Ukweli kuhusu kujenga ukweni.

Ukweli kuhusu kujenga ukweni.

Lodge zimewekwa za kazi gani? Kama hakuna sehemu ya kufikia, tutafikia hotel... Hela yenyewe iko wapi ya kujanga nyumba porini kisa kufikia..hiyo pesa si bora uweke kitega uchumi kikuzarishie maana kuna leo na kesho huwezi jua itakuaje?

Mambo ya kujenga ukweni sijui nyumbani ni jukumu la wazazi.. Watoto ni kusaidia tu ikiwezekana lakini sio lazima

umenena mkuu... Asnam aje asome hii....


Tena unakuta kijijini kwenyewe kwenda mara moja baada ya miaka mitatu.....ni kupoteza nguvu bure na matumizi mabaya ya fedha
 
Last edited by a moderator:
Ukiona kujenga ukweni ni ishu sana jua una pesa ya mawazo.

Mie kama naweza jenga home kwa mume kama hela ipo.

Pesa makaratasi hasara roho.

Imagine nishindwe tumia 10 percent ya pato langu kumfurahisha mme? Hasa kama yeye kafulia daima?

Ujue kama una uwezo afu wakwe zako wanaishi kwenye nyumba mbovu ni aibu yako. Wee unaona raha tu kumachakachua mtoto wao afu unaonaa taabu sana kuwajengea?

Kumbe lile jamaa lilikuwa na akili, salute kwake!
 
Hivi kweli umeoana na mwenza, mmezaa watoto, kwao wana nyumba ya Tembe, afu wee kipato kinaruhusu, kwenye utashindwa jenga nyumba bora zaidi ya ile?

Hata watoto wako wakitembelea kwa bibi na babu watapata raha?

Kwani thamani ya mme/mke ni nini? Thamani yao ni nyumba?

Kwa hiyo sie kwetu kuna mansion aafu kwa mme kuna tembe? Kweli? Kisa naogopa siku tukiachana sitaibeba nyumba? Hata tukiachana naamini kuna wakati aliwahi nifanya nifurahi, kwa hilo anastahili nyumba kwa wazazi wake kama nna uwezo huo.
 
Bujibuji ndio maana unaachwa kwenye mataa kila kukicha kwa misimamo yako iliyopitwa na wakati! Mwenzio Mwita Maranya kajenga kwetu tena kajenga ghorofa! Sasa hivi ndio kaanza kujenga kibanda kwao Tarime. Lol!
mwaJ ninachompendea Mwita Maranya anajua fika kuwa kapewa limbwata, lakini hiyo haimsumbi
 
Last edited by a moderator:
Hahahah, hivi mlinunua mizigo mingapi ya nyasi kwenye nyumba ya Taaarime???

Unadhani hata tulinunua basi? Mwita aliwaomba watoto wa nduguze wakakate na kupeleka hapo kwenye boma. Nadhani aliwapa hela kidogo tu ya kununulia jani na soda moja ya machozi ya simba!
 
Kuna ndugu yangu alijenga ukweni, mapenzi yalipoisha mama mkwe akamwambia toa nyumba yako sasa hivi kwenye kiwanja changu
Hapa unamwambia mwanamke au mwanaume?

Hivi kwa nini ujenge kwa wakwe?
Ni ukosefu wa viwanja?
Nguvu ya limbwata?
Upungu wa fikra?

Na unakuta mtu ana jenga kwa wake heti kisa alipewa kiwanja alaf mwisho wa siku ana fukuzwa!
Cha kushangaza zaidi unakuta mtu kama huyu kwao hajajenga na nyumba ina vuja kabisa!

Kama ulipewa kiwanja na mkwe weka nyumba za kupangisha baada ya kumaliza kujenga kwenu!
 
Hivi kweli umeoana na mwenza, mmezaa watoto, kwao wana nyumba ya Tembe, afu wee kipato kinaruhusu, kwenye utashindwa jenga nyumba bora zaidi ya ile?

Hata watoto wako wakitembelea kwa bibi na babu watapata raha?

Kwani thamani ya mme/mke ni nini? Thamani yao ni nyumba?

