Uko wapi Wimbo wa Taifa wa Tanganyika?



Fungua hapa File:Flag of Tanganyika.svg - Wikimedia Commons uione bendera ya TANGANYIKA iliyopandishwa kileleni mwa mlima Kilimanjaro usiku wa manane Tar 9 Desemba 1961. Hakuna haja ya kutafuta bendera nyingine maana itaonekana kama ni Taifa jipya wakati ni kongwe kwa zaidi ya miaka 50 sasa.


 
Unaitwa God save our Queen!

God save our gracious Queen
Long live our noble Queen
God save the Queen!Send her victorious,Happy and glorious,Long to reign over us:God save The Queen!




duh hii katiba mpya italetaniza na mengine.
 
Kama ingekuwa amri yangu ningeshauri ule wimbo wa "tazama raman utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka...." ni bonge la wimbo

Hatupishani sana, mie ningependekeza ule wa Taanzania x2, Nakupenda kwa moyo woteee....

Badala yake tuimbe Taanganyika x2....Nakupenda kwa moyo woteee...

Tuachane na hii Mungu ibariki Africa mbayo wala haikutungwa na mtanzania.
 
Kama ingekuwa amri yangu ningeshauri ule wimbo wa "tazama raman utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka...." ni bonge la wimbo

Yeah ule ni wimbo mzuri sana, but kuna jina la Karume linatajwa mle. so itabidi LIONDOLEWE!!! MARA MOJA!!!
 
Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanganyika, jina lako ni tamu sana,
Nilalapo nakuota wewe, niamkapo ni heri mama wewe,
Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote!

Huu ndo wimbo wa taifa letu la Tanganyika ambalo siku si nyingi litapata kufufuliwa baada ya miaka 49 ama 50 ya kifo chake.
 
Kama ingekuwa amri yangu ningeshauri ule wimbo wa "tazama raman utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka...." ni bonge la wimbo

Yeah huu wimbo una melody nzuri sana kuliko zingine za kitaifa nilizowahi sikia. Tatizo liko kwenye beti la pili.

tragedy of the commons
 
Habari wanajamvi wenzangu. Mm nina swali nataka kujua. Je Tanganyika ilipopata uhuru kabla ya kuungana na Zanzibar ilikuwa na wimbo wake wa taifa? Maana tangu nakua sijawahi kusikia wimbo wa Tanganyika zaidi ya huu. ...."""" Mungu ibariki Tanzania.....""""" . Naomba mnijulishe watanzania wenzangu.
 
Kila kitu cha Tanganyika kilibatizwa Utanzania. Hivyo penye Tanzania weka Tanganyika na huo wimbo unaoutaka utaupata.
 
Imba wimbo wote wa Tanzania, na kila mahali penye Tanzania weka Tanganyika
 
Kila kitu cha Tanganyika kilibatizwa Utanzania. Hivyo penye Tanzania weka Tanganyika na huo wimbo unaoutaka utaupata.

Ngoja Pinda atuhakikishie ,................. ndiyo nichague Tanganyika ninayoitaka!!
 
Kila kitu kipo ,labda WaCCM wawe wamefisidi na kuuwiba !
 
Kila kitu cha Tanganyika kilibatizwa Utanzania. Hivyo penye Tanzania weka Tanganyika na huo wimbo unaoutaka utaupata.

Kwahiyo ndo kusema kwamba baada ya Tanganyika kupata uhuru huu wimbo wa sasa wa ''Mungu ibariki Tanzania.....''''' ulikuwa wa Tanganyika? Na baada ya kuungana na Zanzibar ukatumika huo huo ila penye Tanganyika wakaweka Tanzania?
 
Kila kitu kipo ,labda WaCCM wawe wamefisidi na kuuwiba !

Wauibe waupeleke wapi? Sijawai hata kusoma kwenye vitabi vua historia. Au ndo kusema baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kila kitu cha Tanganyika kikazikwa?
 
Kwahiyo ndo kusema kwamba baada ya Tanganyika kupata uhuru huu wimbo wa sasa wa ''Mungu ibariki Tanzania.....''''' ulikuwa wa Tanganyika? Na baada ya kuungana na Zanzibar ukatumika huo huo ila penye Tanganyika wakaweka Tanzania?

Naam na hasa ulilenga uwe wa Afrika iliyoungana na Afrika Kusini wakati wa kupigania uhuru walifuata karibu maneno yaliyomo kwenye wimbo huo!
 

Badala ya Tanzania weka Tanganyika - simpo.
 
Mchungaji wa tanganyika anaujua wimbo.muulize atakujuza.rev.mtikila
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…