pole sana mkuu, lakini kuna kila sababu za mtazamo wako kubadilika SHULE NI KWA AJIRI YA KUPATA ELIMU/UFAHAMU. Hivyo basi ni wajibu wako kutumia ELIMU yako kwa kutenegeneza ajira yako mwenyewe, hapa najua utataka kusema huna mtaji, afu watu wengi wamekariri mtaji ni PESA tu, ndo mana miaka nenda rudi wanajikuta hawasongi mbele, mara nyingi FURSA hupatikana mahala ulipo tambua jamii yako wanahitaji huduma gani then toa huduma hiyo, Ulimwengu huu unaendeshwa na mifumo kadha wa kadha lakini mfumo mama waitwa "CAUSE AND EFFECT"..huwezi kaa nyumbani kisha ukadai ajira ngumu/hazipatikani akati huyo ajira hana kawaida ya kupitia watu majumbani mwao, angalizo usiifananishe Degree/Diploma kama kitu chenye thamani fulani hivi, kwa mtindo huu huwezi fika mbali kwani kiukweli maisha ni ubunifu na hayana kanuni, kwani waweza kuwa Prof au Dr alafu ukawa na maisha duni hata darasa la SABA akakupiga kikumbo. Chukua hatua mkuu umri unakimbia huo..