Ukweli kuhusu uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TIC

namtumbo

Member
Aug 30, 2011
78
102
Ndugu Wanabodi,
Tangu kutenguliwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TIC Bi Kairuki, kumekuwepo na mjadala mkubwa wenye kutoa hoja na uchambuzi wa aina mbalimbali wengine wakimtetea na wengine wakimponda,ilimradi kila mtu na fikra zake.

Katika mijadala yote, kwa bahati mbaya msingi wa maoni yaliyotolewa uliegemea kwenye taarifa za uwongo na potofu ambazo zimetolewa aidha kwa makusudi au kwa kutofahamu.

Mimi sitoingia kwenye mtego wa kuingia mjadala, bali nitakachofanya ni kuwasaidia wanaBodi kuwaelezea taarifa zipi zilizotolewa kwenye mitandao sio za kweli:

1) Sio kweli kwamba Bibi Kairuki alifuatwa na Rais Kikwete afrika ya kusini na kuombwa kurudi nchini kuja kufanya kazi TIC na akaahidiwa kiwango chochote kile cha mshahara.

Ukweli ni kwamba mwaka 2012, nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa TIC ilitangazwa baada ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo Bw Ole Naiko kumaliza kipindi chake cha Uongozi.

Awamu ya kwanza ya Usaili wa nafasi hiyo ya Mkurugenzi wa TIC ilifanywa na Kampuni ya KPMG kwa niaba ya Bodi ya TIC. Na awamu ya pili ya usaili ilifanywa na Bodi yenyewe ya TIC. Bibi Kairuki alisailiwa kwenye awamu zote mbili na kushinda usaili huo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Tanzania Investment Act ya mwaka 1997 kifungu cha 10, Mkurugenzi wa TIC anateuliwa na Rais, hivyo baada ya kufaulu usaili jina la Bi Kairuki lilipelekwa kwa Rais ili amteue kama Sheria ya TIC inavyoelekeza.

Kwa mantiki hiyo taarifa zilizotolewa kwamba Bi Kairuki alitafutwa na Rais aje kusaidia TIC na kwamba alikuwa analipwa usd 18,000 na JK akamuahidi atamlipa alafu baadaye wakageuka hazina chembe hata moja ya ukweli.

Pia ipo dhana kwamba Bi Kairuki alipata kazi ya TIC kwasababu amesomea nje. Huo nao ni upotoshaji,Bi Kairuki amesomea shahada yake ya kwanza katika chuo kikuu cha Dar es Salaam na Stashahada amesomea nje ya nchi.

2) Suala la mshahara wa Mkurugenzi wa TIC linatamkwa na Sheria ya Tanzania Investment Act ya mwaka 1997 kifungu cha 10 (b)..kinachoipa Bodi ya TIC jukumu la kumpangia mshahara Mkurugenzi Mkuu wa Kituo hicho. Tafsiri ya sheria ile haisemi suala la mshahara ni la majadiliano.

3) Taarifa zilizoandikwa na baadhi ya magazeti na mitandaoni kwamba Bi Kairuki alikuwa anajilipa posho ya Tshs 25Milioni ni za uwongo na ziliwahi kupikwa na kuandikwa kwenye magazeti huko nyuma (to be specific) gazeti la Raia Mwema mwaka jana. uchunguzi ulifanyika, hesabu za TIC zilikaguliwa na kuthibitisha taarifa zile hazina chembe hata moja ya ukweli. Wapikaji wa taarifa hizo wanajulikana na sababu zao zinafahamika.

Wanabodi,
Tuepuke kuendesha mijadala kwa kutumia taarifa ambazo hazijathibitishwa. Kwa wanahabari ni vema wakafanya kazi yao kwa weledi. Maadili ya fani ya Habari yanawataka kuipokea taarifa iliyotolewa na Serikali na kuitoa kwa umma kama ilivyotoka. Kitendo cha kutia chumvi na kukoleza taarifa kwa habari za uwongo sio sahihi. Kwa mtu mwenye kutaka kupata ufafanuzi kuhusu taarifa iliyotolewa, vipo vyombo vinavyohuika vinavyoweza kutoa maelezo sahihi kuhusu suala hii. Navyo ni Wizara ya Viwanda na Biashara na Bodi ya TIC.
 
Umeandika mengi ambayo msingi wake ni zile taarifa mbili. Moja ni utetezi wa Kairuki na nyingine ni iliyofichua kuwa alikuwa anajilipa posho ya 25M per month na kufanya safari kibao nje ya nchi. Hujaeleza hoja iliyopo kwenye ile barua ya kutumbuliwa kwake kwamba hakuwahi kuchukua mshahara tangu aajiriwe. Nini hasa kilimfanya asichukue mshahara huo?
 
