Ukweli kuhusu Dr. Slaa

wazo la el kujisafisha naliunga mkono. lkn km kweli anakipenda chama na taifa y ajitoe???? kuna ubaya gan el akigombea? as long as hata yy alitoka ccm na akapewa nafac agombee. ooooh siasa. upuuuz mtupu..... nampenda sla bt kura yangu kwa ukawa ipo palepale. wananch tushakubaliana na hiyo hali viongoz msituvuruge. i wish slaa angekua mgombea mwenza.



kwanini usingesema I wish lowassa angekuwA mgombea mwenza? shida ninayopata ki chwani ni yy kuweka sharti la kutokugombea ikiwa atakuwa na kura ya maoni. lkn amevunja hats katiba kwa pesa yake. Mimi in mwanachadema ila simpendi tu lowassa.
 
Slaa amekuwa sooo selfish ni mbayaaa sanaaa, aangalie masilahi ya chama kwanza.
Hata hivyo mwenyekiti Mbowe au mwenyekiti yoyote yule ni ngumuuuu kumridhishaa kila mtu.
Wengi wape bwana.
Mbona yeye aliacha upadri akapokelewa uraiani, asituzenguwe bwana.
 
Madai ya Mbowe kupewa fedha na EL. Yapo madai kuwa Mbowe amehongwa sh. bil 12 ili kumpokea EL. Fedha hizi ameziweka kwenye akaunti yake binafsi na amewawia kidogo wale aliowaona wanaweza kumchallenge. baadhi ya watu waliopata mgao ni wajumbe wa kamati kuu ili kuwaziba mdomo. na si wajumbe wote bali wale wachache viherehere. baadhi yao ni Godbless Lema (anadaiwa kupokea milioni 120), Peter Msigwa (mil 135), Tundu Lissu (mil 180), Salum Mwalimu (Mil 180).

Nilihisi tu kuwa ni ngumu sana kwa Lisu ,Msigwa kukubali kirahisi kumpokea Lowasa ,kumbe wamepokea hongo? Upinzani unajiua wenyewe
 
Yes, nimeumia Dr kukaa pembeni nadhini na wapenda Siasa wote bila kujali vyama,kama mnakumbuka wakati anaombwa kugombea Urais alitoa mashrti. Moja wapo ni kupewa mshahala wa mbunge 10m plus na wa ukatibu.sasa kuja kwa Edo anakosa hiyo 10 wazee kwa kiasi kikubwa ilikuwa mzigo kwa CDM, kumbuka kura za Maoni zishapita ubunge bai bai kikubwa labda anabaki na ukatibu mkuu wa chama ambao kisiasa kwake sidhani kama unamaana sana asee. Natoa hoja
 
Yes, nimeumia Dr kukaa pembeni nadhini na wapenda Siasa wote bila kujali vyama,kama mnakumbuka wakati anaombwa kugombea Urais alitoa mashrti. Moja wapo ni kupewa mshahala wa mbunge 10m plus na wa ukatibu.sasa kuja kwa Edo anakosa hiyo 10 wazee kwa kiasi kikubwa ilikuwa mzigo kwa CDM, kumbuka kura za Maoni zishapita ubunge bai bai kikubwa labda anabaki nabukatibu mkuu wa chama ambao kisisa kwake sidhani kama unamaana sana asee
Hayo ni mawazo yako...
 
Teh Teh ziara ya mwanza ilimpa matumaini hewa Dr.W.Slaa akadhani ameshakuwa Rais ndio maana alikuwa ana ruka ruka kwenye gari!
 
Last edited by a moderator:
Yes, nimeumia Dr kukaa pembeni nadhini na wapenda Siasa wote bila kujali vyama,kama mnakumbuka wakati anaombwa kugombea Urais alitoa mashrti. Moja wapo ni kupewa mshahala wa mbunge 10m plus na wa ukatibu.sasa kuja kwa Edo anakosa hiyo 10 wazee kwa kiasi kikubwa ilikuwa mzigo kwa CDM, kumbuka kura za Maoni zishapita ubunge bai bai kikubwa labda anabaki na ukatibu mkuu wa chama ambao kisiasa kwake sidhani kama unamaana sana asee. Natoa hoja

Lowasa hana shida na ukatibu mkuu wa Chadema,, Slaa ataendelea tu kuwa katibu mkuu, tatizo ni mchumba wake anautaka ufirst lady
 
Teh Teh ziara ya mwanza ilimpa matumaini hewa Dr.W.Slaa akadhani ameshakuwa Rais ndio maana alikuwa ana ruka ruka kwenye gari!

Slaa amepigwa bao la kisigino dakika za majeruhi.. Mchumba wake Josefin amechanganyikiwa haelewi kitu anataka ufirst lady tu
 
Last edited by a moderator:
Yes, nimeumia Dr kukaa pembeni nadhini na wapenda Siasa wote bila kujali vyama,kama mnakumbuka wakati anaombwa kugombea Urais alitoa mashrti. Moja wapo ni kupewa mshahala wa mbunge 10m plus na wa ukatibu.sasa kuja kwa Edo anakosa hiyo 10 wazee kwa kiasi kikubwa ilikuwa mzigo kwa CDM, kumbuka kura za Maoni zishapita ubunge bai bai kikubwa labda anabaki na ukatibu mkuu wa chama ambao kisiasa kwake sidhani kama unamaana sana asee. Natoa hoja

Mwache kipenzi wetu .yuko likizo .
 
Teh Teh ziara ya mwanza ilimpa matumaini hewa Dr.W.Slaa akadhani ameshakuwa Rais ndio maana alikuwa ana ruka ruka kwenye gari!

Anway sina cha kufanya....ninaumia vibaya mno kwa dhihaka kama hizi kwa mzee wetu mpendwa....ninaukika mzee wetu hana tamaa kiasi hicho....Mungu msaidie sana mzee wetu huko aliko....mateso yake mateso yetu!!!!
 
Binafsi ninauheshimu sana msimamo wa Dr Slaa; Na sikuwahi kuamini hata siku moja kuwa Mbowe anaweza kumkaribisha EL CDM bila kwanza kuwa na masilahi ya namna fulani. Ni kweli EL ana following kubwa hasa vijijini lakini alipaswa kujisafisha kwanza. hii haraka haraka ya Mbowe and Co. inaleta wasiwasi sana. Yaani tupoteze watu makini ndani ya CDM ili tupate makapi ya CCM!!!!

EL alipaswa kujisafisha kwanza

Ana following kubwa?kama sijaelewa au ndio kiingereza new.
 
Mwaka huu myanyooka tu wazee wa kijani na njano, mtajiita majina yote, mara watafiti, wanasheria, makada, wachambuzi n.k... Sisi kazi yetu ni moja tu: kuhakikisha CCM inatoka mdarakani.

Waswahili walisema mfamaji, haishi kuandika thread zakutapata Jf...

Tulieni dawa iwaingie taratiibu kabisa...

m2kutu,

Mimi nadhani umekosea. Ungejibu hoja za mleta hoja. Si kila anayetoa mawazo tofauti na yako ni mfa maji. Dr Slaa ni mtu anayeheshimika sana ktk jamii ya Tanzania kuliko mwanasiasa yeyote hapa nchini iwe CCM au Upinzani. Kama yaliyoandikwa ni kweli, basi tambua ya kuwa UKAWA itapoteza na heshima yake.

ASM
 

Taharuki imetanda juu ya wapi alipo Katibu mkuu wa Chadema Dr.Wilbroad Slaa. kila mtu anazungumza lake kwa kadri anavyoelewa. wengine wakisema yupo kwenye maandalizi ya vikao vya kamati kuu na wengine wakisema amejificha kwa sababu hakubaliani na maamuzi ya kumleta EL kwenye chama.

Mimi kama kada wa chadema wa muda mrefu na mwanasheria mzoefu nimefanya utafiti na nimejiridhisha bila shaka yoyote kuwa hali si shwari ndani ya chadema licha ya juhudi mbalimbali zinazofanywa kuonesha kuwa hakuna tatizo.

Ukweli ni upi? Ukweli ni kuwa Dr.Wilbroad Slaa hakubaliani na maamuzi yaliyofanywa na kamati kuu ya Kumleta EL na kumpa nafasi ya kugombea Urais bila kufanya utafiti wa kutosha. Slaa anadai kuwa maamuzi haya ni ya haraka mno na chama kilitakiwa kijitafakari zaidi kabla ya kumpa ridhaa ya kugombea Urais.

Ikumbukwe siku ya jumapili tar.26 wakati UKAWA wamefanya kikao cha mwisho na EL Dr.Slaa alikuwepo na baada ya hapo akapotea kabisa na hajaonekana hadharani hadi leo.


Ukweli ni kwamba ndani ya kikao kile chs jumapili Slaa alionesha msimamo wake juu ya EL na kudai kuwa watanzania hawatatuelewa wakituona tukipita kumsafisha mtu yuleyule tuliyemchafua awali.

Hivyo Slaa akatoa masharti mawili makubwa. La kwanza ni EL aitishe Press na ajisafishe mwenyewe kabla hajatangaza kuja UKAWA. Aruhusu waandishi wamuulize maswali yote kuhusu Richmond na kashfa nyingine ikiwemo umiliki wa jengo la Ubalozi wa S.Africa na EL ajibu hoja zote kwa maelezo ya kueleweka. Sharti la pili la Slaa ni kuwa EL asupewe nafasi ya kugombea urais kwa sasa kwani ni ngumu kupima dhamir yake kama ni ya kweli. Slaa akapendekeza EL aje CHADEMA na aisaidie UKAWA kuchukua dola bila kugombea Urais.

Lakini Mbowe akampinga sana Slaa na akasema Katibu mkuu hawezi kuweka "ultimutum" ya EL kujiunga na chadema. Mbowe akapuuza mawazo ya Slaa na akaagiza mchakato wa kumpokea uanze mara moja na kesho yake Mbatia akaambiwa atoe tamko la kumkaribisha EL UKAWA.

Hali hii ilimfanya Slaa kujihisi mnyonge na aliyepuuzwa. akahisi hathaminiki ndani ya chama licha ya mchango mkubwa alioutoa kukijenga chadema. jambo la ajabu Mbowe alipopelekewa taarifa hizo alijibu kwa kejeli kuwa liwalo na liwe. yani yuko tayari kumpoteza Slaa na kumkumbatia EL.

Haikujulikana wazi Mbowe ana maslahi gani katika hili la EL na kwanini aamue kuwa na msimamo mkali hivyo wa kumtetea EL.

Inadaiwa tangu jumapili Slaa alipoachana na viongozi wenzie wa UKAWA hadi sasa yupo ndani hajatoka na hakuna mgeni anayeruhusiwa kumuona. Anautumia muda huu kusali na kushauriana na marafiki zake kwa njia ya simu (wengi ni maaskofu) juu ya nini afanye katika kipindi hiki.

Wengi wamemshauri aachane na siasa na ajiuzulu nafasi yake ya SG ndani ya chadema wazo ambalo limeungwa mkono na mkewe Josephine na baadhi ya watu wenye misimamo mikali.

Baada ya ushauri huu mkewe wa Slaa ameonekana kufurahia na ameanza kuelezea kwenye mitandao ya kijamii. Jsna kupitia kundi la Nyakahoja la whatsapp Josephine alisema mumewe ameteseka sana na chama hiki na amekitoa mbali sana. Dr.Slaa alivunjika mkono na hadi sasa ana ulemavu wa kudumu kwa sababu ya kuitetea chadema. yeye mwenyewe alipigwa na kuharibiwa mimba mwaka 2011 kwa sababu ya chadema halafu leo wanapuuzwa kama vile si chochote ndani ya chama.

Anasema ni afadhali Mbowe angesikiliza ushauri wa Slaa wa EL kujisafisha kwanza kabla hajaja chadema maana kuja bila kujisafisha ni kuwaweka viongozi wote wa chadema kwenye mtego.

Madai ya Mbowe kupewa fedha na EL. Yapo madai kuwa Mbowe amehongwa sh. bil 12 ili kumpokea EL. Fedha hizi ameziweka kwenye akaunti yake binafsi na amewawia kidogo wale aliowaona wanaweza kumchallenge. baadhi ya watu waliopata mgao ni wajumbe wa kamati kuu ili kuwaziba mdomo. na si wajumbe wote bali wale wachache viherehere. baadhi yao ni Godbless Lema (anadaiwa kupokea milioni 120), Peter Msigwa (mil 135), Tundu Lissu (mil 180), Salum Mwalimu (Mil 180).

Pesa hizi ndizo zinazodaiwa kuwafumba macho kamati kuu na kuamua kumpitisha EL bila kufikiri mara mbili. Kitu cha ajabu kamati kuu imefunga dirisha la kuchukua fomu na kusema eti kamati kuu inamuunga mkono Lowassa tu.

Huu ni ujinga ambao hata CCM haiwezi kuufanya. Kamati kuu inatakiwa kuwa neutral. kamati kuu haitakiwi kuwa na mgombea. kamati kuu haitakiwi kuzuia watu kuchuku fomu. acha wachukue wengi kadri iwezekanavyo halafu wachujwe abaki mmoja.

Kama EL anajiamini yeye ni bora zaidi na ana nguvu zaidi kwanini anaitumia kamati kuu kuzuia watu wasichukue fomu? Siku chache zilizopita watu walilalamikia kamati kuu ya CCM kuwa ilikua na mgombea wake mbona hawaoni hili la kamati kuu ya chadema?

Ikiwa madai haya ya kuhongwa kamati kuu ni ya kweli basi chadema inaelekea ukingoni katika siasa za nchi hii. jambo la ajabu viongozi wanaodaiwa kuhongwa akiwemo Mbowe hawajakanusha habari hizi. halafu wanatuma ujumbe kw Slaa eti wakamsihi asiondoke. wajumbe wote waliotumwa wakaishia getini na hawakufunguliwa mlango. mlitegemea mfunguliwe mlango wakati kuna madai mmehongwa na hamjakanusha? kanusheni kwanza ndio muende kumuona Slaa. Au mnataka mkamhonge na yeye? Kama msipokanusha habari hizo mkienda mtafungiwa tena nje maana nyumbani kwa Slaa hakitaingia chochote kilicho kichafu.