Kwa hiyo sie kwetu kuna mansion aafu kwa mme kuna tembe? Kweli? Kisa naogopa siku tukiachana sitaibeba nyumba? Hata tukiachana naamini kuna wakati aliwahi nifanya nifurahi, kwa hilo anastahili nyumba kwa wazazi wake kama nna uwezo huo.

Kongosho hiyo ni case tofauti....... Kuna watu kibanda cha chumba kimoja hawana ila wanajenga ukweni big no.......

Jenga kwanza makazi yako ....... Then ndo uhamie kujenga kwa wazazi wenu.........

ikishindikana basi repair kwa wazee wenu then jenga kwako ndo ukajenge kwenu/ukweni......

Kuna kesho na keshokutwa
 
Last edited by a moderator:
lipo bora kujenga ukweni au nyumba ndogo?
 
akienda kwao atafikia wapi yeye na familia yake au ndo kujibana na wazazi kwenye kibanda kimoja.

Kwani kufikia guest house/hostel dhambi? Au utamaduni umewadunisha watanzania?
 
Hapa unamwambia mwanamke au mwanaume?

Hivi kwa nini ujenge kwa wakwe?
Ni ukosefu wa viwanja?
Nguvu ya limbwata?
Upungu wa fikra?

Na unakuta mtu ana jenga kwa wake heti kisa alipewa kiwanja alaf mwisho wa siku ana fukuzwa!
Cha kushangaza zaidi unakuta mtu kama huyu kwao hajajenga na nyumba ina vuja kabisa!

Kama ulipewa kiwanja na mkwe weka nyumba za kupangisha baada ya kumaliza kujenga kwenu!

Hapo mwishon ndo umeharibu point ya msingi usijenge ukweni...ukfnya hivyo c umejeng huko huko ukweni ti sema ni nyumba ya kupanga
 
Hivi kweli umeoana na mwenza, mmezaa watoto, kwao wana nyumba ya Tembe, afu wee kipato kinaruhusu, kwenye utashindwa jenga nyumba bora zaidi ya ile?

Hata watoto wako wakitembelea kwa bibi na babu watapata raha?

Kwani thamani ya mme/mke ni nini? Thamani yao ni nyumba?

Kwa hiyo sie kwetu kuna mansion aafu kwa mme kuna tembe? Kweli? Kisa naogopa siku tukiachana sitaibeba nyumba? Hata tukiachana naamini kuna wakati aliwahi nifanya nifurahi, kwa hilo anastahili nyumba kwa wazazi wake kama nna uwezo huo.

tuko wote.
 
Kwani kufikia guest house/hostel dhambi? Au utamaduni umewadunisha watanzania?

ww wasema haina maana kulala na swimming pool sebuleni kwako wakati kwenu nyumba imelalia upande kisa utafikia guesti,hotel,hostel haijalishi una pesa kiasi gani hali ya kwenu ndo itakutambulisha upeo wako wa fikra kama umedumaa au umechangamka.
 
kumbuka kujenga kwa wakwe ni sawa na kujenga kwenye hifadhi ya barabara

Kama na wewe hutawajengea wazazi wako hapo sawa, ila huwezi kujenga kwenu kisha upinge kusaidia kujenga kwa wazazi wa mkeo, na kwao huyo ni mtoto wao.

Japo hilo linategemea vigezo vingi sana ikiwemo uwezo wa wakwe zako na ndugu wa mkeo. Kwa familia zetu wengi wetu wazazi hawajaweza kuwa na uwezo wa kujenga nyumba nzuri ndio maana mtu mambo yakikaa sawa unajitahidi kuwajengea nyumba nzuri wazazi wako, sasa kama kuna umuhimu wa kujenga kwenu kwa nini isiwe na umuhimu kwa wazazi wa mkeo Bujibuji. Na kama la kuwasaidia kujenga linakua gumu, utawasaidia katika mambo mengine kweli?
 
Last edited by a moderator:
Samaritan, tutawajengea wazazi mambo yakiwa sawa. Hapa ninaowaongelea, ni kama Mwita Maranya, mjini hana nyumba anaishi nyumba ya kupanga lakini kaenda kujenga ukweni, kwa wazazi wa mwaJ
Kama na wewe hutawajengea wazazi wako hapo sawa, ila huwezi kujenga kwenu kisha upinge kusaidia kujenga kwa wazazi wa mkeo, na kwao huyo ni mtoto wao.

