Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,952
- 10,037
Mkuu nami nimefuatilia hizi habari na hasa maandiko ya mihangwa tangia zamani. Naona anayoyaandika kwenye Raia mwema ni marudio ya makala alizoziandika kwenye gazeti la Rai hapo zamani. Ni kweli pia kwamba Mihangwa na Ahmed Rajab wametofautiana kuhusu historia hiyo. Kuna siku nilisoma habari za Ahmed nikaona inayofautiana na yaliyoandikwa na Mihangwa ikabidi nimuandikie Mihangwa kumuuliza lakini bahati mbaya hakunijibu. Ila kwa jinsi nilivyofuatilia hizi makala kwangu mimi naona kama Mihangwa ana ukweli mwingi kuliko Ahmed. Naona Ahmed kama anaegemea zaidi kwenye HIZBU ila Mihangwa yupo zaidi upande wa ASP na UMMA party. Pia Mihangwa anaonekana kumkubali Okelo kama kiongozi wa mapinduzi. Ukweli huu unachagizwa zaidi na ile picha ambayo Okelo anaonekana akiwa na wanamapinduzi wengine wakiwa wamemzunguka naye akiwa ameketi kama kiongozi.