Ukraine yapokea miili ya wanajeshi wake waliouawa Urusi

Ukraine yapokea miili ya wanajeshi wake waliouawa Urusi

The Zanzibar Echo

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2025
Posts
490
Reaction score
837
Ukraine imepokea miili 1,212 kutoka Urusi ya wanajeshi wake waliouwawa wakati wa vita vilivyodumu miaka mitatu kati ya majirani hao wawili.

Wanajeshi hao wanadaiwa kuuwawa katika mapigano kwenye jimbo la Kursk pamoja na maeneo mengine ya Ukraine ya Kharkiv, Luhansk, Donetsk, Zaporizhzhya na Kherson.

Taasisi inayoshughulikia wafungwa wa kivita mjini Kiev, imesema kuachiwa kwa miili hiyo kumejiri baada ya siku kadhaa za mvutano.

Urusi imekuwa ikiishutumu Ukraine kukataa kuchukua miili ya wanajeshi wake na kuitaka kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa kati ya pande hizo hasimu katika mazungumzo yaliyofanyika mjini Istanbul mwanzoni mwa mwezi huu.

Urusi ilisafirisha miili hiyo kwa makabidhiano mwishoni mwa juma lakini Ukraine ikasema hakuna tarehe ya makabidhiano iliyofikiwa.

Makubaliano ya Istanbul yalijumuisha kurejeshwa kwa miili ya wanajeshi 6000 kutoka Urusi kwenda Ukraine. Haijawa wazi iwapo Urusi nayo itapokea miili ya wanajeshi wake kutoka Ukraine.
 
  • Tarehe ya mabadilishano
  • Urusi
  • Ukraine
  • June 22
  • 374
  • 365
  • March 2024
  • 29
  • 121
  • April 24
  • 23
  • 99
  • Agosti 24
  • 38
  • 250
  • Oktoba 24
  • 89
  • 501
  • Novemba 24
  • 37
  • 563
  • Desemba 24
  • 42
  • 501
  • Januari 2025
  • 49
  • 757
  • Februari 2025
  • 45
  • 757
  • Machi 2025
  • 43
  • 909
  • April 2025
  • 41
  • 909
  • May 2025
  • 34
  • 909
Aisee Ukraine wanakufa
 
Duniani kote watu wakawa na mindset kama zako sijui dunia itakuwaje?
Ukimaliza kujiuliza swali hilo jiulize pia duniani kote watu wakiwa na mindset kama zako wewe na wale wenzio akina lucas msambwanda, tlaahtlaah, jingalao, chinembe, choice variable nk za kufurahia wakati majeshi hayo yakitumika ovyo kuumiza watu badala ya kuwalinda dunia itakuwaje?

Nasisitiza tena, sijawahi kuielewa kazi ya jeshi tangu enzi hizo za wafalme waliotajwa kwenye maandiko hadi leo hii, maana wao hutumika kwa maslahi mapana ya wenye mamlaka. Wataua na kuuawa ovyo kisa tu wenye mamlaka waliokaa kwenye viyoyozi wameshindwa kukubaliana, watatumika kunyanyasa wapinzani na watu wengineo ili tu kulinda keki ya wanasiasa nk.

Kwani Urusi na Ukraine mgogoro wao hautatuliki kabisa mezani hadi leo hii wakabidhiane maelfu ya maiti za vijana wao huku kukiwa hakuna hata dalili ya makubaliano? Kubwa zaidi waliotibuana wao bado wapo hai hawajawahi kupata hata mchubuko tangu kuanza kwa vita!
 
Back
Top Bottom