Ukweli kuhusu urais CCM huu hapa

Mfukutuzi

JF-Expert Member
Feb 15, 2015
239
175
Uchambuzi Wangu:

Nawashangaa sana baadhi ya Watanzania, wamekalia Lowassa Lowassa, wakati yeye na wenzake wamechukua tu tenda (consultancy) ya kukitangaza Chama (kutumia kivuli cha kutangaza nia na kutafuta wadhamini kuanza kampeni mapema kwa ajili ya chama).

Wengi wao wameahidiwa vyeo Serikali ijayo, na kwa wafanyabiashara kama Lowassa, wameahidiwa misamaha ya kodi na uhuru wa biashara zao. Kusoma shida, hata picha? Amka Mtanzania, jifunze kusoma katikati ya mistari!

Lowassa anafeli katika vigezo vingi mno; ikiwemo afya, makundi, kashfa za ufisadi, na vinginevyo vingi, hata yeye anajua. Anyway, sina lengo la kufika huko, ila majina ya wagombea halisi na wanayoisumbua CCM ni haya. Hesabu zote zinaangukia kwa hawa na sababu nimekuwekea;-

1. Charles Makongoro Nyerere (Historia inambeba)
2. Mohamed Gharib Bilal (Mzanzibari)
3. Mizengo Kayanza Pinda (Waziri Mkuu, ni kawaida kwa mawaziri wakuu)
4. Dr Asharose Migiro (Mwanamke)
5. Jaji Augustino Ramadhani (Mzanzibari/ Ukristo-Uislam)
6. Prof. Mark Mwandosya (Uzoefu)
7. Dr. Salim Ahmed Salim [kama atachukua fomu] - (Hana kashfa/ uzoefu/ Mzanzibari)

Watu watauliza mbona wengine maarufu na hujawataja? Membe ameshaonyesha hana uwezo mkubwa wa ushawishi na pia anakabiliwa na tatizo la Makundi. Magufuli hawawezi kumteua, ni mchapakazi na yuko serious na kazi hivyo atawaharibia mambo yao. Hawawezi kumwacha kwenye kinyang'anyiro, wamemwandalia nafasi nyingine kubwa ila si urais.

Ila pamoja na hayo yote, mgombea wa CCM mwaka huu ni lazima atakuwa Mzanzibari maana hivi karibuni marais kutoka bara wamefululiza sana, na CCM wanataka kuwabembeleza Wazanzibar wabaki kwenye Muungano.

Na huu ndio utabiri wangu. Nimemaliza. Tujadili nchi tuachane na vyama, na kama huamini hili, subiri Julai 10, top 5 ya kupigiwa kura inatoka kwenye list hii, angalia nyuma ya pazia Mtanzania.

By Mr. ZigZag (Mzalendo halisi)
 
Magufuli ndo MTU pekee ambaye CCM itashinda Kiurais sana na wa kuwasaidia wabunge wa CCM kurudi bungeni vinginevyo watashinda urais lkn bunge litakuwa la wapinzani na je itawasaidia CCM kuongoza nchi?
 
Yaani hiyo habarin ya kusema ni zamu ya mzanzibzri umeitoa kwenye katiba ipi ? watu lakini 5 unawashindanisha na watu million 45 ?
Any way tuombe Mungu tupate Raisi kwa amani
 
Historia, Uzanzibari, U-mwanamke, Ukristo-Uislam, na kutokuwa -na-kashfa ndiyo vigezo vya kuchagua RAIS Tanzania......duuuu........hakika....sisi tutakuwa masikini maisha yetu yooooote kutokana na uvivu wa kufikiria....
 
Mfukutuzi

Kwa hiyo wewe kwa akili yako mgombea ni lazima atoke ccm,kwa hiyo tulazimike kumchagua mzanzibar kwa kuwa ccm watampitisha kukamilisha zamu. Huu ni upuuzi na dharau kwa watanzania.
 
Last edited by a moderator:
My observation nakubaliana na mwana Jf mmoja alishawahi kuelezea na mm nakubaluana naye...kwamba top five inaelekea kuwa hivu
1-Mohamed Bilal(Makam rais wote huwa wanaingizwa top five kwa heshima ya cheo chake)
2-M.K.Pinda(mawazir wakuu mara nying hufika top five kwa heshima ya chei chake eg. Msuya, sumaye)
3- Asharose Migiro( 50/50 kama sera yao na kushadidia Katiba pendekezwa)
5- Unknown( may be- A.Ramadhan...A. Mahiga...M.Mwandosya J.P. Magufuli)
Naona hiyo inaweza kuwa ni tiba ya makundi kati ya Lowasa na Membe na akina sita
Kuhusu makongoro Nyerere hana historia yoyote ndan ys CCM..Baba ni baba na kila mtu roho yake...isitoshe alishajichafua kwa kuhama chama na kashfa alizotoa enz hixo...kuteuliwa kuwa mbunge afrika mashariki ilikuwa kuifariji familia tu basda ya kuonekana imetengwa lkn wala siyo presidential material kwa hali yoyote...alomshaur alimpotosha tu hafiki kokotr.
 
Uchambuzi Wangu:

Nawashangaa sana baadhi ya Watanzania, wamekalia Lowassa Lowassa, wakati yeye na wenzake wamechukua tu tenda (consultancy) ya kukitangaza Chama (kutumia kivuli cha kutangaza nia na kutafuta wadhamini kuanza kampeni mapema kwa ajili ya chama).

Wengi wao wameahidiwa vyeo Serikali ijayo, na kwa wafanyabiashara kama Lowassa, wameahidiwa misamaha ya kodi na uhuru wa biashara zao. Kusoma shida, hata picha? Amka Mtanzania, jifunze kusoma katikati ya mistari!

Lowassa anafeli katika vigezo vingi mno; ikiwemo afya, makundi, kashfa za ufisadi, na vinginevyo vingi, hata yeye anajua. Anyway, sina lengo la kufika huko, ila majina ya wagombea halisi na wanayoisumbua CCM ni haya. Hesabu zote zinaangukia kwa hawa na sababu nimekuwekea;-

1. Charles Makongoro Nyerere (Historia inambeba)
2. Mohamed Gharib Bilal (Mzanzibari)
3. Mizengo Kayanza Pinda (Waziri Mkuu, ni kawaida kwa mawaziri wakuu)
4. Dr Asharose Migiro (Mwanamke)
5. Jaji Augustino Ramadhani (Mzanzibari/ Ukristo-Uislam)
6. Prof. Mark Mwandosya (Uzoefu)
7. Dr. Salim Ahmed Salim [kama atachukua fomu] - (Hana kashfa/ uzoefu/ Mzanzibari)

Watu watauliza mbona wengine maarufu na hujawataja? Membe ameshaonyesha hana uwezo mkubwa wa ushawishi na pia anakabiliwa na tatizo la Makundi. Magufuli hawawezi kumteua, ni mchapakazi na yuko serious na kazi hivyo atawaharibia mambo yao. Hawawezi kumwacha kwenye kinyang'anyiro, wamemwandalia nafasi nyingine kubwa ila si urais.

Ila pamoja na hayo yote, mgombea wa CCM mwaka huu ni lazima atakuwa Mzanzibari maana hivi karibuni marais kutoka bara wamefululiza sana, na CCM wanataka kuwabembeleza Wazanzibar wabaki kwenye Muungano.

Na huu ndio utabiri wangu. Nimemaliza. Tujadili nchi tuachane na vyama, na kama huamini hili, subiri Julai 10, top 5 ya kupigiwa kura inatoka kwenye list hii, angalia nyuma ya pazia Mtanzania.

By Mr. ZigZag (Mzalendo halisi)
Hapo kwenye nyekundu hapo ndio kwenye tatizo kubwa sana kuliko hata ulilokuwa unajaribu kulizelezea hapo juu.Tatizo la Rais wa awamu ya TANO kutoka Zanzibar kwa tiketi ya CCM kwa awamu hii ni IMPOSSIBLE kwa kuwa kitendo cha CCM kuchukua Mzanzibar ni kumwaga sumu ya Chroline Gas kwenye mfumo mzima wa MMEA unaitwa CCM na hivyo kuwapa UPINZANIA kusimamia HOJa zilizopata kuzungumzika huko siku za nyuma na kuibua UTATA wa KITAIFA.Si jambo la lelemama...dhama tulizo nazo si kuwafurahisha watu kwa vyeo..muunganao au kuundwa watu wafurahie vyeo na kuonekana ni TAIFA kwa kuwa kuna vyeo.Muungano uliundwa kwa maslahi ya Watanzania na Wanzibara raia wa kawaida watembea barabarani, wauza sokoni, wakulima, wafanyakazi na si previllges za kuwa nani apewe nini kimamlaka.

Kama ni vyeo kuna Wazanzibar wengi sana kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano,lakini hakuna Watanzania Bara kwenye Baraza la Mapinduzi Zanzibar.Mwalimu inajulikana aliiacha Serikali Mbili, Taifa moja ..Je leo ni sentenis gani itatumika kuelezea Mwalimu Nyerere alichokiacha.CCM isitake HOJa hii iludi mezani katika nyakati hizi nzito za Uchaguzi wa Rais kwa kuchagua watu watako leta Mushkeri na mikanganyiko ya kulazimisha watu wachokonoe katiba.Kuna usem upo wa funika kombe Mwana haramu apite ..si mbaya kale kautaratibu ka makamu wa Rais kutokea Zanzibar kaendelee ili kama kawaida na ipatikane team ..ya kuweza kuondoa UTANDU uiiotengenezwa huko nyuma 2010 ambao ni kama yai la kuchemsha kwenye mdomo wa Kenge.

Hoja ya Rais kutoka Zanzibar this time CCM itabdi iliweke Pending kwa USALAMA wa kuikoa ISIKUTANE na KURA za HASIRA YA UMMA.....na kwa bahari mbaya ukapasua kila kitu pasipokuwa na sababu..kisa wamewafurahisha WAKUBWA wa Zanzibar kwa kuwapa URAIS ambao ni kwa gharama ya MASLAHI ya UMMA.Kuna vitu vya kujalibu lakini NYAKATI hizi TAIFA haliitaji majaribio tena.Taifa la Tanzania linaitaji Mtu mwenye maono na mwenye uwezo wa kufanya ...Ulie MTAJA na kumpa nafasi pale juu kwa historia ya familia yake ndiye JAWABU kisha kwa kutoka hapo Sasa makosa yaliyotoke yasahihishwe.Linapokuja swala la KIKATIBA majaribio sio sehemu y mawazo au kufurahisha watu..
 
hajawahi wala hafikirii kushindwaa. Lowassa ni zaidi ya mafuriko. watz wengi wanamhitaji
 
hajawahi wala hafikirii kushindwaa. Lowassa ni zaidi ya mafuriko. watz wengi wanamhitaji

Naona siasa umeianza juzi, "hajawahi kushindwa?", unajua kaanza kugombea mwaka gani hiyo nafasi? Msituletee ushabiki bila hoja za msingi, njoo na hoja watu watakuelewa tu, hii ni JF, home of great thinkers
 
Agustino Ramadhani - Raisi
Asha Rose - Makamu wa Raisi
Agustine Mahiga - Waziri mkuu

wengine tupa chini..... (just joking)
 
Magufuli ndo MTU pekee ambaye CCM itashinda Kiurais sana na wa kuwasaidia wabunge wa CCM kurudi bungeni vinginevyo watashinda urais lkn bunge litakuwa la wapinzani na je itawasaidia CCM kuongoza nchi?
sisemu hawawezi teua jembe ka hili.
 
