikisha mwenzawake. Kama ungelikuwa na akili nzuri ungempa nauli huyo dada ukawai home kwa mkeo mda unao takiwa.
Au ungempigia sim mkeo na kumuliza je umpe nauli au umuendeshe huyo dada. Munayataka wenyewe sababu hamtumii akili.
Kuna ukweli mwingine ni noma hausemeki