Ukweli kuhusu jezi za Simba ni huu

Ukweli kuhusu jezi za Simba ni huu

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Nitalielezea hili jambo kwa ufupi sana, mengine mtajalizia wenyewe. Nimeacha kuongelea sana soka la Tanzania maana wababaishaji ni wengi, kuanzia viongozi, wachezaji, wachambuzi na waandishi wa habari hadi mashabiki.

Kiufupi ni kwamba jezi za Simba zinazoenda kuzinduliwa J5 ni zile zile ambazo Simba ilivaa kipindi hiki cha pre-season.

Kabla haujaja na maneno, "oooh wameona wameharibu na jezi zilizovuja zimepondwa wakaamua kubadili gia", fahamu huu ndiyo ulikuwa mpango wa Simba toka mwanzo walipozindua zile jezi.

Ndiyo maana walizindua jezi tatu, home, away na third kit. Sasa jiulize pre-season unahitaji jezi zote hizo kwa ajili gani?

Kuna sababu kadhaa kwa nini waliamua kuzindua jezi mwanzoni mwa pre-season:
  1. Kupata muda wa kuzitangaza. Ingekuwa soko letu linaweza kudhibiti uuzaji wa jezi feki, kuzindua jezi kwenye pre-season na kuacha wachezaji pekee wavae kwa muda fulani ingekuwa ni mbinu bora sana ya kuzitangaza. Ila kwa soko letu, ni ngumu sana. Kwa hiyo unawaambia hizo ni za pre-season na unatoa onyo kali. Muda ukifika unazitoa kwa mashabiki.
  2. Kuepusha utengenezaji wa jezi feki. Kuendelea na point ya kwanza ila kwa upana zaidi. Kwa soko hili ambalo watu ndani ya masaa 24 wanaweza kutengeneza na kusambaza jezi feki, imagine unawapa mwezi mzima wajiandae kutengeneza jezi feki, si ni kujitengenezea bomu? Kwa kusema zile ni za pre-season na kuonya mtu asiyehusika asionekane amevaa mtaani, iliondoa uwezekano wa wahuni kuziingiza sokoni Ila wakati huo huo ameweza kuzitangaza machoni pa mashabiki wa Simba.
Pia amepata muda wa kutosha wa kutest maoni ya watu. Wangeziponda zile, angesema hizi ni za pre-season tu, akazifanyia maboresho. Kwa kutest soko linasemaje, amejua wanataka nini na anaenda kuwapa kitu wanachotaka.

Keshokutwa watasema walisikia maoni ya watu wengi waliosema jezi zile zile za preseason ndiyo zitumike ila huo ndiyo ulikuwa mpango wa toka awali.
 
Nitalielezea hili jambo kwa ufupi sana, mengine mtajalizia wenyewe. Nimeacha kuongelea sana soka la Tanzania maana wababaishaji ni wengi, kuanzia viongozi, wachezaji, wachambuzi na waandishi wa habari hadi mashabiki.

Kiufupi ni kwamba jezi za Simba zinazoenda kuzinduliwa J5 ni zile zile ambazo Simba ilivaa kipindi hiki cha pre-season.

Kabla haujaja na maneno, "oooh wameona wameharibu na jezi zilizovuja zimepondwa wakaamua kubadili gia", fahamu huu ndiyo ulikuwa mpango wa Simba toka mwanzo walipozindua zile jezi.

Ndiyo maana walizindua jezi tatu, home, away na third kit. Sasa jiulize pre-season unahitaji jezi zote hizo kwa ajili gani?

Kuna sababu kadhaa kwa nini waliamua kusema zile jezi ni za pre-season:
  1. Kupata muda wa kuzitangaza. Ingekuwa soko letu linaweza kudhibiti uuzaji wa jezi feki, kuzindua jezi kwenye pre-season na kuacha wachezaji pekee wavae kwa muda fulani ingekuwa ni mbinu bora sana ya kuzitangaza. Ila kwa soko letu, ni ngumu sana. Kwa hiyo unawaambia hizo ni za pre-season na unatoa onyo kali. Muda ukifika unazitoa kwa mashabiki.
  2. Kuepusha utengenezaji wa jezi feki. Kuendelea na point ya kwanza ila kwa upana zaidi. Kwa soko hili ambalo watu ndani ya masaa 24 wanaweza kutengeneza na kusambaza jezi feki, imagine unawapa mwezi mzima wajiandae kutengeneza jezi feki, si ni kujitengenezea bomu? Kwa kusema zile ni za pre-season na kuonya mtu asiyehusika asionekane amevaa mtaani, iliondoa uwezekano wa wahuni kuziingiza sokoni Ila wakati huo huo ameweza kuzitangaza machoni pa mashabiki wa Simba.
Pia amepata muda wa kutosha wa kutest maoni ya watu. Wangeziponda zile, angesema hizi ni za pre-season tu, akazifanyia maboresho. Kwa kutest soko linasemaje, amejua wanataka nini na anaenda kuwapa kitu wanachotaka.

Keshokutwa watasema walisikia maoni ya watu wengi waliosema jezi zile zile za preseason ndiyo zitumike ila huo ndiyo ulikuwa mpango wa toka awali.
Jtano haiko mbali tuone kama ulichosema ni kweli
 
Utoto+ushamba pia.
Hicho kinafasi walichoweka huo ujinga si Bora wangetafuta Kampuni ikae hapo wapate hela za tofali?
Umeongea pwenti ya maana sana

Sasa ahmed Ally si angekanusha tu leo

Oya wewe kolo nasikia mlisepa

Jtano haiko mbali tuone kama ulichosema ni kweli
1000118327.jpg

Ila hata hizi zilizovuja ni kali sana. Tatizo zimepigwa picha kimkakati sana utadhani ziko mahabusu ya Ukonga.
 
Sasa kama ni hizi mbona nzuri tu
Nyekundu ni nzuri ila angalia picha hizo jinsi zinavyotofautiana ila kwenye nyeupe, mnyama anaonekana vizuri zaidi na hajazibwa na logo ya betway.

Tofauti nilizoona ni pamoja na logo ya Betway haipo sehemu moja, kola hazifanani, logo ya Diadora nyingine ina logo ya maneno nyingine ni alama, kwenye bega pia, nk.
 
Jezi zozote zitakazokuja zitabamba, ni nzuri sana; za pre-season na zilizoonekana kama zimevuja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom