Ukweli kuhusu Mtela Mwampamba

hawa jamaa hawasikiki tena,chezea ccm wewe,umalaya unapohamishiwa hadi kwenye siasa matokeo yake ndio haya..acheni kuendekeza njaa vijana mtapakatwa.

Tupo tunatekeleza Ilani ya chama chetu CCM. CCM Safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Leo ndo umekuja kusema ukweli! Je, yule Tambwe Hiza yeye ni nani saivi ndani ya CCM? Hajasikika muda mrefu saivi kuna nini kimemtokea?

Mbona hata FRED MPENDAZOE nae kama siku hizi pia hasikiki vp kuna nini!!!!!!!
 
Umekuja kujitangaza kuwa umepewa 'cheo' UVCCM!!?
Bwana mdogo tafuta kazi ya kufanya niliwahi kusikia kuwa wewe ni mwalimu tafadhali tafuta pa kujishikiza, utadhalilika sana siku za hivi karibun usipofanya hivyo!
 
Sio vituko nasema kweli nimeajiriwa toka mwezi wa Tano na nimeamua kusema ili kuondoa mkanganyiko wa kuniuliza kwamba nasema nikiwa kama nani!!!
Ahaa! Sasa sister Juliana Shonza vipi yeye bado hajafikiriwa pa kuchomekwa? Nayeye kajitahidi kutumika kwa muda mrefu kidogo sasa!
 

Ndo nini sasa?, acha kutuaribia jamvi. R.U.B.I.S.H.
 
Sio hivyo mkuu nazani umesahau kwamba hata Dk Slaa ni Padre kitaaluma but kwa sasa ni katibu mkuu wa chadema!!! na usisahau kwamba Mbowe ni Disco Joker(DJ) kitaaluma but kwa sasa ni mwenyekiti wa chadema taifa!!!!! tuko pamoja mkuu.

Sasa hapo nimeelewa tatizo kubwa la ndani ulilo nalo. Dr Stephen Ulimboka ni daktari kitaaluma na anafanya kazi yake ya kutibu wagonjwa lakini pia ni MWENYEKITI wa jumuia ya madaktari. Wewe kazi unayoifanya ya afisa habari ni ya KITAALUMA, ila unaweza kuwa Mwenyekiti wa UVCCM kwa mfano kwa sio kazi ya kitaaluma.

Pia sasa nimeelewa kuwa hata majukumu yako inawezekana huyajui. Kuwa fair kwa wanaCCM wenzio ingekuwa vizuri ungeweka na JOB DESCRIPTION yako hapa ili wajiridhishe na kuona ni aina gani ya kazi utakuwa unazifanya. Ila zingatia sana ushauri wangu bwana mdogo, kwa umri wako itafikia kuwa na familia, utapata watoto ambao watahitaji kusoma, tena katika shule nzuri tu. Lazima uwaze kuhusu maisha yako ya baadaye kwa kuwa na Job Security, hizi kazi za kupeana zawadi ni mbaya. Kwa mfano siku inatokema Mwigulu aliyekupa hiyo kazi anakuomba JICHO kwa mfano, na ukimpa jicho lako hutaona tena, lakini ukimnyima unarisk nafasi yako, utabaki njia panda na kujutia maisha yako. Njia nzuri ya maisha yako mdogo wangu ni kumuomba akusaidie upate shule ya kufundisha hapa Dar, piga kazi ya ualimu huku ukifanya siasa kama Party time. Kuna leo na kesho mdogo wangu.
 
Ushauri wa bure, wattalamu wana sema kila mtu amezaliwa na kipaji ambacho ukikitumia vizuri unakuwa mtu huru kabisa na maisha yanakwenda, sasa jitafute kipaji chako, kitumikie kitakupa heshikma saidi ya kuwa mzazi wa Vccm, ukifuata hili baada ya miaka mitano utarudi kunishukuru, ni muda wa kuamka sas muda unaruhusu, acha kuishi kwa ukibaraka, ili kujiletea heshima kwa girlfriend wako kama unae na ndugu zako, haujazaliwa kutmikishwa ubaya ili kulipwa ushuru usio naheshima tafakari chukua hatua
 
Hiyo kazi ina maana hakukuwa na kijana mwingine wa CCM aliyekulia katika maadili ya chama akapewa?walitumia kigezo gani kukupa hiyo kazi mtu hata usiyezijua vizuri sera na misingi ya chama?au ndo malipo ya kazi uliifanya ya kutukana watu wazima....???shame on you dogo...anyway hope utatulia sasa ukijenge chama chako
 
Hivi ile pesa,na gari si walishakupa? Na hii ndio ajira uliyoahidiwa ili usaliti wana mbozi? Mtela mungu akuongoze kutenda,kama kuhama chama kwangu sijaona kosa japo walikutimua,basi huko uliko tenda mema na si kujaza chuki kwa wananchi kwa skendo chafu! Mlikuja na mkakati wa kumchafua slaa mmeishia wapi?
 
Sio hivyo mkuu nazani umesahau kwamba hata Dk Slaa ni Padre kitaaluma but kwa sasa ni katibu mkuu wa chadema!!! na usisahau kwamba Mbowe ni Disco Joker(DJ) kitaaluma but kwa sasa ni mwenyekiti wa chadema taifa!!!!! tuko pamoja mkuu.

Mbowe hajawahi kuwa DJ, ila amewahi kumiliki clubs za Disco kuanzia Mbowe Hotels hadi sasa ni Club Billicanas.
Nadhani wakati wakina Kalikali (RIP) wanapiga DISCO pale Mbowe Hotels miaka ile ya 1980s, wewe bado ulikuwa haujulikani.
Tuletee ushahidi wa kuonyesha kwamba Mbowe alikwahi kuwa DJ.
 

Pia ninaDuka langu pale Mtaa wa ngomati Keko. karibu sana kuna nguo nzuri sana za watoto.
 
Khaa!! Ruzuku ikikata tu kibarua nacho kinaota :bored:
 

Kuna picha Mbowe akiwa ameweka kalikiti nywele na pia nikiwa chadema mala nyingi tu alikuwa anakumbushia UDJ hasa kweli yale mafuso ya chadema.
 
Pia ninaDuka langu pale Mtaa wa ngomati Keko. karibu sana kuna nguo nzuri sana za watoto.

Now you are talking... Hongera sana kama ni kweli!!

Kitumikie chama chako na uondoe ile dhana ya Mwigulu kuwa siasa ni uadui na uhasama. Nje ya siasa kuna maisha ya kawaida yanaendelea. Nitakuja dukani kwako kununua nguo za wanangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…