Response ya Chadema. ni kama vile hawajali yanayoendelea. na bahati mbaya zaidi vijana wa chadema wameanzisha movement ya kumtukana Josephine kuwa yeye ndio anamponza mumewe. kwenye mtandao wa jamiiforums, facebook ma magroup ya whatsapp wanamtukana sana.

kwenye group moja la wabunge wa chadema wameanzisha movement iitwayo "Josephine Bring Back our Dr". wengine wanamwita mwanamke mpumbavu, wengine wanasema ana hasira ya kukosa ufirst lady, lakini wengine wamefika mbali na kudai anatumiwa na TISS na CCM.

Kimsingi madai yote hapo juu hayana mashiko. Josephine hatumiwi na TISS wala CCM. Hana uchungu wa kukosa ufirst lady wala nini. anachofanya ni kutetea haki ya mumewe. haki ya kuthaminiwa, haki ya kuheshimiwa, haki ya kutoa mawazo yake na kusikilizwa.

Hivi mumeo anapuuzwa kwenye vikao vikubwa vya maamuzi halafu unaambiwa waliompuuza wamehongwa fedha na hawajakanusha habari hizo, halafu ukimtetea mumeo unaambiwa unatumika na TISS. this is ridiculous.

Hakuna cha TISS wala CCM mchawi wa chadema ni chadema wenyewe na mchawi wa ukawa ni chadema. Hizi porojo za TISS ni mbinu inayotumika ili Slaa akiamua kutangaza msimamo wake ionekane anatumiwa na CCM. Chadema acheni siasa za kitoto. hivi Slaa aliyepigania chadema zaidi ya miaka 20 akitoa sadaka maisha yake kwenu ndio wa kutumika na TISS leo aache kutumika huyo EL aliyekuja jana? this is very interesting. chadema kitaingia katika rekodi za dunia za kuwa chama cha kwanza kumtilia shaka mwanachama wake wa miaka 20 na kumuamini mwanachama wa siku moja.

Nini kifanyike? Jambo linaloweza kufanyika na kusaidia kuiokoa chadema na UKAWA kwa ujumla ni mediation. zitafutwe mbinu nzuri za kukutana na Slaa na kuongea nae. aeleze yanayomhusu na chama kioneshe concern ya kuyatatua.

pia kwa kuwa Josephine anaonekana kuwa na nguvu kubwa sana kwa Slaa hivi sasa ni bora Watafutwe wanawake wenye heshima ndani ya chama wakaongee nae. kwa mfano Mama Regina Lowassa, mama Ntagazwa na mama Mbatia waende kumuona mwanamke mwenzao waongee nae. hii itasaidia kupunguza hasira za huyu mama maana tangu juzi anatukanwa mitandaoni akidaiwa ndiye anayemzuia Slaa.

Ni vizuri mambo haya yafanyike mapema maana taarifa zilizopo ni kuwa kufikia wiki ijayo kama chama kitakua hakijatoa msimamo kuhusu Slaa basi yeye atatangaza msimamo wake wa kujiuzulu wadhifa wake chadema na kuamua kuachana na siasa kabisa. kisa wataondoka nchini yeye na familia yake kwenda Italia ambapo ataishi huko kwa miaka mitano kabla ya kurudi nchini na kumalizia maisha yake Karatu. mipango ya Slaa kwenda kuishi Italia kwa miaka mitano inaratibiwa na shirika mija la kiroho la kanisa katoliki na maandalizi yanaendelea vizuri.

Hivyo basi ni vema kazi hii ikafanywa mapema na kwa umakini ili tusivuruge kazi yote ya kuijenga Ukawa na kuujenga upinzani nchini. ukweli ni kuwa Slaa akiamua kujiuzulu siasa za upinzani zitapoteza uelekeo na tutashindwa vibaya kwenye uchaguzi mkuu kuanzia udiwani, ubunge hata urais. maana yake ni kuwa kazi yote iliyofanyika kuujenga upinzani inabomolewa siku moja na kuifanya CCM izidi kushamiri. na ikiwa Slaa ataondoka itachukua miska zaidi ya 100 kupata upinzani mwingine wenye nguvu kama huu. hivyo basi juhudi za haraka zinatakiwa.

Mwandishi wa makala haya ni ndugu A.N Chilongola, mwanachama wa chadema na mkurugenzi wa kampuni ya uwakili ya Chilongola &Advocates iliyopo Mabibo
Dar.anchilongola@gmail.com

I fully agree with you Sir

We can
 
Dr Slaa alikuwa anapiga siasa kwa dhati akitaka kuwasaidia watanzania. Wapo wanasiasa wachache nchi hii wa mfano wake
 
Back
Top Bottom