Naona siasa umeianza juzi, "hajawahi kushindwa?", unajua kaanza kugombea mwaka gani hiyo nafasi? Msituletee ushabiki bila hoja za msingi, njoo na hoja watu watakuelewa tu, hii ni JF, home of great thinkers
sishangai kwani huo ndio mtazamo wako na ndipo utofauti wetu kama binadamu unapoanzia. hoja ni kwamba wakati huu ambao amejipanga na yuko tayari kupokea kijiti hajawahi kufikiria kushindwa na wala hafikirii kushindwa. kuanza siasa juzi au zamani bado halimpi mtu uhalali wa kuwa sahihi muda wote. binafsi hija zako huwa naziona nyepesi sana lakini busara hunipa moyo kwamba upo katika hatua za kujifunza zaidi
 
Hapo kwenye nyekundu hapo ndio kwenye tatizo kubwa sana kuliko hata ulilokuwa unajaribu kulizelezea hapo juu.Tatizo la Rais wa awamu ya TANO kutoka Zanzibar kwa tiketi ya CCM kwa awamu hii ni IMPOSSIBLE kwa kuwa kitendo cha CCM kuchukua Mzanzibar ni kumwaga sumu ya Chroline Gas kwenye mfumo mzima wa MMEA unaitwa CCM na hivyo kuwapa UPINZANIA kusimamia HOJa zilizopata kuzungumzika huko siku za nyuma na kuibua UTATA wa KITAIFA.Si jambo la lelemama...dhama tulizo nazo si kuwafurahisha watu kwa vyeo..muunganao au kuundwa watu wafurahie vyeo na kuonekana ni TAIFA kwa kuwa kuna vyeo.Muungano uliundwa kwa maslahi ya Watanzania na Wanzibara raia wa kawaida watembea barabarani, wauza sokoni, wakulima, wafanyakazi na si previllges za kuwa nani apewe nini kimamlaka.

Kama ni vyeo kuna Wazanzibar wengi sana kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano,lakini hakuna Watanzania Bara kwenye Baraza la Mapinduzi Zanzibar.Mwalimu inajulikana aliiacha Serikali Mbili, Taifa moja ..Je leo ni sentenis gani itatumika kuelezea Mwalimu Nyerere alichokiacha.CCM isitake HOJa hii iludi mezani katika nyakati hizi nzito za Uchaguzi wa Rais kwa kuchagua watu watako leta Mushkeri na mikanganyiko ya kulazimisha watu wachokonoe katiba.Kuna usem upo wa funika kombe Mwana haramu apite ..si mbaya kale kautaratibu ka makamu wa Rais kutokea Zanzibar kaendelee ili kama kawaida na ipatikane team ..ya kuweza kuondoa UTANDU uiiotengenezwa huko nyuma 2010 ambao ni kama yai la kuchemsha kwenye mdomo wa Kenge.

Hoja ya Rais kutoka Zanzibar this time CCM itabdi iliweke Pending kwa USALAMA wa kuikoa ISIKUTANE na KURA za HASIRA YA UMMA.....na kwa bahari mbaya ukapasua kila kitu pasipokuwa na sababu..kisa wamewafurahisha WAKUBWA wa Zanzibar kwa kuwapa URAIS ambao ni kwa gharama ya MASLAHI ya UMMA.Kuna vitu vya kujalibu lakini NYAKATI hizi TAIFA haliitaji majaribio tena.Taifa la Tanzania linaitaji Mtu mwenye maono na mwenye uwezo wa kufanya ...Ulie MTAJA na kumpa nafasi pale juu kwa historia ya familia yake ndiye JAWABU kisha kwa kutoka hapo Sasa makosa yaliyotoke yasahihishwe.Linapokuja swala la KIKATIBA majaribio sio sehemu y mawazo au kufurahisha watu..

Bado hujawa na uwezo wa kujenga hoja zenye mashiko . Mengi ya uliyoeleza hayaeleweki kabisa na hata sababu ulizotoa hazipo na zilishapitwa muda.
 
Back
Top Bottom