Japo hilo linategemea vigezo vingi sana ikiwemo uwezo wa wakwe zako na ndugu wa mkeo. Kwa familia zetu wengi wetu wazazi hawajaweza kuwa na uwezo wa kujenga nyumba nzuri ndio maana mtu mambo yakikaa sawa unajitahidi kuwajengea nyumba nzuri wazazi wako, sasa kama kuna umuhimu wa kujenga kwenu kwa nini isiwe na umuhimu kwa wazazi wa mkeo Bujibuji. Na kama la kuwasaidia kujenga linakua gumu, utawasaidia katika mambo mengine kweli?
 
Last edited by a moderator:
Samaritan, tutawajengea wazazi mambo yakiwa sawa. Hapa ninaowaongelea, ni kama Mwita Maranya, mjini hana nyumba anaishi nyumba ya kupanga lakini kaenda kujenga ukweni, kwa wazazi wa mwaJ

Unajua mkuu Bujibuji, kodi ya mwaka hapa mjini unajenga nyumba ya kueleweka huko tunakotoka.
Binafsi kama naweza kupanga mjini na wazazi wangu hawaishi sehem nzuri siwezi kabisa kuwa comfortable hata kama naishi Oysterbay/Masaki.

Mwita Maranya anachotaka ni amani na furaha kwenye ndoa yake, unadhani mwaJ akiwa na furaha ya kuona wazazi wake wanaishi kwenye nyumba nzuri hajisikii vizuri? na hilo haliongezi uimara na upendo kwenye ndoa?

Kuna baraka zake unapowakumbuka wazazi kwa kuwapatia sehem nzuri ya kuishi hasa kama uwezo unaruhusu, usiseme kujenga kwa wakwe ni kama kujenga kwenye hifadhi ya barabara mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Unajua mkuu Bujibuji, kodi ya mwaka hapa mjini unajenga nyumba ya kueleweka huko tunakotoka.
Binafsi kama naweza kupanga mjini na wazazi wangu hawaishi sehem nzuri siwezi kabisa kuwa comfortable hata kama naishi Oysterbay/Masaki.

Mwita Maranya anachotaka ni amani na furaha kwenye ndoa yake, unadhani mwaJ akiwa na furaha ya kuona wazazi wake wanaishi kwenye nyumba nzuri hajisikii vizuri? na hilo haliongezi uimara na upendo kwenye ndoa?

Kuna baraka zake unapowakumbuka wazazi kwa kuwapatia sehem nzuri ya kuishi hasa kama uwezo unaruhusu, usiseme kujenga kwa wakwe ni kama kujenga kwenye hifadhi ya barabara mkuu.

Haelewi huyo bora umueleweshe.
 
Hiki ndicho haswa nilichokuwa nikiongelea....
Bujibuji ndio maana unaachwa kwenye mataa kila kukicha kwa misimamo yako iliyopitwa na wakati! Mwenzio Mwita Maranya kajenga kwetu tena kajenga ghorofa! Sasa hivi ndio kaanza kujenga kibanda kwao Tarime. Lol!
Kama na wewe hutawajengea wazazi wako hapo sawa, ila huwezi kujenga kwenu kisha upinge kusaidia kujenga kwa wazazi wa mkeo, na kwao huyo ni mtoto wao.

Japo hilo linategemea vigezo vingi sana ikiwemo uwezo wa wakwe zako na ndugu wa mkeo. Kwa familia zetu wengi wetu wazazi hawajaweza kuwa na uwezo wa kujenga nyumba nzuri ndio maana mtu mambo yakikaa sawa unajitahidi kuwajengea nyumba nzuri wazazi wako, sasa kama kuna umuhimu wa kujenga kwenu kwa nini isiwe na umuhimu kwa wazazi wa mkeo Bujibuji. Na kama la kuwasaidia kujenga linakua gumu, utawasaidia katika mambo mengine kweli?
 
Back
Top Bottom