Richard H. George
Member
- Jul 11, 2015
- 57
- 19
tatizo mbowe ameweka pesa mbele
Ili tuwe Wazalendo wa kweli ktk nchi yetu hii Tanzania, tunapaswa tuwe wakweli.
Inaweza kuwa ni kweli kuwa mh. Mbowe akawa kapewa kweli pesa mnazomtuhumu, lkn kusema ukweli, hayupo mwenye ushahidi kwa hayo myasemayo au mnayomnenea huyo. Lkn najiuliza, mbona hatuongelei zile fedha zilizokamatwa kule Dodoma, kule Kilimanjaro, kule kwa Nape na sehemu nyingine nyingi zinazowahusu maccm?
Au ni kwa vile nadhani, uozo huo ukitendeka ndani ya ccm ni mafuta tena yenye harufu nzuri kwa wahusika; isipokuwa hata pale ambapo hatuna ushahidi ili mradi tu tumefikiria hivyo yakiwa nje yetu, ndo tunakuwa na ujasiri wa kusema tu tunavyoweza?
Tuweni wakweli hata yale tunayoyafanya sisi wenyewe, kama kweli tunachukia masuala yote ya rushwa?
Tena mbona hatuongelei zile ngumi tulizotwangana kila kona ya nchi wakati wa zoezi la kura za maoni lililofanyika trh 01/08/2015?
Poleni sana!