Ndugu Wanabodi,
Tangu kutenguliwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TIC Bi Kairuki, kumekuwepo na mjadala mkubwa wenye kutoa hoja na uchambuzi wa aina mbalimbali wengine wakimtetea na wengine wakimponda,ilimradi kila mtu na fikra zake.

Katika mijadala yote, kwa bahati mbaya msingi wa maoni yaliyotolewa uliegemea kwenye taarifa za uwongo na potofu ambazo zimetolewa aidha kwa makusudi au kwa kutofahamu.

Mimi sitoingia kwenye mtego wa kuingia mjadala, bali nitakachofanya ni kuwasaidia wanaBodi kuwaelezea taarifa zipi zilizotolewa kwenye mitandao sio za kweli:

1) Sio kweli kwamba Bibi Kairuki alifuatwa na Rais Kikwete afrika ya kusini na kuombwa kurudi nchini kuja kufanya kazi TIC na akaahidiwa kiwango chochote kile cha mshahara.

Ukweli ni kwamba mwaka 2012, nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa TIC ilitangazwa baada ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo Bw Ole Naiko kumaliza kipindi chake cha Uongozi.

Awamu ya kwanza ya Usaili wa nafasi hiyo ya Mkurugenzi wa TIC ilifanywa na Kampuni ya KPMG kwa niaba ya Bodi ya TIC. Na awamu ya pili ya usaili ilifanywa na Bodi yenyewe ya TIC. Bibi Kairuki alisailiwa kwenye awamu zote mbili na kushinda usaili huo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Tanzania Investment Act ya mwaka 1997 kifungu cha 10, Mkurugenzi wa TIC anateuliwa na Rais, hivyo baada ya kufaulu usaili jina la Bi Kairuki lilipelekwa kwa Rais ili amteue kama Sheria ya TIC inavyoelekeza.

Kwa mantiki hiyo taarifa zilizotolewa kwamba Bi Kairuki alitafutwa na Rais aje kusaidia TIC na kwamba alikuwa analipwa usd 18,000 na JK akamuahidi atamlipa alafu baadaye wakageuka hazina chembe hata moja ya ukweli.

2) Suala la mshahara wa Mkurugenzi wa TIC linatamkwa na Sheria ya Tanzania Investment Act ya mwaka 1997 kifungu cha 10 (b)..kinachoipa Bodi ya TIC jukumu la kumpangia mshahara Mkurugenzi Mkuu wa Kituo hicho. Tafsiri ya sheria ile haisemi suala la mshahara ni la majadiliano.

3) Taarifa zilizoandikwa na baadhi ya magazeti na mitandaoni kwamba Bi Kairuki alikuwa anajilipa posho ya Tshs 25Milioni ni za uwongo na ziliwahi kupikwa na kuandikwa kwenye magazeti huko nyuma (to be specific) gazeti la Raia Mwema mwaka jana. uchunguzi ulifanyika, hesabu za TIC zilikaguliwa na kuthibitisha taarifa zile hazina chembe hata moja ya ukweli. Wapikaji wa taarifa hizo wanajulikana na sababu zao zinafahamika.

Wanabodi,
Tuepuke kuendesha mijadala kwa kutumia taarifa ambazo hazijathibitishwa. Kwa wanahabari ni vema wakafanya kazi yao kwa weledi. Maadili ya fani ya Habari yanawataka kuipokea taarifa iliyotolewa na Serikali na kuitoa kwa umma kama ilivyotoka. Kitendo cha kutia chumvi na kukoleza taarifa kwa habari za uwongo sio sahihi. Kwa mtu mwenye kutaka kupata ufafanuzi kuhusu taarifa iliyotolewa, vipo vyombo vinavyohuika vinavyoweza kutoa maelezo sahihi kuhusu suala hii. Navyo ni Wizara ya Viwanda na Biashara na Bodi ya TIC.
taarifa rasmi ndio hii unatoa wewe au na wewe yako ni udaku. hebu tueleze kama wewe ndio mtoa taarifa rasmi, tumeambiwa alikua hapokei mshahara sasa tuseme alikua anafanya kazi bure?
 
taarifa rasmi ndio hii unatoa wewe au na wewe yako ni udaku. hebu tueleze kama wewe ndio mtoa taarifa rasmi, tumeambiwa alikua hapokei mshahara sasa tuseme alikua anafanya kazi bure?
Hilo ndo swali la msingi ambalo alipaswa kutuambia. Ila amefanikiwa kutueleza kuwa kumbe huyu mama kazi aliomba mwenyewe
 
Ok sasa ukweli hasa wa yeye kutolewa kazini ni upi? Je alikuwa anapokea mshahara na kama hapokei sababu ni nini? Je alikuwa anafanya kazi ya kujitolea? Na mshahara wake ni kiasi gani? Kama hauhitaji mshahara wake kwa nini asisaidie kupunguza tatizo la ajira akakaa pemben kuruhusu mtanzania mwingine mwenye shida ya ajira aajiriwe?
 
Sijaona alichoondika mleta mada cha kuweza kudhibitsha uongo naukweli wa mijadala iliyopita ,hata na hivyo amegusa 1/8 tu ya hoja ,swala la kutopokea mashahara bado ni kizungumkuti
 
h
Mtoa mada nadhani atakuw Pasco Mayala , maana huyu baba kalialia na dada Kairuki utadhani ndiye mwajiriwa wake.
watu wengine bwana wakitumbua bosi wako maumivu yatakufikia ww maana mkono hautafik kinywani
 
Hiyo hoja namba moja hata kama Kikwete angemfuata huyo mama afrika kusini taratibu za kuajiri Ni lazima zifuatwe na hiyo hoja yako namba mbili kama mshahara ulikuwa unaeleweka toka anaomba kazi kwa nini hakuchukua huo mshahara?, kama halafu Kuna kifungu cha sheria kinachosema usipochukua mshahara Ni kosa kama hakukua na mgogoro?, habari yako inamaswali Mengi kuliko majibu uliyotuletea
 
Acha uzushi wewe mleta mada, huyu atakuwa aliahidiwa mshahara mkubwa ndio maana akakataa kupokea ule wa kwenye scale za TIC.

Wewe unajua formality za interview? Hauwezi kupeea mkataba kabla hamjakubaliana mshahara. Je ni kwa vipi yeye alianza kazi bila hilo la mshahara kuwa limekamilika?

Mleta mada usitufanye mabwege, tunaelewa kila kitu na ni nani alikuwa anampa kiburi cha kukataa mshahara wa TIC akisubiri alioahidiwa na aliyemleta huku akiishi kwa posho za safari na nyinginezo. Shame on you mleta uzi, shame on her.
 
Leno la mwandishi ni kumsafisha Jakaya period.
1. Kama alifuata taratibu zote je kwa nini ago mee mshahara?
2. Je hizo 25,000 000 mbona huzisemi? Ni nani alimuru ajilipe? Board au?
3. Kama sio Jipu aliishije muda wote huo?
 
Naona unamtetea hapo lazma kutumbuliwa kwake kumeathiri maisha yako kwanamna moja ama nyingne...
Raisi Pombe hachukui maamuzi kutokana na habar za mitandaon au magazetini, yeye anachukua hatua baada ya kujiridhisha kutoka kwenye intelijensia yake,
. Kinachofanyika ni kutafta information baada ya hyo information unafanyika uchunguzi juu ya hyo information inapogundulika ni kweli basi ni kutafutwa kwa wembe na sindano tayar kwa kutumbua...

Hii sio Tz ya kikwete ambayo taarifa zilikuwa hazifanyiwi kazi achane kutafuta huruma
 
Kwanini hakuchukua mshahara wake toka mwaka 2013, hili hujaligusia hata kidogo.
Kama umesoma kwa makini jibu lake lipo kwenye No 2. Maana yake swali hili liulizwe kwa Bodi ambayo ina Mamlaka ya Kisheria kumpangia mshahara.
 
She was ousted because she was not receiving her legal salary ever since she accepted the post,enough.I don't think this news is worthy our attention any more. Next!
 
Tatizo la nchi hii kila mtu akimiliki tecno touch screen akikaa nyuma ya screen bac anadhani ndio anajua kila kitu. Hivi tangu lini watu wakafanyiwa interview ili majina yapelekwe kwa uteuzi na rais? Unajua maana ya interview na uteuzi?
Aaagr...
Fanya utafiti utaelewa.Zipo kazi mbalimbali ambazo unafanyika usaili na mwishowe washindi watatu majina yao yanapelekwa kwenye Mamlaka za Uteuzi. Hii sio kwa TIC peke yake. mfano wa karibuni umeona baada ya bodi ya TCRA kuvunjwa wiki iliyopita, juzi tangazo limetoka watu waombe. Mwisho wake majina ya washindi yatapelekwa kuteuliwa na mwenye Mamlaka ya Uteuzi
 
Nenda kasome katiba ya 1977 itakusaidia, rais hashauliwi na mtu yeyote akiamua ameamua. Nafasi zote za uteuzi hashauliwi na mtu yeyote amteue nan na amwache nani. Sasa kitendo cha kuendesha usaili kwa position ya uteule wa rais ni kinyume na katiba ya tz. Kikwete amewafuata wengi nje akiwemo aliyekua mkurugenzi TBC Tido Mhando hili alithibitisha CAG msaafu hon. Utoh, na akaeleza ndicho chanzo cha mishahara mikubwa isiyoelezeka. Watu walikua wananunuliwa. HAUWEZI ENDESHA USAILI ETI HALAFU RAIS ATEUE, HAPANA.
 
Back
Top Bottom