Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,869
Wakati deni la Taifa linakua kwa kasi ya kutisha, ukweli ni kwamba;
1. Watoto wetu bado wanasoma kwenye shule zenye miundombinu duni sana huku elimu yao ikiwa haijengi kesho bora kwao kwenye dunia hii ya ushindani,
2. Miradi ya maendeleo si barabara, si majengo inajengwa chini ya viwango kwa kasi ya kutisha sana huku ikitumia fedha nyingi zinazoibwa na Wanasiasa na Viongozi wengine.
3. Mifuko ya Serikali na Umma ina madeni ya kutisha sana kiasi ambacho itafika kipindi wastaafu wanaweza kuanza lukosa pensheni.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
4. Huduma za msingi kwa wananchi kama Maji na Matibabu ya uhakika zinatolewa kwa kiwango cha chini sana kila siku kutokana na kukosekana kwa miundombinu ya uhakika ya maji na madawa ya uhakika hospitalini.
5. Hakuna suluhisho la uhakika juu ya matatizo ya msingi kwa wananchi. Kinachosambazwa kwa nguvu kwa wananchi ni propaganda za kuwarubuni na kuwahaadaa ili kuendelea kuwafanya wajinga.
5. Kuna matumizi mabaya sana ya fedha za walipakodi wa Tanzania, hasa kuzitumia kinyume na matakwa ya hii hii Katiba inayosemwa mbovu. Kumekuwa na uchotaji mkubwa wa fedha za walipakodi kwa ajili ya matumizi ya Viongozi wa Kisiasa, Chama Tawala chenyewe CCM na Kundi dogo la watu wa Karibu wa Viongozi wa kisiasa.
Yanayosemwa kuhusu Rais kutoa hela kwa Viongozi wa Dini, Timu za Simba na Yanga na maeneo mengine ni madogo sana kulinganisha na namna hela zimekuwa zikitumiwa. Taarifa nyeti zinasema Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Wilaya wamekuwa wakitumia fedha za Serikali ambazo ni kodi za Wananchi kugharamia shughuli za CCM ikiwemo kulipa posho viongozi wao na makada wao.
Kwa hali hii wana JF tusahau maendeleo ya kweli chini ya hii CCM. Huu ni ukweli mchungu ambao wote lazima tuukubali. CCM wanatumia nguvu kubwa sana kuwekeza kwenye propaganda, wizi wa kura, uongo ili waendelee kubaki mabarakani. Kwa hizi njia tu wanazotumia, kamwe hawawezi kutupa maendeleo ya kweli.
Wanachama na Wanasiasa waliopo ndani ya CCM wote wanachowaza ni vyeo na ulaji. Hakuna anayewaza namna na kuumiza kichwa juu ya Tanzania iweje ili iweze ku survive katika dunia hii ya ushindani katika miaka inayokuja.
Hakuna anayewaza namna ya kutatua moja kwa moja shida na changamoto zinazowakabili watanzania. Wamejaa ujinga tu. Hawana lolote la maana wanalofanya.
Cha kusikitisha sana, Wanasiasa hawa hawawazi kesho yetu kama Taifa, wao ni maumini wa uongo na ulaghai.
Napenda kuhitimisha kwa kusema, tusitegemee chochote cha maana kutoka kwa CCM. Ni heri zitumike mbinu zote halali na zisizo halali watolewe madarakani maana kiukweli na wao wanatumia mbinu zisizo halali ili waendelee kukaa madarakani ikiwemo wizi wa kura, kuiba chaguzi na hadi kuua na kuwapoteza wapinzani wao.
Asanteni
Lord Denning
Ukonga, DSM.
1. Watoto wetu bado wanasoma kwenye shule zenye miundombinu duni sana huku elimu yao ikiwa haijengi kesho bora kwao kwenye dunia hii ya ushindani,
2. Miradi ya maendeleo si barabara, si majengo inajengwa chini ya viwango kwa kasi ya kutisha sana huku ikitumia fedha nyingi zinazoibwa na Wanasiasa na Viongozi wengine.
3. Mifuko ya Serikali na Umma ina madeni ya kutisha sana kiasi ambacho itafika kipindi wastaafu wanaweza kuanza lukosa pensheni.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
4. Huduma za msingi kwa wananchi kama Maji na Matibabu ya uhakika zinatolewa kwa kiwango cha chini sana kila siku kutokana na kukosekana kwa miundombinu ya uhakika ya maji na madawa ya uhakika hospitalini.
5. Hakuna suluhisho la uhakika juu ya matatizo ya msingi kwa wananchi. Kinachosambazwa kwa nguvu kwa wananchi ni propaganda za kuwarubuni na kuwahaadaa ili kuendelea kuwafanya wajinga.
5. Kuna matumizi mabaya sana ya fedha za walipakodi wa Tanzania, hasa kuzitumia kinyume na matakwa ya hii hii Katiba inayosemwa mbovu. Kumekuwa na uchotaji mkubwa wa fedha za walipakodi kwa ajili ya matumizi ya Viongozi wa Kisiasa, Chama Tawala chenyewe CCM na Kundi dogo la watu wa Karibu wa Viongozi wa kisiasa.
Yanayosemwa kuhusu Rais kutoa hela kwa Viongozi wa Dini, Timu za Simba na Yanga na maeneo mengine ni madogo sana kulinganisha na namna hela zimekuwa zikitumiwa. Taarifa nyeti zinasema Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Wilaya wamekuwa wakitumia fedha za Serikali ambazo ni kodi za Wananchi kugharamia shughuli za CCM ikiwemo kulipa posho viongozi wao na makada wao.
Kwa hali hii wana JF tusahau maendeleo ya kweli chini ya hii CCM. Huu ni ukweli mchungu ambao wote lazima tuukubali. CCM wanatumia nguvu kubwa sana kuwekeza kwenye propaganda, wizi wa kura, uongo ili waendelee kubaki mabarakani. Kwa hizi njia tu wanazotumia, kamwe hawawezi kutupa maendeleo ya kweli.
Wanachama na Wanasiasa waliopo ndani ya CCM wote wanachowaza ni vyeo na ulaji. Hakuna anayewaza namna na kuumiza kichwa juu ya Tanzania iweje ili iweze ku survive katika dunia hii ya ushindani katika miaka inayokuja.
Hakuna anayewaza namna ya kutatua moja kwa moja shida na changamoto zinazowakabili watanzania. Wamejaa ujinga tu. Hawana lolote la maana wanalofanya.
Cha kusikitisha sana, Wanasiasa hawa hawawazi kesho yetu kama Taifa, wao ni maumini wa uongo na ulaghai.
Napenda kuhitimisha kwa kusema, tusitegemee chochote cha maana kutoka kwa CCM. Ni heri zitumike mbinu zote halali na zisizo halali watolewe madarakani maana kiukweli na wao wanatumia mbinu zisizo halali ili waendelee kukaa madarakani ikiwemo wizi wa kura, kuiba chaguzi na hadi kuua na kuwapoteza wapinzani wao.
Asanteni
Lord Denning
Ukonga, DSM.